< Marko 14 >
1 Zilikuwa zimebaki siku mbili tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka, na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
GUAJA dos na jaane antes di guipot y pascua yan y taelibadura na pan: ya y magas mamale sija, yan y escriba sija, maaliligao jaftaemano para umafababa, ya umacone, ya umapuno.
2 Lakini walisema, “Tusilifanye jambo hili wakati wa Sikukuu, maana watu wanaweza wakafanya ghasia.”
Lao ilegñija: Munga gui guipot na jaane, sa noseaja uguaja atboroto ni y taotao sija.
3 Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni aliyekuwa na ukoma. Wakati alipokuwa ameketi mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akamiminia hayo manukato kichwani mwa Yesu.
Ya anae estaba guiya Betania, gui guima Simon y ategtog, ya matachong gui lamasa para uchocho; mato un palaoan mañuñule un alabastro na boteyan inggüenten puro nardo, na gosguaguan; ya mafag y boteya, ya jachuda gui jilo y ilon Jesus.
4 Baadhi ya watu waliokuwepo pale walikuwa wakisemezana wao kwa wao, “Upotevu huu wote ni wa nini?
Ya guaja sija ninafanbubo sanjalomñija, ya ilegñija: Jafa este na inggüente na manalalastimaja?
5 Mafuta haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari 300, na fedha hizo wakapewa maskini.” Wakamkemea vikali huyo mwanamke.
Maulegña umabende pot tresientos peseta, ya ufanmanae y mamobble: ya malalatde y palaoan.
6 Lakini Yesu akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Mwacheni! Yeye amenitendea jambo zuri sana.
Lao si Jesus ilegña: Pologüe namaesa. Jafaja na inatbororota güe? Mauleg finatinasña nu guajo.
7 Maskini mtakuwa nao siku zote na mnaweza kuwasaidia wakati wowote mnaotaka. Lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.
Sa manjajamyoja yan y mamobble siempre; ya ngaeanja nae manmalago jamyo, infatinasja mauleg guiya sija: lao guajo ti tafanjijitaja siempre.
8 Huyu mwanamke amenitendea lile aliloweza. Ameumiminia mwili wangu manukato ili kuniandaa kwa maziko yangu.
Güiya jafatinas taemanoja y ninasiñaña: güiya mato antes, para uinggüentiye y tataotaojo, para y naftan.
9 Amin, nawaambia, mahali popote ulimwenguni ambapo Injili itahubiriwa, jambo hili alilolitenda huyu mwanamke litatajwa pia kwa ukumbusho wake.”
Magajet jusangane jamyo: Manoja este na ebangelio nae mapredica, gui todo y tano, este locue y finatinasña umasangan, para memoriasña.
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa viongozi wa makuhani ili kumsaliti Yesu kwao.
Ya si Judas Iscariote, uno gui dose, mapos malag y magas mamale, para umentrega güe guiya sija.
11 Walifurahi sana kusikia jambo hili na wakaahidi kumpa fedha. Hivyo yeye akawa anatafuta wakati uliofaa wa kumsaliti.
Ya anae majungog, ninafansenmagof, ya mapromete manae güe salape. Ya jaaliligao jaftaemano para uinentrega.
12 Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo kwa desturi mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, “Unataka twende wapi ili tukuandalie mahali pa kula Pasaka?”
Ya y finenana na jaane y taelibadura na pan, anae maofrese y pascua, y disipuluña ilegñija nu güiya; Manojam malagomo guato ya infamauleg nae para unchocho gui pascua?
13 Basi akawatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake, akawaambia, “Nendeni mjini. Huko mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni.
Ya jatago y dos gui disipuluña, ya ilegña nu sija: Janao fanmalag y siuda, sa infanasoda güije yan un taotao na mangangatga un jarran janom: dalalag güe.
14 Mwambieni mwenye nyumba ile atakayoingia, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba changu cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
Ya amanoja nae jumalom, alog ni y taotao guma: Y Maestro, ilegña: Mangue y aposento ni y anae para infañocho gui pascua yan y disipulujo?
15 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kilichopambwa tena kilicho tayari. Tuandalieni humo.”
Ya güiya infanfinanue un dangculo na cuatto; esta mafamauleg yan listo; ayo nae famauleg para jita.
16 Wale wanafunzi wakaondoka na kwenda mjini, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
Ya y disipuluña sija manmapos, ya manmato gui siuda, ya jasoda jaftaemano y mansinangane sija: ya mafamauleg para y pascua.
17 Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wale wanafunzi wake kumi na wawili.
Ya y pupuenge mato yan y dose.
18 Walipoketi mezani wakila, Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti, mmoja anayekula pamoja nami.”
Ya anae manmatatachong ya mañochocho, si Jesus ilegña: Magajet jusangane jamyo: Uno guiya jamyo umentregayo; güiyaja uchumocho yan guajo.
19 Wakaanza kuhuzunika na kumuuliza mmoja baada ya mwingine, “Je, ni mimi Bwana?”
Ayo nae ninafangostriste, ya ilegñija nu güiya uno yan otro: Guajo? y otro ilegña: Guajo?
20 Akawajibu, “Ni mmoja miongoni mwenu ninyi kumi na wawili, yule anayechovya mkate kwenye bakuli pamoja nami.
Ayo nae manope ilegña nu sija: Uno gui dose ni y jumajame manotche gui tason.
21 Mwana wa Adamu anaenda zake kama vile alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule amsalitiye Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu huyo kama hangezaliwa.”
Y Lajin taotao magajet na mapos, ni y esta matugue pot güiya: lao namaase ayo na taotao ni y jaentrega y Lajin taotao. Maulegña ayo na taotao na ti umafañago.
22 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
Ya anae mañochocho, jachule si Jesus y pan, ya jabendise, ya jaipe, ya janae sija, ilegña: Chile ya incano, sa este y tataotaojo.
23 Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
Ya jachule y posuelo, ya anae munjayan janae grasia, janae sija: ya todos manguimen.
24 Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
Ya ilegña nu sija: Este y jâgâjo, gui nuebo na testamento, ni machuda pot y megae.
25 Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
Magajet jusangane jamyo, na ti juguimen talo ni y tinegcha ubas, asta ayo na jaane, na juguimen nuebo gui raenon Yuus.
26 Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
Ya anae munjayan macanta un himno, manmapos manmalag y finabeca Olibo.
27 Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: “‘Nitampiga mchungaji, nao kondoo watatawanyika.’
Ya si Jesus ilegña nu sija: Todos jamyo infaninefende pot guajo; sa esta matugue: Bae jupanag y pastot, ya y quinilo sija ufanmachalapon.
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
Lao despues di lâlâyo talo, ya cumajuloyo, jujanao esta y menanmiyo guiya Galilea.
29 Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
Ayo nae si Pedro ilegña: Achogja todos maninefende; lao guajo aje.
30 Yesu akamwambia, “Amin, nakuambia; leo, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, wewe mwenyewe utanikana mara tatu.”
Ya sinangane as Jesus ilegña: Magajet jusanganejao na jago pagoja na puenge, antes qui uoo dos biaje y gayo, unpuneyo tres biaje.
31 Lakini Petro akasisitiza zaidi, “Hata kama itabidi kufa pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Nao wale wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Lao guiya janaguefchadeg y cuentosña, ilegña: Yanguin jumitamatae, ti jupunejao ni jaftaemano. Taegüineja locue sinanganñija todos.
32 Wakaenda mahali paitwapo Gethsemane. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa, nami niende nikaombe.”
Ya manmato un lugat na y naaña Gethsemane: ya ilegña ni y disipuluña sija: Fanmatatachong güine, mientras mananaetaeyo.
33 Kisha akawachukua pamoja naye Petro, Yakobo na Yohana. Akaanza kuhuzunika sana na kutaabika.
Ya jacone gachongña si Pedro, yan si Santiago, yan si Juan, ya jatutujon manmajalang, yan mangostriste,
34 Akawaambia, “Moyo wangu umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mkeshe.”
Ya ilegña nu sija: Y antijo sentriste asta qui jumatae; fañaga güine, ya iafanmamulan.
35 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akaomba kwamba kama ingewezekana saa hiyo ya mateso imwondokee.
Ya jumanao mona didide, dumimo papa gui jilo oda, ya manaetae, na yanguin siña, ufalofan y ora guiya güiya.
36 Akasema, “Abba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo mimi, bali vile upendavyo wewe.”
Ya ilegña: Abba, Tata: todo y güinaja mansiña para jago; nasuja este y posuelo guiya guajo: lao ti taemanoja minalagojo, na y minalagomo.
37 Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Je, hukuweza kukesha hata kwa saa moja?
Ya mato talo guato ya jasoda sija manmaego, ya ilegña as Pedro: Simon mamaegojao? ti siñajao bumela un oraja?
38 Kesheni na mwombe, msije mkaingia majaribuni. Roho iko radhi, lakini mwili ni mdhaifu.”
Fanbela, yan infanmanaetae; para chamiyo fanjajalom gui tentasion: Y Espiritu magajet na malago; lao y catne echecho.
39 Akaenda tena kuomba, akisema maneno yale yale.
Ya jumanao talo ya manaetae ya ayoja mismo na sinangan.
40 Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa sababu macho yao yalikuwa mazito. Nao hawakujua la kumwambia.
Ya anae tumalo guato jasoda talo sija na manmamaego: sa y atadogñija mangosmacat, ya ti ujatungo jafa umaope güe.
41 Akaja mara ya tatu, akawaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imewadia. Tazameni, Mwana wa Adamu anasalitiwa na kutiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Ya mato talo gui mina tres biaje, ya ilegña nu sija: Fanmaego pago, ya infandescansa: esta najong; y ora esta mato; lie y Lajin taotao na maentrega gui canae y manisao sija.
42 Inukeni, twende zetu! Tazameni, msaliti wangu yuaja!”
Fangajulo ya nije tafanjanao; sa esta y umentregayo jijot.
43 Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili, akatokea. Alikuwa amefuatana na umati wa watu wenye panga na marungu, waliokuwa wametumwa na viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, na wazee.
Ya enseguidas, mientras cumuecuentos, mato si Judas, uno gui dose, ya mañisija yan un linajyan taotao, manmañuñule espada, yan galute guinen y magas mamale, yan y escriba, yan y manamco sija.
44 Basi msaliti alikuwa amewapa hao watu ishara, kwamba: “Yule nitakayembusu ndiye. Mkamateni, mkamchukue chini ya ulinzi.”
Ya ayo y umentrega güe, mannae señat, ilegña: Jaye y juchico, güiya ayo: guiot ya inquene na seguro.
45 Mara Yuda akamjia Yesu na kusema, “Rabi.” Akambusu.
Ya enseguidas nae matogüe, jumajanaoja guato guiya güiya, ya ilegña: Maestro; ya jachico.
46 Wale watu wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi.
Ya ayonae mapolo canae sija gui jiloña ya macone.
47 Ndipo mmoja wa wale waliokuwa wamesimama karibu aliuchomoa upanga wake na kumpiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio.
Ya uno guiya sija ni y tumotojgue gui oriya, jalagnos y espadaña, ya jataga y tentago y magas mamale, ya jautut talangaña.
48 Kisha Yesu akawaambia, “Mmekuja na panga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
Ya manope si Jesus ilegña nu sija: Ada manmato jamyo calang contra y saque, na manmañuñule jamyo espada, yan galute para inguiotyo?
49 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni, wala hamkunikamata. Lakini Maandiko sharti yatimie.”
Guinen manjijitaja todo y jaane gui templo manmamananagüe, ya ti inquequeneyo? lao mafatinas este para umacumple y tinigue.
50 Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.
Ya madingo, ya manmalago todos.
51 Kijana mmoja, ambaye hakuwa amevaa kitu isipokuwa alijitanda nguo ya kitani, alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata,
Ya dinalalaggüe un patgon na taotao, na jatatampe güe un sábanas, sa taya magagago: ya y mamatgon sija na taotao, maguot güe.
52 alikimbia uchi, akaliacha vazi lake.
Lao güiya japolo y sábanas, ya malago sin magago.
53 Wakampeleka Yesu kwa kuhani mkuu, nao viongozi wa makuhani wote, na wazee na walimu wa sheria wote wakakusanyika pamoja.
Ya macone si Jesus para y magas na pale: ya mandaña y manmagas mamale yan y manamco, yan y escriba sija.
54 Petro akamfuata kwa mbali, hadi uani kwa kuhani mkuu. Huko akaketi pamoja na walinzi, akiota moto.
Ya si Pedro dinalalag güe, lao chago, asta gui sanjalom, sanjalom y palasyon y magas na pale: ya matachong yan y tentago sija, ya janama maope güe gui guafe.
55 Viongozi wa makuhani na Baraza la Wayahudi lote wakatafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumuua. Lakini hawakupata jambo lolote.
Ya y magas mamale, yan todo y inetnon ofisiat, manmanaliligao testimonio contra si Jesus para umapuno; lao taya masoda.
56 Wengi walitoa ushahidi wa uongo dhidi yake, lakini maelezo yao hayakukubaliana.
Sa megae manmannae ti manmagajet na testimonio contra güiya: lao y testimonioñija ti manparejo.
57 Ndipo wengine wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo dhidi yake, wakisema:
Ya mangajulo palo ni manmannae contra güiya y testimonio na ti manmagajet, ilegñija:
58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitalibomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga jingine ambalo halikujengwa na wanadamu.’”
Injingog y ilegña: Juyulang este na templo, ni y mafatinas nu canae, ya y tres na jaane, janacajulo talo otro na ti finatinas canae.
59 Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukukubaliana.
Lao este na testimonioñija, locue ti manparejo.
60 Basi kuhani mkuu akasimama mbele yao, akamuuliza Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni ushahidi gani hawa watu wanauleta dhidi yako?”
Ya y magas na pale tumojgue julo gui talolo, ya jafaesen si Jesus ilegña: Ti unfanope ni jafa? Jafa este sija na testimonioñija contra jago?
61 Lakini Yesu akakaa kimya, hakusema neno lolote. Kuhani mkuu akamuuliza tena, “Je, wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu Aliyebarikiwa?”
Lao mamatquiquiloja, taya inepeña. Tumalo y magas na pale finaesen ilegña: Jago si Jesucristo Lajin y Bendito?
62 Yesu akajibu, “Mimi ndimi. Nanyi mtamwona Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa kuume wa Mwenye Nguvu, na akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
Ya si Jesus ilegña: Guajo; ya umamaela y tiempo anae inlie y Lajin taotao matatachong gui agapa y gaeninasiña na canae, ya umamaela gui jalom y mapagajes y langet.
63 Kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi zaidi?
Ayonae y magas na pale, jatiteg y magaguña, ya ilegña: Para jafajit palo testigo sija?
64 Ninyi mmesikia hayo makufuru. Uamuzi wenu ni gani?” Wote wakamhukumu kwamba anastahili kifo.
Injingogja y chinatfinoña contra si Yuus: Jafa jinasonmimiyo? Ya todos manmañentensia para umapuno.
65 Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa machoni, wakampiga kwa ngumi na kumwambia, “Tabiri!” Walinzi wakamchukua na kumpiga makofi.
Ya y palo matutujon matolae, yan matatampe mataña, yan mapatmada, ya ilegñija nu güiya: Profetisa: ya y ofisiat sija rumesibe güe ya japatmada ni y canaeñija.
66 Petro alipokuwa bado yuko chini kwenye ua wa jumba la kifalme, tazama akaja mmoja wa watumishi wa kike wa kuhani mkuu.
Ya anae si Pedro gaegue gue sanpapa gui palasyo, mato un palaoan tentago y magas na pale:
67 Alipomwona Petro akiota moto, akamtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
Ya anae jalie si Pedro na janamamaepe güe, jaatan ya ilegña: Jago locue manjajamyo yan si Jesus Nasareno?
68 Lakini Petro akakana, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema.” Naye akaondoka kuelekea kwenye njia ya kuingilia.
Lao jadague ilegña: Ti jutungo, ni jutungo jafa ilelegmo. Ya mapos juyong gui cajida; ya umoo y gayo.
69 Yule mtumishi wa kike alipomwona mahali pale, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama hapo, “Huyu mtu ni mmoja wao.”
Ya linie talo ni y palaoan, ya jatutujon sumangane ayo sija y manotojgue gui oriyaña: Este uno guiya sija.
70 Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo karibu na Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!”
Ya jadague talo. Ti apmam ayo y manotojgue gui oriya ilegñija as Pedro: Magajet na jago uno guiya sija? sa jago taotao Galileajao.
71 Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui huyu mtu mnayesema habari zake!”
Lao jatutujon mamatdise yan manjula ya ilegña: Ti jutungo este na taotao y insasangan.
72 Papo hapo jogoo akawika mara ya pili. Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alikuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akavunjika moyo, akalia sana.
Ya enseguidas y mina dos biaje umoo y gayo. Jajaso si Pedro y sinangan, jaftaemano si Jesus nu güiya ilegña: Antes que uoo y gayo dos biaje, undagueyo tres biaje. Ya anae jajaso, tumanges.