< Marko 14 >

1 Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
Now it was the Passover and the Unleavened [cakes], after two days. And the High-priests and Scribes were seeking, how, with guile, they might secure, and lay him;
2 Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”
for they were saying—Not in the feast, lest there be an uproar of the people.
3 Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.
And, he being in Bethany, in the house of Simon the leper, as he was reclining, there came a woman, holding an alabaster-jar of perfume, pure spikenard, very costly; and breaking the jar she was pouring down [the perfume], upon his head.
4 Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini?
But there were some much displeased among themselves—To what end hath, this waste of the perfume happened?
5 Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.
For this perfume could have been sold for above three hundred denaries, and given unto the destitute! and they were indignant with her.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana.
But, Jesus, said—Let her alone! Why are ye reproaching, her? A seemly work, hath she wrought, in me;
7 Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
For, always, have ye, the destitute, with you, and whensoever ye please, ye can, unto them, [at any time] do well! But, me, not, always, have ye.
8 Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu.
What she had, she used, —She took it beforehand to anoint my body for the burial;
9 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
And, verily, say unto you—Wheresoever the glad-message shall be proclaimed throughout the whole world, —also what she did, will be told for a memorial of her.
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao.
And, Judas Iscariot, who was one of he twelve, went away unto the High-priests, that, him, he might deliver up unto them.
11 Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.
Now, when they heard, they rejoiced, and promised to give him, silver; and he was seeking how, at a favourable opportunity, he might, deliver him up.
12 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
And, on the first day of the unleavened cakes, when, the passover, they were slaying, his disciples say unto him—Where wilt thou, we depart and make ready, that thou mayest eat the passover?
13 Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni.
And he sendeth forth two of his disciples, and saith unto them—Go your way into the city, and there will meet you a man, a jar of water, bearing, —follow him;
14 Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
and, wheresoever he shall enter, say ye unto the householder—The teacher, saith, Where is my lodging, where, the passover, with my disciples, I may eat?
15 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”
And, he, unto you, will shew, a large upper-room, spread ready, and, there, make ye ready for us.
16 Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
And the disciples went forth, and came into the city, and found, according as he had said unto them, —and they made ready the passover.
17 Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
And, when evening arrived, he cometh, with the twelve.
18 Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
And, as they were reclining and eating, Jesus said—Verily, I say unto you—One from among you, will deliver me up, he that is eating with me.
19 Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
They began to be grieved, and to be saying unto him, one by one, —Can it be, I?
20 Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
And, he, said unto them—One of the twelve, he that is dipping with me into the [one] bowl:
21 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
Because, the Son of Man, indeed, goeth his way, —according as it is written concerning him; but alas! for that man, through whom the Son of Man is being delivered up, —Well for him, if that man, had not been born!
22 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
And, as they were eating, taking a loaf, he blessed and brake, and gave unto them, and said—Take! this, is, my body;
23 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
And, taking a cup, he offered thanks, and gave unto them; and they, all, drank of it.
24 Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
And he said unto them—This, is, my blood of the covenant, that is to be poured out in behalf of many.
25 Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
Verily, I say unto you—No more, will I in anywise drink of the fruit of the vine, until that day when I shall be drinking it new, in the kingdom of God.
26 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
And, having sung praise, they went forth unto the Mount of Olives.
27 Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
And Jesus saith unto them—Ye, all, will find cause of stumbling, because it is written, —I will smite the shepherd, and, the sheep, will be scattered abroad;
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
But, after my arising, I will go before you into Galilee.
29 Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
And, Peter, said unto him—Even if, all, shall find cause of stumbling, certainly not, I.
30 Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
And Jesus saith unto him—Verily, I say unto thee, thou, this day, in this night, before that twice a cock crow, thrice, will deny me.
31 Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
But he, most vehemently, was saying—Even though I must needs die with thee, in nowise, will I, deny thee. Likewise, indeed, were, all besides, saying.
32 Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
And they come into an estate the name of which is Gethsemane, and he saith unto his disciples—Sit ye here, while I pray.
33 Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
And he taketh Peter and James and John with him, and began to be exceedingly amazed, and in great distress;
34 Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
and he saith unto them—Encompassed with grief is my soul, unto death: Abide ye here, and be watching.
35 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
And, going forward a little, he fell upon the ground, and was praying that, if it were possible, the hour might pass from him;
36 Akasema, “Abba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
and was saying—Abba! O Father! All things, are possible to thee: Bear aside this cup from me; but not what, I, will, but what, thou, [wilt].
37 Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
And he cometh and findeth them sleeping, and saith unto Peter—Simon! art thou sleeping? Hadst thou not strength, one hour, to watch?
38 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Be watching and praying, that ye enter not into temptation: the, spirit, indeed, is willing, but, the flesh, weak.
39 Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
And, again, departing, he prayed, [the same thing, saying].
40 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.
And, again, coming, he found them sleeping, for their eyes were being, weighed down, —and they knew not what to answer him.
41 Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
And he cometh the third time, and saith unto them—Ye are sleeping the remaining time and taking your rest: —It is enough! the hour hath come! Lo! the Son of Man is being delivered up into the hands of sinners.
42 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Be rousing yourselves, let us be leading on! Lo! he that is delivering me up, hath drawn near.
43 Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.
And, straightway, while yet he is speaking, Judas Iscariot, one of the twelve, cometh near, and, with him, a multitude, with swords and clubs, from the High-priests and the Scribes and the Elders.
44 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”
He that is delivering him up hath given an agreed sign unto them, saying—Whomsoever I shall kiss, he, it is! Secure him, and be leading away, safely.
45 Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.” Akambusu.
And, coming, straightway, stepping forward to him, he saith—Rabbi! and openly kissed him.
46 Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi.
And, they, thrust their hands on him, and secured him.
47 Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
[A certain] one of the by-standers, drawing a sword, smote the servant of the High priest, and took off his, ear.
48 Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
And Jesus, answering, said unto them—As against a robber, came ye forth, with swords and clubs, to arrest me?
49 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”
Daily, was I with you, in the temple, teaching; and ye secured me not. But, that, the Scriptures, may be fulfilled…
50 Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.
And they, all, forsook, him, and fled.
51 Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata,
And, a certain young man, was following with him, having cast about himself a fine Indian cloth, over his naked body, —and they are securing him;
52 alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.
but, he, leaving behind the cloth, fled naked.
53 Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja.
And they led away Jesus unto the High-priest; and all the High-priests and the Elders and the Scribes gather together.
54 Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.
And, Peter, afar of, followed him, as far as within, into the court of the High-priest; and was sitting with the attendants, and warming himself by the light.
55 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.
Now, the High-priest, and all the High-council, were seeking, against Jesus, testimony, with the intent to put him to death, —and were not finding any;
56 Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.
for, many, were bearing false-witness against him, and the testimonies were not, agreed.
57 Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:
And some, standing up, were bearing false-witness against him, saying—
58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’”
We, heard him saying, I, will pull down this shrine, the one made by hand, and, in three days, another, not made by hand, will I raise.
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.
And, not even so, was the testimony, agreed.
60 Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
And, the High-priest rising up into the midst, questioned Jesus, saying—Answerest thou, nothing? What are these, against thee, witnessing?
61 Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”
But, he, was silent, and answered, nothing. Again, the High-priest was questioning him, and saith unto him—Art, thou, the Christ the Son of the Blessed?
62 Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
And Jesus said—I, am; and ye shall see the Son of Man—sitting, on the right hand, of Power, and coming with the clouds of heaven.
63 Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?
And, the High-priest, having rent asunder his inner-garments, saith—What, further, need have we, of witnesses?
64 Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.
Heard ye the profanity? What, to you, doth it appear? And they, all, condemned him to be, worthy, of, death.
65 Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.
And some began to be spitting at him, and, covering up his face, and to be buffeting him, and saying to him—Prophesy! And, the attendants, with smart blows, took him.
66 Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu.
And, Peter, being, below in the court, there cometh one of the maid-servants of the High-priest;
67 Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
and, seeing Peter warming himself, having looked at him, saith—And, thou, wast, with the Nazarene—with Jesus.
68 Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.
But, he, denied, saying—I neither know [him], nor do I well understand what, thou, sayest; and went out into the porch.
69 Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”
And, the maid-servant, seeing him, began, again, to be saying unto the by-standers—This one, is, from among them.
70 Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”
But, he, again, was denying. And, after a little again, the by-standers, were saying unto Peter—Truly, thou, art, from among them; for thou art, a Galilaean, also.
71 Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”
And, he, began to be cursing and swearing—I know not this man, of whom ye are speaking!
72 Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.
And, straightway, a second time, a cock, crowed; and Peter was reminded of the declaration, how Jesus had said to him—Before a cock, twice, crow, thrice, wilt thou deny me. And, when he thought thereon, he began to weep.

< Marko 14 >