< Marko 16 >

1 Sabato ilipomalizika, Maria Magdalene, Maria mama yake Yakobo, na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu.
And, the Sabbath having passed, Mary the Magdalene, and Mary the mother of James, and Salome, bought spices, that, coming, they might anoint him.
2 Asubuhi na mapema, siku ya kwanza ya juma, mara tu baada ya kuchomoza jua, walikwenda kaburini.
And, very early, on the first of the week, they are coming towards the tomb—when, the sun, arose.
3 Njiani wakawa wanaulizana wao kwa wao, “Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe kutoka kwenye ingilio la kaburi?”
And they were saying one to another—Who, shall roll away for us the stone, out of the door of the tomb?
4 Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha kuvingirishwa kutoka pale penye ingilio la kaburi.
And, looking up, they observe that the stone hath been rolled up, —for it was exceeding great.
5 Walipokuwa wakiingia mle kaburini, wakamwona kijana mmoja aliyevaa joho jeupe akiwa ameketi upande wa kuume, nao wakastaajabu.
And, entering into the tomb, they saw a young man, sitting on the right, clothed with a white robe, —and they were greatly alarmed.
6 Yule malaika akawaambia, “Msistaajabu. Mnamtafuta Yesu, Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa. Tazameni mahali walipomlaza.
But, he, saith unto them—Be not alarmed! Jesus, ye are seeking, the Nazarene, the crucified: He hath arisen! he is not here, —See! the place where they laid him!
7 Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro, kwamba, ‘Anawatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko mtamwona, kama alivyowaambia.’”
But go your way, tell his disciples, and Peter—He is going before you into Galilee: there, shall ye yourselves see him, —according as he said unto you.
8 Hivyo wakatoka, wakakimbia kutoka mle kaburini wakiwa na hofu kuu na mshangao. Nao hawakumwambia mtu yeyote neno lolote, kwa sababu waliogopa.
And, going out, they fled from the tomb, for, trembling and transport, were holding them; and, unto no one, said they, anything, for they were afraid.
9 (note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) Yesu alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Maria Magdalene, yule ambaye alikuwa amemtoa pepo wachafu saba.
(note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) And, arising early, on the first of the week, he was manifested, first, unto Mary the Magdalene, from whom he had cast, seven demons.
10 Maria akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Yesu, waliokuwa wanaomboleza na kulia.
She, going her way, bare tidings unto them who had come to be with him, as they were mourning and weeping.
11 Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria alikuwa amemwona, hawakusadiki.
And, they, hearing that he was living, and had been looked upon by her, disbelieved.
12 Baadaye Yesu akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine.
But, after these things, unto two from among them, as they were walking, was he manifested, in a different form, as they were going unto a country place;
13 Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.
and, they, departing, bare tidings unto the rest, —but, even them, they believed not.
14 Baadaye Yesu akawatokea wale wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa wakila chakula. Akawakemea kwa kutoamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao kwa kutosadiki wale waliomwona baada yake kufufuka.
But, afterwards, unto the eleven themselves, as they reclined, was he manifested, and he upbraided their disbelief and hardness of heart, —because, them who had looked upon him when arisen [from among the dead] they believed not;
15 Akawaambia, “Enendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
and he said unto them—Go ye into all the world, and proclaim the glad-message, to the whole creation:
16 Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa.
He that hath believed, and been immersed, shall be saved; but, he that hath disbelieved, shall be condemned:
17 Nazo ishara hizi zitafuatana na wanaoamini: Kwa Jina langu watatoa pepo wachafu; watasema kwa lugha mpya;
Signs, moreover, shall follow, them who have believed, —these: —In my name, shall they cast, demons, out, with tongues, shall they speak, —[and, in their hands, ] they shall take up, serpents;
18 watashika nyoka kwa mikono yao; na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”
And, if, any deadly thing, they have drunk, in nowise, shall it, hurt, them: Upon sick persons, shall they lay, hands, and, well, shall they remain.
19 Baada ya Bwana Yesu kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni na kuketi mkono wa kuume wa Mungu.
The Lord [Jesus], therefore, on the one hand, after talking with them, was taken up into heaven, and sat down on the right hand of God:
20 Kisha wanafunzi wake wakatoka, wakahubiri kila mahali, naye Bwana akatenda kazi pamoja nao na kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo.]
They, on the other hand, going forth, proclaimed on every side, the Lord, co-working, and confirming, the word, through, the closely following signs. OTHERWISE. All the things given in charge unto the companions of Peter, they concisely reported. But, after these things, Jesus also, himself, from east even unto west, sent forth, through them, the sacred and incorruptible proclamation of the age-abiding salvation.

< Marko 16 >