< Marko 16 >

1 Sabato ilipomalizika, Maria Magdalene, Maria mama yake Yakobo, na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu.
And when the sabbath was past, Mary the Magdalene, and Mary the mother of James, and Salome, bought spices, that they might come and anoint him.
2 Asubuhi na mapema, siku ya kwanza ya juma, mara tu baada ya kuchomoza jua, walikwenda kaburini.
And very early on the first day of the week, they came to the tomb at the rising of the sun.
3 Njiani wakawa wanaulizana wao kwa wao, “Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe kutoka kwenye ingilio la kaburi?”
And they said to one another, Who will roll away for us the stone from the door of the tomb?
4 Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha kuvingirishwa kutoka pale penye ingilio la kaburi.
And looking up they see that the stone had been rolled back; for it was very large.
5 Walipokuwa wakiingia mle kaburini, wakamwona kijana mmoja aliyevaa joho jeupe akiwa ameketi upande wa kuume, nao wakastaajabu.
And they entered the tomb, and saw a young man sitting on the right side, clothed in a long white garment; and they were affrighted.
6 Yule malaika akawaambia, “Msistaajabu. Mnamtafuta Yesu, Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa. Tazameni mahali walipomlaza.
But he saith to them, Be not affrighted; ye seek Jesus the Nazarene who was crucified; he hath risen; he is not here; behold the place where they laid him.
7 Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro, kwamba, ‘Anawatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko mtamwona, kama alivyowaambia.’”
But go, tell his disciples and Peter, that he is going before you into Galilee; there ye will see him, as he said to you.
8 Hivyo wakatoka, wakakimbia kutoka mle kaburini wakiwa na hofu kuu na mshangao. Nao hawakumwambia mtu yeyote neno lolote, kwa sababu waliogopa.
And they went out, and fled from the tomb; for trembling and amazement had seized them, and they said nothing to any one; for they were terrified.
9 (note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) Yesu alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Maria Magdalene, yule ambaye alikuwa amemtoa pepo wachafu saba.
(note: The most reliable and earliest manuscripts do not include Mark 16:9-20.) (The remaining twelve verses, according to Tischendorf and others, made originally no part of Mark's Gospel. As the passage was added very early, however, since it is referred to by Irenaeus in the latter part of the second century, it is here given, as an appendix.) [[And having risen early, on the first day of the week, he appeared first to Mary the Magdalene, out of whom he had cast seven demons.
10 Maria akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Yesu, waliokuwa wanaomboleza na kulia.
She went and reported it to those who had been with him, who were mourning and weeping.
11 Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria alikuwa amemwona, hawakusadiki.
And they, when they heard that he was alive, and had been seen by her, did not believe.
12 Baadaye Yesu akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine.
After this, he manifested himself in another form to two of them as they walked, going into the country.
13 Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.
And they went and reported it to the rest; and even them they did not believe.
14 Baadaye Yesu akawatokea wale wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa wakila chakula. Akawakemea kwa kutoamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao kwa kutosadiki wale waliomwona baada yake kufufuka.
Afterward he manifested himself to the eleven themselves, as they were reclining at table, and upbraided them with their unbelief and hardness of heart, because they did not believe those who had seen him after he had risen.
15 Akawaambia, “Enendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
And he said to them, Go ye into all the world, and preach the glad tidings to the whole creation.
16 Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa.
He that believeth and is baptized will be saved; but he that doth not believe will be condemned.
17 Nazo ishara hizi zitafuatana na wanaoamini: Kwa Jina langu watatoa pepo wachafu; watasema kwa lugha mpya;
And these signs will accompany believers: In my name they will cast out demons; they will speak with new tongues;
18 watashika nyoka kwa mikono yao; na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”
they will take up serpents; and if they drink any deadly thing, it will not hurt them; they will lay their hands on the sick, and they will recover.
19 Baada ya Bwana Yesu kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni na kuketi mkono wa kuume wa Mungu.
So then, the Lord, after he had spoken to them, was taken up into heaven, and sat down on the right hand of God;
20 Kisha wanafunzi wake wakatoka, wakahubiri kila mahali, naye Bwana akatenda kazi pamoja nao na kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo.]
and they went forth, and preached every where, the Lord working with them, and confirming the word by the signs which followed it.]]

< Marko 16 >