< Marko 14 >
1 Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
After two days was the feast of the passover, and of unleavened bread: and the chief priests and the scribes sought how they might take him by craft, and put him to death.
2 Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”
But they said, Not on the feast day, lest there be an uproar of the people.
3 Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.
And being in Bethany in the house of Simon the leper, as he sat at meat, there came a woman having an alabaster box of ointment of spikenard very precious; and she brake the box, and poured it on his head.
4 Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini?
And there were some that had indignation within themselves, and said, Why was this waste of the ointment made?
5 Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.
For it might have been sold for more than three hundred pence, and have been given to the poor. And they murmured against her.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana.
And Yahushua said, Let her alone; why trouble ye her? she hath wrought a good work on me.
7 Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
For ye have the poor with you always, and whensoever ye will ye may do them good: but me ye have not always.
8 Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu.
She hath done what she could: she is come aforehand to anoint my body to the burying.
9 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Verily I say unto you, Wheresoever this gospel shall be preached throughout the whole world, this also that she hath done shall be spoken of for a memorial of her.
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao.
And Judas Iscariot, one of the twelve, went unto the chief priests, to betray him unto them.
11 Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.
And when they heard it, they were glad, and promised to give him money. And he sought how he might conveniently betray him.
12 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
And the first day of unleavened bread, when they killed the passover, his disciples said unto him, Where wilt thou that we go and prepare that thou mayest eat the passover?
13 Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni.
And he sendeth forth two of his disciples, and saith unto them, Go ye into the city, and there shall meet you a man bearing a pitcher of water: follow him.
14 Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
And wheresoever he shall go in, say ye to the goodman of the house, The Rabbi saith, Where is the guestchamber, where I shall eat the passover with my disciples?
15 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”
And he will shew you a large upper room furnished and prepared: there make ready for us.
16 Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
And his disciples went forth, and came into the city, and found as he had said unto them: and they made ready the passover.
17 Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
And in the evening he cometh with the twelve.
18 Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
And as they sat and did eat, Yahushua said, Verily I say unto you, One of you which eateth with me shall betray me.
19 Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
And they began to be sorrowful, and to say unto him one by one, Is it I? and another said, Is it I?
20 Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
And he answered and said unto them, It is one of the twelve, that dippeth with me in the dish.
21 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
The Son of man indeed goeth, as it is written of him: but woe to that man by whom the Son of man is betrayed! good were it for that man if he had never been born.
22 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
And as they did eat, Yahushua took bread, and blessed, and brake it, and gave to them, and said, Take, eat: this is my body.
23 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
And he took the cup, and when he had given thanks, he gave it to them: and they all drank of it.
24 Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
And he said unto them, This is my blood of the new testament, which is shed for many.
25 Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
Verily I say unto you, I will drink no more of the fruit of the vine, until that day that I drink it new in the kingdom of YHWH.
26 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
And when they had sung an hymn, they went out into the mount of Olives.
27 Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
And Yahushua saith unto them, All ye shall be offended because of me this night: for it is written, I will smite the shepherd, and the sheep shall be scattered.
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
But after that I am risen, I will go before you into Galilee.
29 Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
But Kepha said unto him, Although all shall be offended, yet will not I.
30 Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
And Yahushua saith unto him, Verily I say unto thee, That this day, even in this night, before the cock crow twice, thou shalt deny me thrice.
31 Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
But he spake the more vehemently, If I should die with thee, I will not deny thee in any wise. Likewise also said they all.
32 Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
And they came to a place which was named Gethsemane: and he saith to his disciples, Sit ye here, while I shall pray.
33 Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
And he taketh with him Kepha and James and John, and began to be sore amazed, and to be very heavy;
34 Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
And saith unto them, My soul is exceeding sorrowful unto death: tarry ye here, and watch.
35 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
And he went forward a little, and fell on the ground, and prayed that, if it were possible, the hour might pass from him.
36 Akasema, “Abba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
And he said, Abba, Father, all things are possible unto thee; take away this cup from me: nevertheless not what I will, but what thou wilt.
37 Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
And he cometh, and findeth them sleeping, and saith unto Kepha, Simon, sleepest thou? couldest not thou watch one hour?
38 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Watch ye and pray, lest ye enter into temptation. The spirit truly is ready, but the flesh is weak.
39 Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
And again he went away, and prayed, and spake the same words.
40 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.
And when he returned, he found them asleep again, (for their eyes were heavy, ) and they knew not what to answer him.
41 Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
And he cometh the third time, and saith unto them, Sleep on now, and take your rest: it is enough, the hour is come; behold, the Son of man is betrayed into the hands of sinners.
42 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Rise up, let us go; lo, he that betrayeth me is at hand.
43 Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.
And immediately, while he yet spake, cometh Judas, one of the twelve, and with him a great multitude with swords and staves, from the chief priests and the scribes and the elders.
44 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”
And he that betrayed him had given them a token, saying, Whomsoever I shall kiss, that same is he; take him, and lead him away safely.
45 Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.” Akambusu.
And as soon as he was come, he goeth straightway to him, and saith, Rabbi, Rabbi; and kissed him.
46 Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi.
And they laid their hands on him, and took him.
47 Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
And one of them that stood by drew a sword, and smote a servant of the high priest, and cut off his ear.
48 Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
And Yahushua answered and said unto them, Are ye come out, as against a thief, with swords and with staves to take me?
49 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”
I was daily with you in the temple teaching, and ye took me not: but the scriptures must be fulfilled.
50 Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.
And they all forsook him, and fled.
51 Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata,
And there followed him a certain young man, having a linen cloth cast about his naked body; and the young men laid hold on him:
52 alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.
And he left the linen cloth, and fled from them naked.
53 Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja.
And they led Yahushua away to the high priest: and with him were assembled all the chief priests and the elders and the scribes.
54 Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.
And Kepha followed him afar off, even into the palace of the high priest: and he sat with the servants, and warmed himself at the fire.
55 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.
And the chief priests and all the council sought for witness against Yahushua to put him to death; and found none.
56 Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.
For many bare false witness against him, but their witness agreed not together.
57 Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:
And there arose certain, and bare false witness against him, saying,
58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’”
We heard him say, I will destroy this temple that is made with hands, and within three days I will build another made without hands.
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.
But neither so did their witness agree together.
60 Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
And the high priest stood up in the midst, and asked Yahushua, saying, Answerest thou nothing? what is it which these witness against thee?
61 Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”
But he held his peace, and answered nothing. Again the high priest asked him, and said unto him, Art thou the Messiah, the Son of the Blessed?
62 Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
And Yahushua said, I am: and ye shall see the Son of man sitting on the right hand of power, and coming in the clouds of heaven.
63 Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?
Then the high priest rent his clothes, and saith, What need we any further witnesses?
64 Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.
Ye have heard the blasphemy: what think ye? And they all condemned him to be guilty of death.
65 Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.
And some began to spit on him, and to cover his face, and to buffet him, and to say unto him, Prophesy: and the servants did strike him with the palms of their hands.
66 Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu.
And as Kepha was beneath in the palace, there cometh one of the maids of the high priest:
67 Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
And when she saw Kepha warming himself, she looked upon him, and said, And thou also wast with Yahushua of Nazareth.
68 Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.
But he denied, saying, I know not, neither understand I what thou sayest. And he went out into the porch; and the cock crew.
69 Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”
And a maid saw him again, and began to say to them that stood by, This is one of them.
70 Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”
And he denied it again. And a little after, they that stood by said again to Kepha, Surely thou art one of them: for thou art a Galilaean, and thy speech agreeth thereto.
71 Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”
But he began to curse and to swear, saying, I know not this man of whom ye speak.
72 Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.
And the second time the cock crew. And Kepha called to mind the word that Yahushua said unto him, Before the cock crow twice, thou shalt deny me thrice. And when he thought thereon, he wept.