< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitoka Hekaluni, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”
anantaraM mandirAd bahirgamanakAle tasya shiShyANAmekastaM vyAhR^itavAn he guro pashyatu kIdR^ishAH pAShANAH kIdR^ik cha nichayanaM|
2 Ndipo Yesu akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”
tadA yIshustam avadat tvaM kimetad bR^ihannichayanaM pashyasi? asyaikapAShANopi dvitIyapAShANopari na sthAsyati sarvve. adhaHkShepsyante|
3 Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani,
atha yasmin kAle jaitungirau mandirasya sammukhe sa samupaviShTastasmin kAle pitaro yAkUb yohan Andriyashchaite taM rahasi paprachChuH,
4 “Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”
etA ghaTanAH kadA bhaviShyanti? tathaitatsarvvAsAM siddhyupakramasya vA kiM chihnaM? tadasmabhyaM kathayatu bhavAn|
5 Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye.
tato yAshustAn vaktumArebhe, kopi yathA yuShmAn na bhrAmayati tathAtra yUyaM sAvadhAnA bhavata|
6 Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi.
yataH khrIShTohamiti kathayitvA mama nAmnAneke samAgatya lokAnAM bhramaM janayiShyanti;
7 Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado.
kintu yUyaM raNasya vArttAM raNADambara ncha shrutvA mA vyAkulA bhavata, ghaTanA etA avashyammAvinyaH; kintvApAtato na yugAnto bhaviShyati|
8 Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.
deshasya vipakShatayA desho rAjyasya vipakShatayA cha rAjyamutthAsyati, tathA sthAne sthAne bhUmikampo durbhikShaM mahAkleshAshcha samupasthAsyanti, sarvva ete duHkhasyArambhAH|
9 “Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao.
kintu yUyam AtmArthe sAvadhAnAstiShThata, yato lokA rAjasabhAyAM yuShmAn samarpayiShyanti, tathA bhajanagR^ihe prahariShyanti; yUyaM madarthe deshAdhipAn bhUpAMshcha prati sAkShyadAnAya teShAM sammukhe upasthApayiShyadhve|
10 Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia.
sheShIbhavanAt pUrvvaM sarvvAn deshIyAn prati susaMvAdaH prachArayiShyate|
11 Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.
kintu yadA te yuShmAn dhR^itvA samarpayiShyanti tadA yUyaM yadyad uttaraM dAsyatha, tadagra tasya vivechanaM mA kuruta tadarthaM ki nchidapi mA chintayata cha, tadAnIM yuShmAkaM manaHsu yadyad vAkyam upasthApayiShyate tadeva vadiShyatha, yato yUyaM na tadvaktAraH kintu pavitra AtmA tasya vaktA|
12 “Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe.
tadA bhrAtA bhrAtaraM pitA putraM ghAtanArthaM parahasteShu samarpayiShyate, tathA patyAni mAtApitro rvipakShatayA tau ghAtayiShyanti|
13 Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.
mama nAmahetoH sarvveShAM savidhe yUyaM jugupsitA bhaviShyatha, kintu yaH kashchit sheShaparyyantaM dhairyyam AlambiShyate saeva paritrAsyate|
14 “Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani.
dAniyelbhaviShyadvAdinA proktaM sarvvanAshi jugupsita ncha vastu yadA tvayogyasthAne vidyamAnaM drakShatha (yo janaH paThati sa budhyatAM) tadA ye yihUdIyadeshe tiShThanti te mahIdhraM prati palAyantAM;
15 Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote.
tathA yo naro gR^ihopari tiShThati sa gR^ihamadhyaM nAvarohatu, tathA kimapi vastu grahItuM madhyegR^ihaM na pravishatu;
16 Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.
tathA cha yo naraH kShetre tiShThati sopi svavastraM grahItuM parAvR^itya na vrajatu|
17 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!
tadAnIM garbbhavatInAM stanyadAtrINA ncha yoShitAM durgati rbhaviShyati|
18 Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi.
yuShmAkaM palAyanaM shItakAle yathA na bhavati tadarthaM prArthayadhvaM|
19 Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe.
yatastadA yAdR^ishI durghaTanA ghaTiShyate tAdR^ishI durghaTanA IshvarasR^iShTeH prathamamArabhyAdya yAvat kadApi na jAtA na janiShyate cha|
20 Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo.
apara ncha parameshvaro yadi tasya samayasya saMkShepaM na karoti tarhi kasyApi prANabhR^ito rakShA bhavituM na shakShyati, kintu yAn janAn manonItAn akarot teShAM svamanonItAnAM hetoH sa tadanehasaM saMkShepsyati|
21 Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristohuyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki.
anyachcha pashyata khrIShTotra sthAne vA tatra sthAne vidyate, tasminkAle yadi kashchid yuShmAn etAdR^ishaM vAkyaM vyAharati, tarhi tasmin vAkye bhaiva vishvasita|
22 Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule.
yatoneke mithyAkhrIShTA mithyAbhaviShyadvAdinashcha samupasthAya bahUni chihnAnyadbhutAni karmmANi cha darshayiShyanti; tathA yadi sambhavati tarhi manonItalokAnAmapi mithyAmatiM janayiShyanti|
23 Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.
pashyata ghaTanAtaH pUrvvaM sarvvakAryyasya vArttAM yuShmabhyamadAm, yUyaM sAvadhAnAstiShThata|
24 “Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki, “‘jua litatiwa giza nao mwezi hautatoa nuru yake;
apara ncha tasya kleshakAlasyAvyavahite parakAle bhAskaraH sAndhakAro bhaviShyati tathaiva chandrashchandrikAM na dAsyati|
25 nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’
nabhaHsthAni nakShatrANi patiShyanti, vyomamaNDalasthA grahAshcha vichaliShyanti|
26 “Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu.
tadAnIM mahAparAkrameNa mahaishvaryyeNa cha meghamAruhya samAyAntaM mAnavasutaM mAnavAH samIkShiShyante|
27 Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.
anyachcha sa nijadUtAn prahitya nabhobhUmyoH sImAM yAvad jagatashchaturdigbhyaH svamanonItalokAn saMgrahIShyati|
28 “Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
uDumbarataro rdR^iShTAntaM shikShadhvaM yadoDumbarasya taro rnavInAH shAkhA jAyante pallavAdIni cha rnigachChanti, tadA nidAghakAlaH savidho bhavatIti yUyaM j nAtuM shaknutha|
29 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni.
tadvad etA ghaTanA dR^iShTvA sa kAlo dvAryyupasthita iti jAnIta|
30 Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
yuShmAnahaM yathArthaM vadAmi, AdhunikalokAnAM gamanAt pUrvvaM tAni sarvvANi ghaTiShyante|
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
dyAvApR^ithivyo rvichalitayoH satyo rmadIyA vANI na vichaliShyati|
32 “Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake.
apara ncha svargasthadUtagaNo vA putro vA tAtAdanyaH kopi taM divasaM taM daNDaM vA na j nApayati|
33 Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia.
ataH sa samayaH kadA bhaviShyati, etajj nAnAbhAvAd yUyaM sAvadhAnAstiShThata, satarkAshcha bhUtvA prArthayadhvaM;
34 Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.
yadvat kashchit pumAn svaniveshanAd dUradeshaM prati yAtrAkaraNakAle dAseShu svakAryyasya bhAramarpayitvA sarvvAn sve sve karmmaNi niyojayati; aparaM dauvArikaM jAgarituM samAdishya yAti, tadvan naraputraH|
35 “Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko.
gR^ihapatiH sAyaMkAle nishIthe vA tR^itIyayAme vA prAtaHkAle vA kadAgamiShyati tad yUyaM na jAnItha;
36 Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala.
sa haThAdAgatya yathA yuShmAn nidritAn na pashyati, tadarthaM jAgaritAstiShThata|
37 Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’”
yuShmAnahaM yad vadAmi tadeva sarvvAn vadAmi, jAgaritAstiShThateti|

< Marko 13 >