< Marko 16 >
1 Sabato ilipomalizika, Maria Magdalene, Maria mama yake Yakobo, na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu.
When the Sabbath was over, Mary Magdalene, Mary the mother of James, and Salome bought spices, so that they might go and anoint Jesus' body.
2 Asubuhi na mapema, siku ya kwanza ya juma, mara tu baada ya kuchomoza jua, walikwenda kaburini.
Very early in the morning of the first day of the week, when the sun had risen, they went to the tomb.
3 Njiani wakawa wanaulizana wao kwa wao, “Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe kutoka kwenye ingilio la kaburi?”
On the way, they were saying to one another, “Who will roll the stone away from the entrance of the tomb for us?”
4 Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha kuvingirishwa kutoka pale penye ingilio la kaburi.
But when they arrived, they looked up and saw that the stone, which was very large, had already been rolled away.
5 Walipokuwa wakiingia mle kaburini, wakamwona kijana mmoja aliyevaa joho jeupe akiwa ameketi upande wa kuume, nao wakastaajabu.
As they went into the tomb, they saw a young man sitting on the right side, clothed in a long white robe, and they were alarmed.
6 Yule malaika akawaambia, “Msistaajabu. Mnamtafuta Yesu, Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa. Tazameni mahali walipomlaza.
But he said to them, “Do not be alarmed; you seek Jesus of Nazareth, who was crucified. He is risen; he is not here. Behold, this is the place where they laid him.
7 Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro, kwamba, ‘Anawatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko mtamwona, kama alivyowaambia.’”
Now go tell his disciples and Peter that he is going ahead of you to Galilee. There you will see him, just as he told you.”
8 Hivyo wakatoka, wakakimbia kutoka mle kaburini wakiwa na hofu kuu na mshangao. Nao hawakumwambia mtu yeyote neno lolote, kwa sababu waliogopa.
So they went out and fled from the tomb, and trembling and amazement seized them. But they did not say anything to anyone, for they were afraid.
9 (note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) Yesu alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Maria Magdalene, yule ambaye alikuwa amemtoa pepo wachafu saba.
(note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) In the morning on the first day of the week, after Jesus had risen, he appeared first to Mary Magdalene, from whom he had cast out seven demons.
10 Maria akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Yesu, waliokuwa wanaomboleza na kulia.
She then went and told those who had been with him, while they were mourning and weeping.
11 Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria alikuwa amemwona, hawakusadiki.
But when they heard that he was alive and that she had seen him, they did not believe it.
12 Baadaye Yesu akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine.
After this, Jesus appeared in a different form to two of his followers as they were walking along in the countryside.
13 Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.
They went back and told the others, but they did not believe them either.
14 Baadaye Yesu akawatokea wale wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa wakila chakula. Akawakemea kwa kutoamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao kwa kutosadiki wale waliomwona baada yake kufufuka.
Later Jesus appeared to the eleven as they were reclining at the table, and he rebuked them for their unbelief and hardness of heart, because they had not believed those who had seen him after he had risen.
15 Akawaambia, “Enendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
He said to them, “Go into all the world and preach the gospel to all creation.
16 Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa.
Whoever believes and is baptized will be saved, but whoever does not believe will be condemned.
17 Nazo ishara hizi zitafuatana na wanaoamini: Kwa Jina langu watatoa pepo wachafu; watasema kwa lugha mpya;
And these signs will accompany those who believe: They will cast out demons in my name, they will speak in new tongues,
18 watashika nyoka kwa mikono yao; na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”
they will pick up serpents, and if they drink any deadly poison, it will certainly not harm them; they will lay hands on the sick, and they will get well.”
19 Baada ya Bwana Yesu kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni na kuketi mkono wa kuume wa Mungu.
After the Lord had spoken to them, he was taken up into heaven, and he sat down at the right hand of God.
20 Kisha wanafunzi wake wakatoka, wakahubiri kila mahali, naye Bwana akatenda kazi pamoja nao na kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo.]
Then the disciples went out and preached everywhere, while the Lord worked through them and confirmed the message by the signs that accompanied it. Amen.