< Marko 15 >
1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
Wczesnym rankiem naczelni kapłani, naradziwszy się razem ze starszymi, uczonymi w Piśmie i całą Radą, związali Jezusa, odprowadzili go i wydali Piłatowi.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
A Piłat zapytał go: Czy ty jesteś królem Żydów? On mu odpowiedział: Ty [sam to] mówisz.
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
I oskarżali go naczelni kapłani o wiele rzeczy, ale on nic nie odpowiedział.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
Wtedy Piłat znowu go zapytał: Nic nie odpowiadasz? Zobacz, jak wiele zeznają przeciwko tobie.
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
Jezus jednak nic nie odpowiedział, tak że Piłat się dziwił.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
Na święto miał on zwyczaj wypuszczać im jednego więźnia, o którego prosili.
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
A był [jeden], zwany Barabaszem, więziony wraz z buntownikami, którzy podczas rozruchów popełnili zabójstwo.
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
I tłum zaczął wołać i prosić, [żeby zrobił] to, co zawsze dla nich robił.
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
Lecz Piłat im odpowiedział: Chcecie, abym wam wypuścił króla Żydów?
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
Wiedział bowiem, że naczelni kapłani wydali go z zawiści.
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
Ale naczelni kapłani podburzyli tłum, żeby raczej wypuścił im Barabasza.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
A Piłat znowu im odpowiedział: Cóż więc chcecie, abym uczynił [z tym], którego nazywacie królem Żydów?
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
A oni znowu zawołali: Ukrzyżuj go!
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
Wtedy Piłat zapytał: Cóż on złego uczynił? Lecz oni jeszcze głośniej wołali: Ukrzyżuj go!
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
Piłat więc, chcąc zadowolić tłum, wypuścił im Barabasza, a Jezusa ubiczował i wydał im na ukrzyżowanie.
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
Żołnierze wprowadzili go do sali, czyli do ratusza, i zwołali cały oddział.
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
Potem ubrali go w purpurę, a uplótłszy koronę z cierni, włożyli mu na [głowę].
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
I zaczęli go pozdrawiać: Witaj, królu Żydów!
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
Bili go trzciną po głowie i pluli na niego, a upadając na kolana, oddawali mu pokłon.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
A gdy go wyszydzili, zdjęli z niego purpurę, ubrali go w [jego] własne szaty i wyprowadzili na ukrzyżowanie.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
I przymusili przechodzącego obok niejakiego Szymona z Cyreny, który szedł z pola, ojca Aleksandra i Rufusa, aby niósł jego krzyż.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
I przyprowadzili go na miejsce [zwane] Golgotą, co się tłumaczy: Miejsce Czaszki.
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
Dawali mu do picia wino z mirrą, ale go nie przyjął.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
A gdy go ukrzyżowali, rozdzielili jego szaty, rzucając o nie losy, [by rozstrzygnąć], co kto ma wziąć.
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
A była godzina trzecia, gdy go ukrzyżowali.
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
Był też napis z podaniem jego winy: Król Żydów.
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
I ukrzyżowali z nim dwóch bandytów, jednego po prawej, a drugiego po jego lewej stronie.
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
Tak wypełniło się Pismo, które mówi: Zaliczono go w poczet złoczyńców.
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
A ci, którzy przechodzili obok, bluźnili mu, kiwając głowami i mówiąc: Ej! Ty, który burzysz świątynię i w trzy dni [ją] odbudowujesz;
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
Ratuj samego siebie i zejdź z krzyża!
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
Podobnie naczelni kapłani wraz z uczonymi w Piśmie, naśmiewając się, mówili między sobą: Innych ratował, a samego siebie uratować nie może.
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
Niech Chrystus, król Izraela, zejdzie teraz z krzyża, żebyśmy ujrzeli i uwierzyli. Urągali mu także ci, którzy byli z nim ukrzyżowani.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
A gdy była szósta godzina, ciemność ogarnęła całą ziemię aż do godziny dziewiątej.
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
O godzinie dziewiątej Jezus zawołał donośnym głosem: Eloi, Eloi, lama sabachthani? – co się tłumaczy: Boże mój, Boże mój, czemu mnie opuściłeś?
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
A niektórzy ze stojących tam [ludzi], usłyszawszy to, mówili: Woła Eliasza.
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
Wtedy ktoś podbiegł, napełnił gąbkę octem i włożywszy na trzcinę, dał mu pić, mówiąc: Przestańcie, zobaczymy, czy przyjdzie Eliasz, aby go zdjąć.
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
A Jezus zawołał donośnym głosem i oddał ducha.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
I rozerwała się na pół zasłona świątyni, od góry aż do dołu.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
A setnik, który stał naprzeciw, widząc, że tak wołając, oddał ducha, powiedział: Ten człowiek prawdziwie był Synem Bożym.
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
Były [tam] też kobiety, które przypatrywały się z daleka, a wśród nich Maria Magdalena i Maria, matka Jakuba Mniejszego i Józefa, oraz Salome.
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
One to, gdy jeszcze był w Galilei, chodziły za nim i usługiwały mu. [Było] też wiele innych, które wraz z nim przyszły do Jerozolimy.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
A ponieważ był [dzień] przygotowania, który jest przed szabatem, i nastał już wieczór;
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
Przyszedł Józef z Arymatei, ważny członek Rady, który sam też oczekiwał królestwa Bożego, śmiało wszedł do Piłata i poprosił o ciało Jezusa.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
A Piłat zdziwił się, że już nie żyje, i zawoławszy setnika, zapytał go, czy dawno umarł.
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
I upewniony przez setnika, wydał ciało Józefowi.
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
Ten kupił płótno, zdjął go, owinął płótnem i złożył w grobowcu, który był wykuty w skale, a przed wejście do grobowca zatoczył kamień.
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
A Maria Magdalena i Maria, [matka] Józefa, patrzyły, gdzie go złożono.