< Marko 15 >

1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
Muy de mañana, los principales sacerdotes consultaron con los ancianos, los escribas y el Tribunal Supremo. Ataron a Jesús, [lo] llevaron y [lo] entregaron a Pilato.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
Pilato le preguntó: ¿Eres Tú el Rey de los judíos? Le respondió: Tú [lo ]dices.
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
Los principales sacerdotes lo acusaban mucho.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
Pilato le preguntó otra vez: ¿Nada respondes? Mira de cuántas cosas te acusan.
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
Pero Jesús nada más respondió, de tal modo que Pilato se asombró.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
En cada fiesta [Pilato] les soltaba un preso: el que pidieran.
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
Un hombre llamado Barrabás estaba preso con los sublevados que habían cometido un homicidio en una revuelta.
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
Cuando la multitud pidió a Pilato que hiciera lo que siempre les hacía,
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
Pilato les preguntó: ¿Quieren que les suelte al Rey de los judíos?
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
Porque entendía que los principales sacerdotes lo habían entregado por envidia.
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
Pero los principales sacerdotes incitaron a la multitud para [pedirle] que más bien les soltara a Barrabás.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
Pilato les volvió a preguntar: ¿Qué hago al Rey de los judíos?
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
Ellos gritaron otra vez: ¡Crucifícalo!
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
Pero Pilato les preguntaba: ¿Pues qué mal hizo? Y ellos gritaron aún más: ¡Crucifícalo!
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
Pilato, entonces, quiso satisfacer a la multitud y les soltó a Barrabás. Azotó a Jesús y lo entregó para que lo crucificaran.
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
Entonces los soldados lo llevaron a la residencia oficial del gobernador y reunieron a toda la tropa.
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
Lo vistieron de púrpura, trenzaron una corona de espinas y se la pusieron [en la cabeza].
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
Lo saludaban: ¡Honores, Rey de los judíos!
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
También le golpeaban la cabeza con una caña, lo escupían y se arrodillaban para rendirle homenaje.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
Cuando lo ridiculizaron, le quitaron la ropa de púrpura, lo vistieron con su ropa y lo sacaron para crucificarlo.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
Obligaron a uno que pasaba, quien llegaba del campo, Simón cireneo, el padre de Alejandro y Rufo, a llevar la cruz de Jesús.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
Lo llevaron al Gólgota, que significa: Lugar de una Calavera.
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
Le dieron vino mezclado con mirra, pero no tomó.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
Lo crucificaron y se repartieron sus ropas para lo cual echaron suerte a fin de saber qué llevaría cada uno.
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
Eran las nueve de la mañana cuando lo crucificaron.
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
Entonces escribieron la acusación contra Él encima de la cruz: El Rey de los judíos.
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
Crucificaron con Él a dos ladrones, uno a su derecha y otro a su izquierda.
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
Los que pasaban lo ofendían, meneaban sus cabezas y decían: ¡Bah! ¡El que derriba el Santuario y [lo] reedifica en tres días,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
baja de la cruz, sálvate a Ti mismo!
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
Del mismo modo, los principales sacerdotes y los escribas se burlaban y se decían unos a otros: Salvó a otros. Él mismo no puede salvarse.
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
¡El Cristo, el Rey de Israel! Baja ahora de la cruz para que veamos y creamos. También lo insultaban los que fueron crucificados con Él.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
Cuando llegó el mediodía hubo oscuridad en toda la tierra hasta las tres de la tarde.
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
A esa hora Jesús exclamó a gran voz: Eloi, Eloi, ¿lema sabajtani? que significa: Dios mío, Dios mío, ¿por qué me desamparaste?
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
Al oírlo algunos de los presentes, decían: ¡Mira, llama a Elías!
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
Entonces alguien corrió y empapó una esponja con vinagre, la sujetó a una caña, le dio a beber y dijo: Dejen, veamos si Elías viene a bajarlo.
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
Pero Jesús, con una fuerte exclamación, expiró.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
El velo del Santuario fue rasgado en dos, de arriba abajo.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
El centurión destacado frente a Él, al ver cómo había expirado, exclamó: ¡Verdaderamente este Hombre era Hijo de Dios!
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
También estaban unas mujeres que miraban de lejos, entre quienes estaban María Magdalena, María, la madre de Jacobo el menor y de José, Salomé,
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
y muchas otras que subieron con Él a Jerusalén, las cuales lo seguían y le servían cuando estaba en Galilea.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
Al llegar la noche, puesto que era Preparación, es decir, víspera del sábado,
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
cuando llegó José de Arimatea, miembro prominente del Tribunal Supremo, quien también esperaba el reino de Dios, con audacia entró ante Pilato y pidió el cuerpo de Jesús.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
Pilato [se] sorprendió de que ya había muerto. Llamó al centurión para preguntar si ya había muerto.
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
Cuando el centurión le informó, [Pilato] entregó el cuerpo a José.
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
Éste compró una sábana, [lo] bajó, [lo ]envolvió en la sábana, [lo ]puso en un sepulcro excavado en una roca y rodó una piedra contra la entrada del sepulcro.
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
María Magdalena y María la [madre] de José observaban dónde era puesto.

< Marko 15 >