< Marko 2 >

1 Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu, watu wakasikia kwamba amerudi nyumbani.
A po kilku dniach znowu przyszedł do Kafarnaum i usłyszano, że jest w domu.
2 Hivyo watu wengi wakakusanyika kiasi kwamba hapakubaki nafasi yoyote hata mlangoni! Naye akawahubiria Neno.
I zaraz zeszło się tak wielu [ludzi], że nie mogli się zmieścić nawet przed drzwiami. I głosił im słowo [Boże].
3 Ndipo baadhi ya watu wakaja wakamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne.
Wtedy przyszli do niego, niosąc sparaliżowanego, a niosło go czterech [ludzi].
4 Kwa kuwa walikuwa hawawezi kumfikisha kwa Yesu kwa ajili ya umati wa watu, walitoboa tundu kwenye paa mahali pale alipokuwa Yesu, wakamshusha yule aliyepooza kwa kitanda alichokuwa amelalia.
A gdy nie mogli do niego podejść z powodu tłumu, odkryli dach [nad miejscem], gdzie był [Jezus], wyłamali go i spuścili na dół posłanie, na którym leżał sparaliżowany.
5 Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
A Jezus, widząc ich wiarę, powiedział do sparaliżowanego: Synu, twoje grzechy są ci przebaczone.
6 Basi baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wameketi huko wakawaza mioyoni mwao,
A byli tam niektórzy z uczonych w Piśmie, siedząc i myśląc w swoich sercach:
7 “Kwa nini mtu huyu anasema hivi? Huyu anakufuru! Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
Czemu on mówi takie bluźnierstwa? Któż może przebaczać grzechy oprócz samego Boga?
8 Mara moja Yesu akatambua rohoni mwake kile walichokuwa wanawaza mioyoni mwao, naye akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
A zaraz Jezus, poznawszy w swym duchu, że tak myśleli, powiedział do nich: Czemuż tak myślicie w swoich sercach?
9 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uchukue mkeka wako, uende’?
Cóż jest łatwiej – powiedzieć sparaliżowanemu: Przebaczone są ci grzechy, czy powiedzieć: Wstań, weź swoje posłanie i chodź?
10 Lakini ili mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Yesu akamwambia yule aliyepooza,
Ale żebyście wiedzieli, że Syn Człowieczy ma na ziemi moc przebaczać grzechy – powiedział do sparaliżowanego:
11 “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
Mówię ci: Wstań, weź swoje posłanie i idź do domu.
12 Yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama, akachukua mkeka wake, akatembea machoni pao wote! Jambo hili likawashangaza wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, “Hatujapata kuona jambo kama hili kamwe!”
A on natychmiast wstał, wziął swoje posłanie i wyszedł na oczach wszystkich, tak że wszyscy byli zdumieni i chwalili Boga, mówiąc: Nigdy nie widzieliśmy czegoś takiego.
13 Yesu akaenda tena kandokando ya Bahari ya Galilaya. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akaanza kuwafundisha.
I wyszedł znów nad morze. I przychodził do niego cały lud, a on ich nauczał.
14 Alipokuwa akitembea, akamwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru, akamwambia, “Nifuate.” Lawi akaondoka, akamfuata Yesu.
A przechodząc, zobaczył Lewiego, [syna] Alfeusza, siedzącego w punkcie celnym, i powiedział do niego: Pójdź za mną. A on wstał i poszedł za nim.
15 Yesu alipokuwa akila chakula nyumbani mwa Lawi, watoza ushuru wengi pamoja na “wenye dhambi” walikuwa wakila pamoja naye na wanafunzi wake, kwa maana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimfuata.
Kiedy Jezus siedział za stołem w jego domu, razem z Jezusem i jego uczniami siedziało wielu celników i grzeszników. Było ich bowiem wielu i chodzili za nim.
16 Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa Mafarisayo walipomwona akila pamoja na watoza ushuru na “wenye dhambi,” wakawauliza wanafunzi wake: “Mbona Yesu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
A uczeni w Piśmie i faryzeusze, widząc, że je z celnikami i grzesznikami, mówili do jego uczniów: Cóż to [jest], że on je i pije z celnikami i grzesznikami?
17 Yesu aliposikia haya akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa. Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
A Jezus, usłyszawszy to, powiedział im: Nie zdrowi, lecz chorzy potrzebują lekarza. Nie przyszedłem wzywać do pokuty sprawiedliwych, ale grzeszników.
18 Basi wanafunzi wa Yohana pamoja na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Baadhi ya watu wakamjia Yesu na kumuuliza, “Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”
A uczniowie Jana i faryzeuszy pościli. Przyszli więc i pytali go: Czemu uczniowie Jana i faryzeuszy poszczą, a twoi uczniowie nie poszczą?
19 Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kufunga wakati angali pamoja nao? Wakati bwana arusi bado yuko pamoja nao, hawawezi kufunga.
I odpowiedział im Jezus: Czy przyjaciele oblubieńca mogą pościć, gdy jest z nimi oblubieniec? Dopóki mają ze sobą oblubieńca, nie mogą pościć.
20 Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Siku hiyo ndipo watakapofunga.
Lecz przyjdą dni, gdy oblubieniec zostanie od nich zabrany, a wtedy, w tych dniach, będą pościć.
21 “Hakuna mtu ashoneaye kiraka cha nguo mpya kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, kile kiraka kipya kitachanika kutoka ile nguo iliyochakaa, nayo itachanika zaidi.
Nikt nie przyszywa łaty z nowego sukna do starej szaty, inaczej nowa łata ujmuje [nieco] od starej [szaty] i rozdarcie staje się gorsze.
22 Wala hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, ile divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo hiyo divai itamwagika na viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya.”
Nikt też nie wlewa młodego wina do starych bukłaków, bo inaczej młode wino rozsadza bukłaki i wino wycieka, a bukłaki się psują. Lecz nowe wino należy wlewać do nowych bukłaków.
23 Siku moja ya Sabato, Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wakipita katikati ya mashamba ya nafaka. Walipokuwa wakitembea, wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke.
A gdy Jezus szedł w szabat przez zboża, jego uczniowie zaczęli po drodze zrywać kłosy.
24 Mafarisayo wakamwambia, “Tazama, mbona wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato?”
Wtedy faryzeusze mówili do niego: Spójrz, czemu oni robią w szabat to, czego nie wolno [robić]?
25 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa, wakahitaji chakula?
A on im odpowiedział: Nigdy nie czytaliście, co zrobił Dawid, gdy znalazł się w potrzebie i był głodny, on i ci, którzy z nim byli?
26 Daudi aliingia katika nyumba ya Mungu, wakati Abiathari alikuwa kuhani mkuu, akaila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
Jak wszedł do domu Bożego za Abiatara, najwyższego kapłana, i jadł chleby pokładne, których nie wolno było jeść nikomu oprócz kapłanów, i dał również tym, którzy z nim byli?
27 Kisha Yesu akawaambia, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, lakini si mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
Powiedział im także: Szabat został ustanowiony dla człowieka, a nie człowiek dla szabatu.
28 Hivyo, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
Dlatego Syn Człowieczy jest też Panem szabatu.

< Marko 2 >