< Marko 15 >

1 Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani, pamoja na wazee, walimu wa sheria na Baraza lote, wakafikia uamuzi. Wakamfunga Yesu, wakamchukua na kumkabidhi kwa Pilato.
Odmah izjutra glavari svećenički zajedno sa starješinama i pismoznancima - cijelo Vijeće - upriličili su vijećanje pa Isusa svezali, odveli i predali Pilatu.
2 Pilato akamuuliza, “Je, wewe ndiye Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
I upita ga Pilat: “Ti li si kralj židovski?” On mu odgovori: “Ti kažeš.”
3 Viongozi wa makuhani wakamshtaki kwa mambo mengi.
I glavari ga svećenički teško optuživahu.
4 Pilato akamuuliza tena, “Je, huna la kujibu? Tazama ni mashtaka mangapi wanayaleta juu yako.”
Pilat ga opet upita: “Ništa ne odgovaraš? Gle, koliko te optužuju.”
5 Lakini Yesu hakujibu lolote, hivyo Pilato akashangaa.
A Isus ništa više ne odgovori te se Pilat čudio.
6 Ilikuwa desturi wakati wa Sikukuu ya Pasaka kumfungulia mfungwa yeyote ambaye watu wangemtaka.
O Blagdanu bi im pustio uznika koga bi zaiskali.
7 Wakati huo, mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa gerezani pamoja na waasi wengine waliokuwa wametekeleza uuaji wakati wa maasi.
A zajedno s pobunjenicima koji u pobuni počiniše umorstvo bijaše u okove bačen čovjek zvani Baraba.
8 Ule umati wa watu ukamjia Pilato na kumwomba awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake.
I uziđe svjetina te poče od Pilata iskati ono što im običavaše činiti.
9 Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie huyu Mfalme wa Wayahudi?”
A on im odgovori: “Hoćete li da vam pustim kralja židovskoga?”
10 Kwa maana yeye alitambua kuwa viongozi wa makuhani walikuwa wamemtia Yesu mikononi mwake kwa ajili ya wivu.
Znao je doista da ga glavari svećenički bijahu predali iz zavisti.
11 Lakini viongozi wa makuhani wakauchochea ule umati wa watu wamwombe awafungulie Baraba badala yake.
Ali glavari svećenički podjare svjetinu da traži neka im radije pusti Barabu.
12 Pilato akawauliza tena, “Basi mnataka nifanye nini na huyu mtu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
Pilat ih opet upita: “Što dakle da učinim s ovim kojega zovete kraljem židovskim?”
13 Wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe!”
A oni opet povikaše: “Raspni ga!”
14 Pilato akawauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakapiga kelele kwa nguvu zaidi, wakisema, “Msulubishe!”
Reče im Pilat: “Ta što je zla učinio?” Povikaše još jače: “Raspni ga!”
15 Pilato, akitaka kuuridhisha ule umati wa watu, akawafungulia Baraba. Naye baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
Hoteći ugoditi svjetini, Pilat im pusti Barabu, a Isusa izbičeva i preda da se razapne.
16 Askari wakampeleka Yesu hadi kwenye ukumbi wa ndani wa jumba la kifalme, ndio Praitorio, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
Vojnici ga odvedu u unutarnjost dvora, to jest u pretorij, pa sazovu cijelu četu
17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
i zaogrnu ga grimizom; spletu trnov vijenac i stave mu na glavu
18 Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
te ga stanu pozdravljati: “Zdravo, kralju židovski!”
19 Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.
I udarahu ga trskom po glavi, pljuvahu po njemu i klanjahu mu se prigibajući koljena.
20 Walipokwisha kumdhihaki, wakamvua lile joho la zambarau, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakamtoa nje ili wakamsulubishe.
A pošto ga izrugaše, svukoše mu grimiz i obukoše mu njegove haljine. I izvedu ga da ga razapnu.
21 Mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, baba yao Aleksanda na Rufo, alikuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shamba, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
I prisile nekog prolaznika koji je dolazio s polja, Šimuna Cirenca, oca Aleksandrova i Rufova, da mu ponese križ.
22 Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
I dovuku ga na mjesto Golgotu, što znači Lubanjsko mjesto.
23 Nao wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini hakuinywa.
I nuđahu mu piti namirisana vina, ali on ne uze.
24 Basi wakamsulubisha, nazo nguo zake wakagawana miongoni mwao kwa kuzipigia kura ili kuamua ni gani kila mtu ataichukua.
Kad ga razapeše, razdijele među se haljine njegove bacivši za njih kocku - što će tko uzeti.
25 Ilikuwa yapata saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
A bijaše treća ura kad ga razapeše.
26 Tangazo likaandikwa la mashtaka dhidi yake lenye maneno haya: “Mfalme wa Wayahudi.”
Bijaše napisan i natpis o njegovoj krivici: “Kralj židovski.”
27 Pamoja naye walisulubiwa wanyangʼanyi wawili, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. [
A zajedno s njime razapnu i dva razbojnika, jednoga njemu zdesna, drugoga slijeva.
28 Nayo maandiko yakatimizwa, yale yasemayo, “Alihesabiwa pamoja na watenda dhambi.]”
29 Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
Prolaznici su ga pogrđivali mašući glavama: “Ej, ti, koji razvaljuješ Hram i sagradiš ga za tri dana,
30 basi shuka kutoka msalabani na ujiokoe mwenyewe!”
spasi sam sebe, siđi s križa!”
31 Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani pamoja na walimu wa sheria wakamdhihaki miongoni mwao wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe!
Slično i glavari svećenički s pismoznancima rugajući se govorahu jedni drugima: “Druge je spasio, sebe ne može spasiti!
32 Basi huyu Kristo, huyu Mfalme wa Israeli, ashuke sasa kutoka msalabani, ili tupate kuona na kuamini.” Wale waliosulubiwa pamoja naye pia wakamtukana.
Krist, kralj Izraelov! Neka sad siđe s križa da vidimo i povjerujemo!” Vrijeđahu ga i oni koji bijahu s njim raspeti.
33 Ilipofika saa sita, giza liliifunika nchi yote hadi saa tisa.
A o šestoj uri tama nasta po svoj zemlji - sve do ure devete.
34 Mnamo saa tisa, Yesu akapaza sauti, akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
O devetoj uri povika Isus iza glasa: “Eloi, Eloi lama sabahtani?” To znači: “Bože moj, Bože moj, zašto si me ostavio?”
35 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama karibu waliposikia hayo, wakasema, “Msikieni, anamwita Eliya.”
Neki od nazočnih čuvši to govorahu: “Gle, Iliju zove.”
36 Mtu mmoja akaenda mbio, akachovya sifongo kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe, akisema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumshusha kutoka hapo msalabani.”
A jedan otrča, natopi spužvu octom, natakne na trsku i pruži mu piti govoreći: “Pustite da vidimo hoće li doći Ilija da ga skine.”
37 Kisha Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
A Isus zavapi jakim glasom i izdahnu.
38 Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
I zavjesa se hramska razdrije nadvoje, odozgor dodolje.
39 Basi yule jemadari aliyekuwa amesimama hapo mbele ya msalaba wa Yesu aliposikia ile sauti yake na kuona jinsi alivyokata roho, akasema, “Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
A kad satnik koji stajaše njemu nasuprot vidje da tako izdahnu, reče: “Zaista, ovaj čovjek bijaše Sin Božji!”
40 Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakiangalia kwa mbali. Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo mdogo na Yose, pia na Salome.
Izdaleka promatrahu i neke žene: među njima Marija Magdalena i Marija, majka Jakova Mlađega i Josipa, i Saloma -
41 Hawa walifuatana na Yesu na kushughulikia mahitaji yake alipokuwa Galilaya. Pia walikuwepo wanawake wengine wengi waliokuwa wamekuja pamoja naye Yerusalemu.
te su ga pratile kad bijaše u Galileji i posluživale mu - i mnoge druge koje uziđoše s njim u Jeruzalem.
42 Ilipofika jioni, kwa kuwa ilikuwa Siku ya Maandalizi, yaani siku moja kabla ya Sabato,
A uvečer, budući da je bila Priprava, to jest predvečerje subote,
43 Yosefu wa Arimathaya, mtu aliyeheshimiwa katika Baraza, na ambaye alikuwa anautarajia Ufalme wa Mungu, akamwendea Pilato kwa ujasiri na kumwomba mwili wa Yesu.
dođe Josip iz Arimateje, ugledan vijećnik, koji također isčekivaše kraljevstvo Božje: odvaži se, uđe k Pilatu i zaiska tijelo Isusovo.
44 Pilato alikuwa akijiuliza kama Yesu alikuwa amekwisha kufa. Hivyo akamwita yule jemadari, akamuuliza iwapo Yesu alikuwa amekwisha kufa.
Pilat se začudi da je već umro pa dozva satnika i upita ga je li odavna umro.
45 Baada ya kupata habari kutoka kwa yule jemadari kwamba kweli amekwisha kufa, Pilato akampa Yosefu ruhusa ya kuuchukua huo mwili.
Kad sazna od satnika, darova Josipu tijelo.
46 Hivyo Yosefu akanunua kitambaa cha kitani safi, akaushusha mwili kutoka msalabani, akaufunga katika kile kitambaa cha kitani, na kuuweka ndani ya kaburi lililochongwa kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kwenye ingilio la kaburi.
Josip kupi platno, skine tijelo i zavije ga u platno te položi u grob, koji bijaše izduben iz stijene. I dokotrlja kamen na grobna vrata.
47 Maria Magdalene na Maria mamaye Yose walipaona mahali pale alipolazwa.
A Marija Magdalena i Marija Josipova promatrahu kamo ga polažu.

< Marko 15 >