< Marko 14 >
1 Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
Chiyi vali hanu mazuva overe niwuseni kusika mukiti we Paseka ni Mukiti we nkonko isena Mulungo. Mukulwana wavaPurisita ni vañoli vavali kunganisisa mwete vawolere kuwonda Jesu ni kumwihaya.
2 Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”
Ka kuti vavali kuwamba. “Isiñi hamukiti, iri kuti kanji kuvuki inyakanyaka mukati kavantu.”
3 Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.
Lyahanu Jesu avena mwa Betani mwizuvo ya Simoni we mbingwa, sina havali kwikere he tafule, mukulwakazi chakeza kwali ni votera lya alabasitera lyomunikiso undula ahulu, uvali wa menzi a nandi. Cha pwachula ivotera ni kuitira hamutwi wakwe.
4 Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini?
Mi kuvena vamwi vavali kuvengete. Chiva wamba kukati kavo nivati, “Ivakanzi lye shinyehero iyi?
5 Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.
Iwu munukiso uvali kuswanera kuwuziwa kumashereñi a hitilira miyanda yotatwe ye dinarii, ni kuha kuva shevete. Imi vavali kumu kalimera.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana.
Kono Jesu chawamba, “Mu musiye yenke, mu mu kataleza nzi? Wapanga chitu chilotu kwangu.
7 Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
Mwina inako yonse vashevete nanwe, mi inakao yonse imwa saka muwola kupanga zilotu kuvali, kono kete muve name inako yonse.
8 Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu.
Wapanga icho cha wola: wa singa muvili wangu haku zikwa.
9 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
“Chovu niti ni wamba kwenu, konse uko ivangeli kwete ikakutaziwe mwi kanda yonse, icho chapanga uzu mukulwakazi kachika wambiwe, mwikupuzo yakwe.”
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao.
Lyinu Judasi Isikariyota, zumwe wava vena ikumi ne tovere, a va yendi ku vapurisita vakulwana kuti a wolye kumuva wuzukiza choku muva tambika.
11 Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.
Lyahanu mukulwana wa mapurisita hazizuwa, vavali kutavite ni kumu sepisa kumuha mashereñi. Chatanga kulola inzira yate awane chivaka cho kumutambika kuvali.
12 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
Mu izuva lye ntazi lye chinkwe chisena mumera, chinga va panga chitavero che imberere ye paseka, varutwana vakwe choku mucho kuti, “U saka kuti tuye kuhi kutu wola kuka ku vakanyeza zilyio ze paseka, iri kuti ukalye zilyo ze paseka?
13 Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni.
Choku tuma vovere va varutwana vakwe choku vacho kuti, “Mu kwiya mu muleneñi, ku zwaho mumu wane mukwame yo hindite kahambwe kamenzi mwami katane. Mu muichirire.
14 Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
Mu inzuvo yeeti a ke injire, mu muichirire mo mi muka cho kusi inzuvo kuti, 'Muruti ucho kuti, inzuvo yangu yeti ni lyire ipaseka ne varutwana vangu yina kuhi?'”
15 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”
Mwa a ka mutondeza inzuvo inkando yi vakanyizwe yahe wulu, muka tuvakanyeze mwateni.”
16 Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
Varutwana ni va zwa ni kuyenda mumuleneñi. Mi ni va ka wani chimwe ne chimwe china sina mwa a vawambiri kuvali, mi.
17 Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
Ha chivali chitengu, chakeza ni vekumi nivovere.
18 Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
Sina havavali kwi kere he tafule ni kulya, Jesu chati, “Chovuniti ni wamba kwenu, wumwina kwenu yo lya name.”
19 Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
Vonse vavali lizuwi inkumbu, mi zumwi ni zumwi chiva wamba kwali, “Luli isiñi me?”
20 Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
Jesu che tava ni kuvawamba kuvali, “nje zumwi wa vena ikumi ne vovere, yozo yo sunsa name inkonko mu kasuva.
21 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
Kakuti Mwana wo Muntu mwayende mwinzira iyo mañolo awamba kuyamana naye. Mi ku mayivite kozuo mukwame yo veteka Mwana o Muntu! Ku vaa shiyeme kuti kalyi uzu muntu na sana a va zalwa.”
22 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
Chi va si kwete kulyia, Jesu cha hinda chinkwe, ni kuchi fuyola, ni kuchi jamona. Ava chivahi ni kuwamba, “Muhinde ichi. Uwu chimuviri wangu.”
23 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
Chahinda i komoki, nikulitumera, ni kuitambika kuvali, mi vonse chiva nya kuili.
24 Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
Chawamba kuvali, “Aya jamalaha angu echilikani, malaha awo etilirwe vangi.
25 Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
Chovu niti niwamba kwenu, Kasane kani nywe hape kwezi zihikantu hape ze veine kusikira kusikira lina izuva hate kani inwe mumuvuso we Ireeza.”
26 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
Hachiva manite kuzimba luzimbo, chiva yenda hanze kwi Lundu lya Olive.
27 Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
Jesu chata kuvali, “Muvonse mumunitiyire, kakuti kuñoletwe, 'Muni kave mulisani mi imberere kazi hasane.'
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
Kono china mana kuvuswa hape, Kanili tangize kwenu kuya kwa Galileya.”
29 Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
Pitorosi choku mucho kuti, “Nangati vonse kava ku tiyire ime keti ni ni ku tiyiire.”
30 Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
Jesu chamu wambira kuti, “Cho vuniti nikuwambira, masiku a sunu, mukombwe ni useni kulira kovere, moni sapule kotwatwe.”
31 Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Kono Pitorosi chati, “Haiva nini wola kufwa nawe, kete nikusampule.” Vonse vava chiva panga i sepiso i swana.
32 Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
Va veza ku chivaka chi sumpwa Getesimani, Jesu cho kucho varutwana vakwe, “Mu ikale a ha chini rapera.”
33 Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
Cha hinda Pitorosi, Jakovo ni Johani choku zwa navo, choku tanga ku wirirwa ne ku katazeha a hulu.
34 Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
Cha wamba kuvali, “Luhuho lwangu lu zuwire ku chisa a hulu, nanga kwi nako yefu. Mu shale hanu ni kutonda.”
35 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
Jesu na ya ha vusuzana, choku wa hansi, choku rapera kuti kambe ni ku wolyeka, iyi inako imu hitirire kwali.
36 Akasema, “Abba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
Nati, “Abba, Tayo, zintu zonse zi wolyeka nawe. Zwisa iyi inkomoki kwangu. Kono isiñi chini saka, Kono yako.”
37 Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
Chaka vola ni kwiza kuvawana valere, mi chawamba kwa Pitorosi, “Simoni, ulere? Wakangwa kutonda nagati i hola yonke?
38 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Mutonde ni kulapera iri kuti kanji mwinjiri mumuliko. Luhuho che niti lusaka, kono inyama i kangitwe.”
39 Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
Hape chayenda kule ni kukalapera, mi ava severisi manzwi a swana.
40 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.
Hape cha vola ni kukavawana valere, kakuti menso avo avali kulema mi kena vavali kwizi cho kuwamba kwali.
41 Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Cho kuiza lo vutatu na vacho kuti, “Mu si lere ne ku pumula? Muvuke! inako chi ya sika. Muvone! Mwana o Muntu cha vekwa mumanza ava ezalivi.
42 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Mu vuke; tuyende. Muvone, uzo yo ni veteka wina hafuhi.”
43 Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.
Cho usi kwete ku wamba, Judasi, zumwe wa vena ikumi ne tovere, choku sika, nena ni vantu vangi ni va ka kwete mikwale ni masavule, kukazwa ku vapurisita vakulwana, n vañoli, ni vakulwana.
44 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”
Lyahanu yo muveteka avava here chisupo, kuti, “Uzo yete ni chunchune nji yena.”
45 Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.” Akambusu.
Judasi hasika, pona aho cheza kwa Jesu nikuwamba, “'Rabbi! mi chamu chunchuna.
46 Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi.
Linu chivavika maanza hali ni kumu sumina.
47 Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
Kono zumwi yava zimene hembali chazwisa mukwale niku kosola kutwi kwa muhikana wo mupurisita mukulwana.
48 Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
Jesu chawamba kuvali, “mu ka ni izilile mane ili musa, cha mikwale ni che inkolyi kwiza kuni wonda?
49 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”
Nivena nenwe izuva nezuva hini vaku siina nnaanwe izu nva niva kuluta mwi tempele, kena muva nisumini. Kono ichi chiva pangahali kuti intimana zi zuzilizwe.”
50 Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.
Mi vavena ni Jesu vava musiyi niku valeha.
51 Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata,
Mu lombwaana, ya va zwete vulyo inguvo ivali kumuzingerete, avali kwi chilire Jesu. Aho vakwame hava mukwata,
52 alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.
chasiya inguvo ye line ni kutiya mapunu.
53 Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja.
Vavatwali Jesu kumupurisita mukulwana. Uko vavali kungene naye vonse malena vamapurisita, vakulwana, niva ñoli.
54 Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.
Lyahanu Pitorosi avali kumwi chilire chaka vakazana, mane mbwita kukasika he rapa lya mupurisita mukulwana. Avake kali mukati kava ngateri, vavali kwina hembali ni muliro kuli tukusa.
55 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.
Linu mukulwana wava purisita ni nkuta ya Majuda vonse vavali kungana vupaki vuhambiriza Jesu iri kuli vamwi haye. Kono kakwina vuvava wani.
56 Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.
Kakuti vangi vavaleti vupaki bwa mapa kumulwisa, kono mane vupaki bwavo kena vuva zumizani.
57 Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:
Vamwe ni va zimana avo choku mu hambiriza, ni vaati,
58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’”
“Tu vamu zuwi nati, 'Ka ni rutunune iyi itempere yi va pangwa cha manza, mi ku zwaho njeti nini pange yimwe yi sana yiva pangwa cha manza.'”
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.
Mane nangati aho hape vupaki vwavo ni vwa vula ku zuminzana.
60 Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
Mu purisita mukulwana ava zimani mukati kavo ni kuvuza Jesu, “Kowina iwe ikalavo? Chintu nzi ava vakwame zivapaka kuamana nawe?
61 Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”
Kono avali kuntontwere ni kusetava chimwi. Hape mupurisita mukulwana chamuvuza ni kuti, “Jewe Keresite, mwana wozo yo fuyaulitwe?”
62 Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
Jesu chati, “Jeme. Mi kovone Mwana o Muntu hasana kekale he yanza lyokulisa lya ziho ni kukeza ni makope e wulu.”
63 Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?
Mu purisita mukulwaana cha halula mukanjo wakwe ni kucho, “Tusi saka vumwi vupaki?
64 Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.
Mwazuwa vunyefuli. Ikatulo yenu jeyihi?” Mi vonse chiva yatula uvu zumwi yoswanera ifu.
65 Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.
Vamwi chivatanga kumu swira mate ni kuwumba impata yakwe ni kumu vakula ni kucho kwali, “Porofite!” Mapokola chiva muhinda ni kuka mundama.
66 Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu.
Linu Pitorosi havali kwina hanze ye rapa, omwina muhikana wo mukazana wo mupurisita mukulwana cheza kwali.
67 Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
Avavoni Pitorosi sina havali kuzimene ha muliro kuli tukusa, mi chalola hande kwali. Mi cha wamba, “I we nawe uvali kwina nimu Nazareta, Jesu.”
68 Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.
Kono ava sampuli, nati, “Kanimwizi kamba kuzuwisisa chizi chowamba nacho.”Lyaho che jira mwirapa.
69 Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”
Kono muhikana wo mukazana umo chamuvona nikutanga kuwamba hape kwavo vavali kuzimene, “Uzu mukwame ji zumwi wavo!”
70 Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”
Kono cha kanana hape. Hakuhita inako zana vulyo avo vavali kuzimene ho vavali kuwamba kwa Pitorosi, “Kamaniti uzumwi wavo, kakuli nawe umu Galileya.”
71 Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”
Kono chatanga kulivika muchikuto ni kulinkonka, “Kanizi uzu mukwame umukwete kuwamba zakwe.”
72 Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.
Mukombwe yahaho chiwa lira lyo vuveri. Mi Pitorosi cha hupula manzwi awo Jesu ava muwambiri: “Pilio mukombwe niuseni kulira tovere, moni sampule to tatwe.” Imi cha virera ni kulira.