< Marko 15 >
1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
Et d'abord au matin les principaux Sacrificateurs avec les Anciens et les Scribes, et tout le Consistoire, ayant tenu conseil, firent lier Jésus, et l'emmenèrent, et le livrèrent à Pilate.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
Et Pilate l'interrogea, disant: es-tu le Roi des Juifs? Et [Jésus] répondant lui dit: tu le dis.
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
Or les principaux Sacrificateurs l'accusaient de plusieurs choses, mais il ne répondit rien.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
Et Pilate l'interrogea encore, disant: ne réponds-tu rien? vois combien de choses ils déposent contre toi.
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
Mais Jésus ne répondit rien non plus; de sorte que Pilate s'en étonnait.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
Or il leur relâchait à la Fête un prisonnier, lequel que ce fût qu'ils demandassent.
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
Et il y en avait un, nommé Barabbas, qui était prisonnier avec ses complices pour une sédition, dans laquelle ils avaient commis un meurtre.
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
Et le peuple criant tout haut, se mit à demander [à Pilate qu'il fît] comme il leur avait toujours fait.
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
Mais Pilate leur répondit, en disant: voulez-vous que je vous relâche le Roi des Juifs?
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
(Car il savait bien que les principaux Sacrificateurs l'avaient livré par envie.)
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
Mais les principaux Sacrificateurs excitèrent le peuple à demander que plutôt il relâchât Barabbas.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
Et Pilate répondant, leur dit encore: que voulez-vous donc que je fasse de celui que vous appelez Roi des Juifs?
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
Et ils s'écrièrent encore: crucifie-le.
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
Alors Pilate leur dit: mais quel mal a-t-il fait? et ils s'écrièrent encore plus fort: crucifie-le.
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
Pilate donc voulant contenter le peuple, leur relâcha Barabbas; et après avoir fait fouetter Jésus, il le livra pour être crucifié.
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
Alors les soldats l'emmenèrent dans la cour, qui est le Prétoire, et toute la cohorte s'étant là assemblée,
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
Ils le vêtirent d'une robe de pourpre, et ayant fait une couronne d'épines entrelacées l'une dans l'autre, ils la lui mirent sur la tête;
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
Puis ils commencèrent à le saluer, [en lui disant]: nous te saluons, Roi des Juifs;
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
Et ils lui frappaient la tête avec un roseau, et crachaient contre lui; et se mettant à genoux, ils se prosternaient devant lui.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
Et après s'être [ainsi] moqués de lui, ils le dépouillèrent de la robe de pourpre, et le revêtirent de ses habits, et l'emmenèrent dehors pour le crucifier.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
Et ils contraignirent un certain [homme, nommé] Simon, Cyrénéen, père d'Alexandre et de Rufus, qui passait [par là], revenant des champs, de porter sa croix.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
Et ils le menèrent au lieu [appelé] Golgotha, c'est-à-dire, le lieu du Crâne.
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
Et ils lui donnèrent à boire du vin mixtionné avec de la myrrhe; mais il ne le prit point.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
Et quand ils l'eurent crucifié, ils partagèrent ses vêtements, en les jetant au sort pour savoir ce que chacun en aurait.
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
Or il était trois heures quand ils le crucifièrent.
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
Et l'écriteau contenant la cause de sa condamnation était: LE ROI DES JUIFS.
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
Ils crucifièrent aussi avec lui deux brigands, l'un à sa main droite, et l'autre à sa gauche.
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
Et ainsi fut accomplie l'Ecriture, qui dit: Et il a été mis au rang des malfaiteurs.
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
Et ceux qui passaient près de là lui disaient des outrages, branlant la tête, et disant: Hé! toi, qui détruis le Temple, et qui le rebâtis en trois jours,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
Sauve-toi toi-même, et descends de la croix.
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
Les principaux Sacrificateurs se moquant aussi avec les Scribes disaient entre eux: il a sauvé les autres, il ne peut se sauver lui-même.
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
Que le Christ, le Roi d’Israël descende maintenant de la croix, afin que nous le voyions et que nous croyions! Ceux aussi qui étaient crucifiés avec lui, lui disaient des outrages.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
Mais quand il fut six heures, il y eut des ténèbres sur tout le pays jusqu'à neuf heures.
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
Et à neuf heures Jésus cria à haute voix, disant: Eloï, Eloï, lamma sabachthani? c'est-à-dire: Mon Dieu! Mon Dieu! pourquoi m'as-tu abandonné?
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
Ce que quelques-uns de ceux qui étaient là présents, ayant entendu, ils dirent: voilà, il appelle Elie.
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
Et quelqu'un accourut, qui remplit une éponge de vinaigre, et qui l'ayant mise au bout d'un roseau, lui en donna à boire, en disant: laissez, voyons si Elie viendra pour l'ôter de la croix.
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
Et Jésus ayant jeté un grand cri, rendit l'esprit.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
Et le voile du Temple se déchira en deux, depuis le haut jusqu'en bas.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
Et le Centenier qui était là vis-à-vis de lui, voyant qu'il avait rendu l'esprit en criant ainsi, dit: certainement cet homme était Fils de Dieu.
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
Il y avait là aussi des femmes qui regardaient de loin, entre lesquelles étaient Marie-Magdeleine, et Marie [mère] de Jacques le mineur, et de Joses, et Salomé.
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
Qui lorsqu'il était en Galilée, l'avaient suivi, et l'avaient servi; [il y avait là] aussi plusieurs autres femmes qui étaient montées avec lui à Jérusalem.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
Et le soir étant déjà venu, parce que c'était la Préparation qui est avant le Sabbat;
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
Joseph d'Arimathée, Conseiller honorable, qui attendait aussi le Règne de Dieu, s'étant enhardi, vint à Pilate, et [lui] demanda le corps de Jésus.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
Et Pilate s'étonna qu'il fût déjà mort; et ayant appelé le Centenier, il lui demanda s'il y avait longtemps qu'il était mort.
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
Ce qu'ayant appris du Centenier, il donna le corps à Joseph.
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
Et [Joseph] ayant acheté un linceul, le descendit de la croix, et l'enveloppa du linceul, et le mit dans un sépulcre qui était taillé dans le roc, puis il roula une pierre sur l'entrée du sépulcre.
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
Et Marie-Magdeleine, et Marie [mère] de Joses regardaient où on le mettait.