< Marko 15 >

1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
atha prabhAte sati pradhAnayAjakAH prA ncha upAdhyAyAH sarvve mantriNashcha sabhAM kR^itvA yIshuM bandhayitva pIlAtAkhyasya deshAdhipateH savidhaM nItvA samarpayAmAsuH|
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
tadA pIlAtastaM pR^iShTavAn tvaM kiM yihUdIyalokAnAM rAjA? tataH sa pratyuktavAn satyaM vadasi|
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
aparaM pradhAnayAjakAstasya bahuShu vAkyeShu doShamAropayA nchakruH kintu sa kimapi na pratyuvAcha|
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
tadAnIM pIlAtastaM punaH paprachCha tvaM kiM nottarayasi? pashyaite tvadviruddhaM katiShu sAdhyeShu sAkShaM dadati|
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
kantu yIshustadApi nottaraM dadau tataH pIlAta AshcharyyaM jagAma|
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
apara ncha kArAbaddhe kastiMshchit jane tanmahotsavakAle lokai ryAchite deshAdhipatistaM mochayati|
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
ye cha pUrvvamupaplavamakArShurupaplave vadhamapi kR^itavantasteShAM madhye tadAnoM barabbAnAmaka eko baddha AsIt|
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
ato hetoH pUrvvAparIyAM rItikathAM kathayitvA lokA uchchairuvantaH pIlAtasya samakShaM nivedayAmAsuH|
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
tadA pIlAtastAnAchakhyau tarhi kiM yihUdIyAnAM rAjAnaM mochayiShyAmi? yuShmAbhiH kimiShyate?
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
yataH pradhAnayAjakA IrShyAta eva yIshuM samArpayanniti sa viveda|
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
kintu yathA barabbAM mochayati tathA prArthayituM pradhAnayAjakA lokAn pravarttayAmAsuH|
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
atha pIlAtaH punaH pR^iShTavAn tarhi yaM yihUdIyAnAM rAjeti vadatha tasya kiM kariShyAmi yuShmAbhiH kimiShyate?
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
tadA te punarapi prochchaiH prochustaM krushe vedhaya|
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
tasmAt pIlAtaH kathitavAn kutaH? sa kiM kukarmma kR^itavAn? kintu te punashcha ruvanto vyAjahrustaM krushe vedhaya|
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
tadA pIlAtaH sarvvAllokAn toShayitumichChan barabbAM mochayitvA yIshuM kashAbhiH prahR^itya krushe veddhuM taM samarpayAmbabhUva|
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
anantaraM sainyagaNo. aTTAlikAm arthAd adhipate rgR^ihaM yIshuM nItvA senAnivahaM samAhuyat|
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
pashchAt te taM dhUmalavarNavastraM paridhApya kaNTakamukuTaM rachayitvA shirasi samAropya
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
he yihUdIyAnAM rAjan namaskAra ityuktvA taM namaskarttAmArebhire|
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
tasyottamA Nge vetrAghAtaM chakrustadgAtre niShThIva ncha nichikShipuH, tathA tasya sammukhe jAnupAtaM praNomuH
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
itthamupahasya dhUmravarNavastram uttAryya tasya vastraM taM paryyadhApayan krushe veddhuM bahirninyushcha|
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
tataH paraM sekandarasya ruphasya cha pitA shimonnAmA kurINIyaloka ekaH kutashchid grAmAdetya pathi yAti taM te yIshoH krushaM voDhuM balAd dadhnuH|
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
atha gulgaltA arthAt shiraHkapAlanAmakaM sthAnaM yIshumAnIya
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
te gandharasamishritaM drAkShArasaM pAtuM tasmai daduH kintu sa na jagrAha|
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
tasmin krushe viddhe sati teShAmekaikashaH kiM prApsyatIti nirNayAya
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
tasya paridheyAnAM vibhAgArthaM guTikApAtaM chakruH|
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
aparam eSha yihUdIyAnAM rAjeti likhitaM doShapatraM tasya shiraUrdvvam AropayA nchakruH|
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
tasya vAmadakShiNayo rdvau chaurau krushayo rvividhAte|
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
tenaiva "aparAdhijanaiH sArddhaM sa gaNito bhaviShyati," iti shAstroktaM vachanaM siddhamabhUta|
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
anantaraM mArge ye ye lokA gamanAgamane chakruste sarvva eva shirAMsyAndolya nindanto jagaduH, re mandiranAshaka re dinatrayamadhye tannirmmAyaka,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
adhunAtmAnam avitvA krushAdavaroha|
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
ki ncha pradhAnayAjakA adhyApakAshcha tadvat tiraskR^itya parasparaM chachakShire eSha parAnAvat kintu svamavituM na shaknoti|
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
yadIsrAyelo rAjAbhiShiktastrAtA bhavati tarhyadhunaina krushAdavarohatu vayaM tad dR^iShTvA vishvasiShyAmaH; ki ncha yau lokau tena sArddhaM krushe. avidhyetAM tAvapi taM nirbhartsayAmAsatuH|
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
atha dvitIyayAmAt tR^itIyayAmaM yAvat sarvvo deshaH sAndhakArobhUt|
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
tatastR^itIyaprahare yIshuruchchairavadat elI elI lAmA shivaktanI arthAd "he madIsha madIsha tvaM paryyatyAkShIH kuto hi mAM?"
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
tadA samIpasthalokAnAM kechit tadvAkyaM nishamyAchakhyuH pashyaiSha eliyam AhUyati|
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
tata eko jano dhAvitvAgatya spa nje. amlarasaM pUrayitvA taM naDAgre nidhAya pAtuM tasmai dattvAvadat tiShTha eliya enamavarohayitum eti na veti pashyAmi|
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
atha yIshuruchchaiH samAhUya prANAn jahau|
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
tadA mandirasya javanikordvvAdadhaHryyantA vidIrNA dvikhaNDAbhUt|
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
ki ncha itthamuchchairAhUya prANAn tyajantaM taM dR^iShdvA tadrakShaNAya niyukto yaH senApatirAsIt sovadat naroyam Ishvaraputra iti satyam|
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
tadAnIM magdalInI marisam kaniShThayAkUbo yoseshcha mAtAnyamariyam shAlomI cha yAH striyo
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
gAlIlpradeshe yIshuM sevitvA tadanugAminyo jAtA imAstadanyAshcha yA anekA nAryo yIshunA sArddhaM yirUshAlamamAyAtAstAshcha dUrAt tAni dadR^ishuH|
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
athAsAdanadinasyArthAd vishrAmavArAt pUrvvadinasya sAyaMkAla Agata
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
IshvararAjyApekShyarimathIyayUShaphanAmA mAnyamantrI sametya pIlAtasavidhaM nirbhayo gatvA yIshordehaM yayAche|
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
kintu sa idAnIM mR^itaH pIlAta ityasambhavaM matvA shatasenApatimAhUya sa kadA mR^ita iti paprachCha|
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
shatasemanApatimukhAt tajj nAtvA yUShaphe yIshordehaM dadau|
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
pashchAt sa sUkShmaM vAsaH krItvA yIshoH kAyamavarohya tena vAsasA veShTAyitvA girau khAtashmashAne sthApitavAn pAShANaM loThayitvA dvAri nidadhe|
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
kintu yatra sosthApyata tata magdalInI mariyam yosimAtR^imariyam cha dadR^ishatR^iH|

< Marko 15 >