< Marko 14 >

1 Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
Po dvou pak dnech byl hod beránka a přesnic; i hledali přední kněží a zákonníci, kterak by jej lstivě jmouce, zamordovali.
2 Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”
Ale pravili: Ne v svátek, aby snad nebyl rozbroj v lidu.
3 Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.
A když byl v Betany, v domu Šimona malomocného, a seděl za stolem, přišla žena, mající nádobu alabastrovou masti velmi drahé, z nardového koření. A rozbivši alabastrovou nádobu, vylila ji na hlavu jeho.
4 Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini?
I hněvali se někteří mezi sebou, řkouce: I proč ztráta masti této stala se?
5 Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.
Nebo mohlo toto prodáno býti, dráže než za tři sta peněz, a dáno býti chudým. I zpouzeli se na ni.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana.
Ale Ježíš řekl: Nechte jí. Proč ji rmoutíte? Dobrýť skutek učinila nade mnou.
7 Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
Však chudé máte vždycky s sebou, a když budete chtíti, můžete jim dobře činiti, ale mne ne vždycky míti budete.
8 Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu.
Ona což mohla, to učinila; předešlať, aby těla mého pomazala ku pohřebu.
9 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Amen pravím vám: Kdežkoli bude kázáno toto evangelium po všem světě, takéť i to, což učinila tato, bude vypravováno na památku její.
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao.
Tedy Jidáš Iškariotský, jeden ze dvanácti, odšel k předním kněžím, aby jim ho zradil.
11 Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.
Oni pak uslyševše, zradovali se, a slíbili mu peníze dáti. I hledal, kterak by ho příhodně zradil.
12 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
Prvního pak dne přesnic, když velikonoční beránek zabíjín býval, řkou jemu učedlníci jeho: Kde chceš, ať jdouce, připravíme, abys jedl beránka?
13 Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni.
I poslal dva z učedlníků svých, a řekl jim: Jděte do města, a potkáť vás člověk dčbán vody nesa. Jdětež za ním.
14 Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
A kamžkoli vejde, rcete hospodáři: Mistrť praví: Kde jest večeřadlo, v němž bych jedl beránka s učedlníky svými?
15 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”
A on vám ukáže večeřadlo veliké, podlážené a připravené. Tu nám připravte.
16 Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
I odešli učedlníci jeho, a přišli do města, a nalezli tak, jakož jim byl pověděl. I připravili beránka.
17 Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
Když pak byl večer, přišel se dvanácti.
18 Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
A když seděli za stolem a jedli, řekl Ježíš: Amen pravím vám, že jeden z vás mne zradí, kterýž jí se mnou.
19 Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
A oni se počali rmoutiti, a praviti jemu jeden každý obzvláštně: Zdali já jsem? A jiný: Zdali já?
20 Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
On pak odpověděv, řekl jim: Jeden ze dvanácti, kterýž omáčívá se mnou v mise.
21 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
Syn zajisté člověka jde, jakož psáno o něm, ale běda člověku tomu, skrze něhož Syn člověka bude zrazen. Dobré by bylo jemu, aby se byl nenarodil člověk ten.
22 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
A když oni jedli, vzav Ježíš chléb, a dobrořečiv, lámal a dával jim, řka: Vezměte, jezte, to jest tělo mé.
23 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
A vzav kalich, a díky učiniv, dal jim. A pili z něho všickni.
24 Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
I řekl jim: To jest krev má smlouvy té nové, kteráž se za mnohé vylévá.
25 Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
Amen pravím vám, žeť již více nikoli nebudu píti z plodu vinného kořene, až do onoho dne, když jej píti budu nový v království Božím.
26 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
A sezpívavše písničku, vyšli na horu Olivetskou.
27 Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
Potom řekl jim Ježíš: Všickni vy zhoršíte se nade mnou této noci. Nebo psáno jest: Bíti budu pastýře, a rozprchnou se ovce.
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
Ale když z mrtvých vstanu, předejduť vás do Galilee.
29 Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
Tedy Petr řekl jemu: Byť se pak všickni zhoršili, ale já nic.
30 Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
I řekl jemu Ježíš: Amen pravím tobě, že dnes této noci, prvé než kohout po dvakrát zazpívá, třikrát mne zapříš.
31 Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
On pak mnohem více mluvil: Bychť pak měl s tebou i umříti, nikoliť nezapřím tebe. A takž také i všickni mluvili.
32 Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
I přišli na místo, kterémuž jméno Getsemany. Tedy řekl učedlníkům svým: Seďtež tuto, až se pomodlím.
33 Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
A pojav s sebou Petra a Jakuba a Jana, počal se lekati a velmi teskliv býti.
34 Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
I dí jim: Smutnáť jest duše má až k smrti. Počekejtež tuto a bděte.
35 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
A poodšed maličko, padl na zemi a modlil se, aby, bylo-li by možné, odešla od něho hodina ta.
36 Akasema, “Abba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
I řekl: Abba, Otče, všecko jest možné tobě. Přenes kalich tento ode mne, ale však ne, což já chci, ale co ty.
37 Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
I přišel a nalezl je, ani spí. I řekl Petrovi: Šimone, spíš? Nemohl-lis jediné hodiny bdíti?
38 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Bděte a modlte se, abyste nevešli v pokušení. Duchť zajisté hotov jest, ale tělo nemocno.
39 Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
A opět odšed, modlil se, táž slova mluvě.
40 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.
A navrátiv se, nalezl je, ani opět spí, (nebo oči jejich byly obtíženy; ) aniž věděli, co by jemu odpověděli.
41 Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
I přišel po třetí, a řekl jim: Spětež již a odpočívejte; dostiť jest. Přišlať ta hodina; aj, Syna člověka zrazují v ruce hříšných.
42 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Vstaňte, poďme. Aj, kterýž mne zrazuje, blízkoť jest.
43 Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.
A hned, když on ještě mluvil, přišel Jidáš, kterýž byl jeden ze dvanácti, a s ním zástup veliký s meči a s kyjmi, od předních kněží a od zákonníků a starších.
44 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”
Zrádce pak jeho byl jim dal znamení, řka: Kteréhožkoli políbím, tenť jest; jmětež ho, a veďte opatrně.
45 Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.” Akambusu.
A přišed, hned přistoupiv k němu, řekl: Mistře, Mistře, a políbil ho.
46 Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi.
Tedy oni vztáhli naň ruce své, a jali jej.
47 Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
Jeden pak z těch, kteříž tu okolo stáli, vytrh meč, udeřil služebníka nejvyššího kněze, a uťal jemu ucho.
48 Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
I odpověděv Ježíš, řekl jim: Jako na lotra vyšli jste s meči a s kyjmi, abyste mne jali?
49 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”
Na každý den býval jsem u vás, uče v chrámě, a nejali jste mne. Ale aby se naplnila písma.
50 Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.
Tedy opustivše jej, všickni utekli.
51 Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata,
Jeden pak mládenček šel za ním, odín jsa rouchem lněným po nahém těle. I popadli jej mládenci.
52 alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.
On pak opustiv roucho, nahý utekl od nich.
53 Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja.
I přivedli Ježíše k nejvyššímu knězi, a sešli se k němu všickni přední kněží i starší i zákonníci.
54 Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.
Petr pak šel za ním zdaleka až na dvůr nejvyššího kněze; i seděl s služebníky, zhřívaje se u ohně.
55 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.
Ale přední kněží i všecka ta rada hledali proti Ježíšovi svědectví, aby jej na smrt vydali, a však nenalezli.
56 Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.
Nebo ač mnozí křivé svědectví vydávali proti němu, však svědectví jejich nebyla jednostejná.
57 Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:
Tedy někteří povstavše, křivé svědectví dávali proti němu, řkouce:
58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’”
My jsme slyšeli tohoto, že řekl: Já zbořím chrám tento rukou udělaný, a ve třech dnech jiný ne rukou udělaný postavím.
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.
Ale ani to jejich svědectví nebylo jednostejné.
60 Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
Tedy povstav nejvyšší kněz u prostřed, otázal se Ježíše, řka: Neodpovídáš ničeho, což tito na tebe svědčí?
61 Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”
Ale on mlčel, a nic neodpověděl. Opět nejvyšší kněz otázal se ho a řekl jemu: Jsi-liž ty Kristus, ten Syn toho Požehnaného?
62 Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
A Ježíš řekl: Jáť jsem, a uzříte Syna člověka, an sedí na pravici moci Boží, a přichází s oblaky nebeskými.
63 Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?
Tedy nejvyšší kněz roztrh roucha svá, řekl: I což ještě potřebujeme svědků?
64 Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.
Slyšeli jste rouhání. Co se vám zdá? Oni pak všickni potupili jej, že jest hoden smrti.
65 Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.
I počali někteří naň plvati, a tvář jeho zakrývati, a jej poličkovati, a říkati jemu: Prorokuj. A služebníci kyji jej bili.
66 Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu.
A když byl Petr v síni dole, přišla jedna z děvek nejvyššího kněze.
67 Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
A uzřevši Petra, an se ohřívá, a popatřivši naň, dí: I ty s Ježíšem Nazaretským byl jsi.
68 Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.
Ale on zapřel, řka: Aniž vím, ani rozumím, co ty pravíš. I vyšel ven před síň, a kohout zazpíval.
69 Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”
Tedy děvka, uzřevši jej opět, počala praviti těm, kteříž tu okolo stáli, že tento z nich jest.
70 Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”
A on opět zapřel. A po malé chvíli opět ti, kteříž tu stáli, řekli Petrovi: Jistě z nich jsi, nebo i Galilejský jsi, i řeč tvá podobná jest.
71 Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”
On pak počal se proklínati a přisahati: Neznám člověka toho, o němž pravíte.
72 Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.
A hned po druhé kohout zazpíval. I rozpomenul se Petr na slovo, kteréž byl řekl jemu Ježíš: Že prvé než kohout dvakrát zazpívá, třikrát mne zapříš. A vyšed, plakal.

< Marko 14 >