< Marko 2 >

1 Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu, watu wakasikia kwamba amerudi nyumbani.
And (He was entering *N(k)O*) again into Capernaum after [some] days (and *k*) it was heard that (in [the] house *N(k)O*) He is.
2 Hivyo watu wengi wakakusanyika kiasi kwamba hapakubaki nafasi yoyote hata mlangoni! Naye akawahubiria Neno.
And (immediately *KO*) were gathered together many so that no more to have space not even [space] at the door, and He was speaking to them the word.
3 Ndipo baadhi ya watu wakaja wakamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne.
And they come bringing to Him a paralytic being carried by four.
4 Kwa kuwa walikuwa hawawezi kumfikisha kwa Yesu kwa ajili ya umati wa watu, walitoboa tundu kwenye paa mahali pale alipokuwa Yesu, wakamshusha yule aliyepooza kwa kitanda alichokuwa amelalia.
And not being able (to bring to *N(k)O*) to Him on account of the crowd they removed the roof where He was and having broken up [it] they let down the pallet (where *N(k)O*) the paralytic was lying.
5 Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
(And *no*) having seen (now *ko*) Jesus the faith of them He says to the paralytic; Son, (are forgiven of you *N(k)O*) the sins (of you. *k*)
6 Basi baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wameketi huko wakawaza mioyoni mwao,
were now some of the scribes there sitting and reasoning in the hearts of them;
7 “Kwa nini mtu huyu anasema hivi? Huyu anakufuru! Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
Why this [man] thus does speak? (He blasphemes! *N(k)O*) Who is able to forgive sins only except one God?
8 Mara moja Yesu akatambua rohoni mwake kile walichokuwa wanawaza mioyoni mwao, naye akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
And immediately having known Jesus in the spirit of Him that thus (they themselves *o*) are reasoning within themselves (He speaks *N(k)O*) to them; Why these things reason you in the hearts of you?
9 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uchukue mkeka wako, uende’?
Which is easier, to say to the paralytic; (Are forgiven of you *N(k)O*) the sins, or to say; (do arise *N(k)(o)*) and do take up the mat of you and do walk?
10 Lakini ili mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Yesu akamwambia yule aliyepooza,
That however you may know that authority has the Son of Man to forgive sins on the earth He says to the paralytic;
11 “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
To you I say; (do arise *N(k)O*) (and *k*) do take up the mat of you and do go to the home of you.
12 Yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama, akachukua mkeka wake, akatembea machoni pao wote! Jambo hili likawashangaza wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, “Hatujapata kuona jambo kama hili kamwe!”
And he arose and immediately having taken up the mat he went forth (before *N(k)O*) all so as for to be amazed all and to glorify God saying that Thus never did we see.
13 Yesu akaenda tena kandokando ya Bahari ya Galilaya. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akaanza kuwafundisha.
And He went forth again beside the sea, and all the crowd was coming to Him, and He was teaching them.
14 Alipokuwa akitembea, akamwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru, akamwambia, “Nifuate.” Lawi akaondoka, akamfuata Yesu.
And passing on He saw Levi the [son] of Alphaeus sitting at the tax booth and He says to him; do follow Me. And having arisen he followed Him.
15 Yesu alipokuwa akila chakula nyumbani mwa Lawi, watoza ushuru wengi pamoja na “wenye dhambi” walikuwa wakila pamoja naye na wanafunzi wake, kwa maana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimfuata.
And (it came to pass *N(k)(o)*) (in the *ko*) reclining of Him in the house of him, that many tax collectors and sinners were reclining with Jesus and with the disciples of Him; there were for many, and (they were following *N(k)O*) Him.
16 Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa Mafarisayo walipomwona akila pamoja na watoza ushuru na “wenye dhambi,” wakawauliza wanafunzi wake: “Mbona Yesu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
And the scribes (*k*) (of the Pharisees *N(k)O*) (*o*) having seen (that *N(k)O*) (he eats *N(k)(o)*) with the sinners and tax collectors were saying to the disciples of Him; (Why [is it] *k*) that with the tax collectors and sinners He eats (and drinks? *KO*)
17 Yesu aliposikia haya akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa. Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
And having heard Jesus says to them: (that *no*) No need have those being strong of a physician but those sick being; Not I came to call [the] righteous but sinners (into repentance. *K*)
18 Basi wanafunzi wa Yohana pamoja na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Baadhi ya watu wakamjia Yesu na kumuuliza, “Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”
And were the disciples of John and the (of the *K*) (Pharisees *N(k)O*) fasting And they come and they say to Him; Because of why the disciples of John and the (disciples *no*) of the Pharisees fast, but Your disciples not fast?
19 Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kufunga wakati angali pamoja nao? Wakati bwana arusi bado yuko pamoja nao, hawawezi kufunga.
And said to them Jesus; Not are able the sons of the bridechamber in which the bridegroom with them is to fast? As long as time they have the bridegroom with (them *N(k)O*) not they are able to fast.
20 Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Siku hiyo ndipo watakapofunga.
Will come however [the] days when may have been taken away from them the bridegroom, and then they will fast in (that *N(K)O*) (*N(k)O*) (day. *N(K)O*)
21 “Hakuna mtu ashoneaye kiraka cha nguo mpya kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, kile kiraka kipya kitachanika kutoka ile nguo iliyochakaa, nayo itachanika zaidi.
(and *k*) No [one] a patch of cloth unshrunk sews on (clothing old; *N(k)O*) lest then except tears away the patch (from *no*) it new from the old, And worse a tear takes place.
22 Wala hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, ile divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo hiyo divai itamwagika na viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya.”
And no [one] puts wine new into wineskins old; lest then except, (will burst *N(k)O*) the wine (new *k*) the wineskins and the wine (is destroyed *N(K)O*) and the wineskins (will perish; *ko*) Instead wine new into wineskins new (must be put. *ko*)
23 Siku moja ya Sabato, Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wakipita katikati ya mashamba ya nafaka. Walipokuwa wakitembea, wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke.
And it came to pass He on the Sabbaths (passing through *NK(o)*) through the grainfields, and the disciples of Him began [their] way to make plucking the heads of grain.
24 Mafarisayo wakamwambia, “Tazama, mbona wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato?”
And the Pharisees were saying to Him; Behold why do they (in *k*) on the Sabbaths that which not is lawful?
25 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa, wakahitaji chakula?
And (he himself *k*) (says *N(k)O*) to them; Surely you did read what did David when need he had and hungered he himself and those with him?
26 Daudi aliingia katika nyumba ya Mungu, wakati Abiathari alikuwa kuhani mkuu, akaila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
How he entered into the house of God in [the days of] Abiathar (the *k*) high priest and the loaves of the presentation ate which not it is lawful to eat only except (for the priests, *N(k)O*) And he gave even to those with him being?
27 Kisha Yesu akawaambia, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, lakini si mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
And He was saying to them; The Sabbath on account of the man was made, (and *no*) not the man on account of the Sabbath.
28 Hivyo, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
So then Lord is the Son of Man also even of the Sabbath.

< Marko 2 >