< Marko 15 >
1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
And forthwith in the morning the chief priests held a consultation with the elders and scribes, and the whole council, and bound Jesus, and carried [him] away, and delivered [him] to Pilate.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
And Pilate asked him, Art thou the King of the Jews? And he answering, said to him, Thou sayest [it].
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
And the chief priests accused him of many things: but he answered nothing.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
And Pilate asked him again, saying, Answerest thou nothing? behold how many things they testify against thee.
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
But Jesus yet answered nothing: so that Pilate marveled.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
Now at [that] feast he released to them one prisoner, whom they desired.
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
And there was [one] named Barabbas, [who lay] bound with them that had made insurrection with him, who had committed murder in the insurrection.
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
And the multitude crying aloud, began to desire [him to do] as he had ever done to them.
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
But Pilate answered them, saying, Will ye that I release to you the King of the Jews?
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
(For he knew that the chief priests had delivered him for envy.)
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
But the chief priests moved the people that he should rather release Barabbas to them.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
And Pilate answered, and said again to them, What will ye then that I shall do [to him] whom ye call the King of the Jews?
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
And they cried out again, Crucify him.
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
Then Pilate said to them, Why, what evil hath he done? And they cried out the more exceedingly, Crucify him.
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
And [so] Pilate, willing to content the people, released Barabbas to them, and having scourged Jesus, delivered him to be crucified.
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
And the soldiers led him away into the hall, called Pretorium; and they call together the whole band;
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
And they clothed him with purple, and platted a crown of thorns, and put it about his [head],
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
And began to salute him, Hail, King of the Jews!
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
And they struck him on the head with a reed, and spit upon him, and bowing [their] knees, worshiped him.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
And when they had mocked him, they took off the purple from him, and put his own clothes on him, and led him out to crucify him.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
And they constrain one Simon, a Cyrenian, who was passing by, coming from the country, the father of Alexander and Rufus, to bear his cross.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
And they bring him to the place Golgotha, which is, being interpreted, The place of a skull.
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
And they gave him to drink, wine mingled with myrrh: but he received [it] not.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
And when they had crucified him, they parted his garments, casting lots upon them, what every man should take.
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
And it was the third hour, and they crucified him.
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
And the superscription of his accusation was written over, THE KING OF THE JEWS.
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
And with him they crucify two thieves, the one on his right hand, and the other on his left.
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
And the scripture was fulfilled, which saith, And he was numbered with the transgressors.
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
And they that passed by, railed on him, wagging their heads, and saying, Ah, thou that destroyest the temple, and buildest [it] in three days,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
Save thyself, and come down from the cross.
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
Likewise also the chief priests mocking, said among themselves with the scribes, He saved others, himself he cannot save.
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
Let Christ the king of Israel descend now from the cross, that we may see and believe. And they that were crucified with him, reviled him.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
And when the sixth hour was come, there was darkness over the whole land, until the ninth hour.
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
And at the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, Eloi, Eloi, lama, sabacthani? which is, being interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me?
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
And some of them that stood by, when they heard [it], said, Behold, he calleth Elijah.
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
And one ran and filled a sponge full of vinegar, and put [it] on a reed, and gave him to drink, saying, Let alone; let us see whether Elijah will come to take him down.
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
And Jesus cried with a loud voice, and expired.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
And the vail of the temple was rent in two, from the top to the bottom.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
And when the centurion who stood over against him, saw that he so cried out, and expired, he said, Truly this man was the Son of God.
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
There were also women looking on at a distance, among whom was Mary Magdalene, and Mary the mother of James the younger, and of Joses, and Salome;
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
Who also, when he was in Galilee, followed him, and ministered to him; and many other women who came with him to Jerusalem.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
And now, when the evening was come, (because it was the preparation, that is, the day before the sabbath)
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
Joseph of Arimathea, an honorable counselor, who also waited for the kingdom of God, came, and went in boldly to Pilate, and craved the body of Jesus.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
And Pilate wondered if he was already dead: and calling the centurion, he asked him whether he had been any while dead.
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
And when he knew [it] from the centurion, he gave the body to Joseph.
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
And he bought fine linen, and took him down, and wrapped [him] in the linen, and laid him in a sepulcher which was hewn out of a rock, and rolled a stone to the door of the sepulcher.
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
And Mary Magdalene and Mary [the mother] of Joses, beheld where he was laid.