< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitoka Hekaluni, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”
Yesu bho igenda kuh'omela ku lihekalu mmonga ghwa bhanafunzi bha muene akan'kota, “Mwalimu, langayi maganga agha gha kusyangasya ni majengo!”
2 Ndipo Yesu akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”
Akan'jobhela, ghwilola majengo agha mabhaha? Lijhelepi hata liganga limonga lyalibetakubakila panani pa lenge ambalyo libetakubinisibhwa pasi”.
3 Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani,
Na muene bho atamili panani pa kidonda kya Mizeituni kunyuma ku lihekalu, Petro, Yakobo, Yohana ni Andrea bhakan'kota kwa siri,
4 “Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”
Tujobhilayi, mambo agha ghibeta kujha ndali? Na kiki dalili gha mambo agha kuh'omela?”
5 Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye.
Yesu akajhanda kubhajobhela, “Mujhiajhi makini kwamba asihidi munu kubhapotosya.
6 Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi.
Bhingi bhibeta kuhida kwa lihina lya nene bhibeta kujobha, 'Nene ndiye', na bhibetakubhapotosya bhingi.
7 Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado.
Pa mwibeta kup'eleka vita ni tetesi sya vita, musitili; mambo agha ghilondeka kuh'omela lakini mwisho bado.
8 Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.
Taifa libeta kujhinuka kinyume ni litaifa l'enge, ni bhufalme kinyume ni bhufalme. Pibeta kujha ni matetemeku sehemu mbalimbali ni njala. Obho ndo mwanzo ghwa bhutungu.
9 “Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao.
Mujhelayi mihu. Bhibetakubhapeleka mpaka mabarazani, na mwibetakupingibhwa mu masinagogi. Mwibetakujhemikibhwa mbele jha bhatawala ni bhafalme kwa ndabha jha nene, kama bhushuhuda bhwa bhene.
10 Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia.
Lakini injili lazima hoti ihubiribhwayi kwa mataifa ghoha.
11 Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.
Pabhibeta kubhakamula ni kubhakabidhi, musitili kuhusu khela kya mwibeta kujobha. Ndani jha muda obhu, mwibetakupelibhwa kiki kya kujobha; Mwibeta lepi kujha muenga mwilongila, bali Roho mtakatifu.
12 “Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe.
Ndugu ibetakun'shtaki ndugu kukomibhwa, Dadi ni mwana munu. Bhana bhibeta kujhama kinyume ni Dadi jhabhi ni kusababisya kukomibhwa.
13 Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.
Mwibetakudadibhwa ni khila munu kwa ndabha jha lihina lya nene. Lakini jha ibetakuvumilila mpaka kumuisu, munu ojhu ibeta kuokoka.
14 “Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani.
Pamwibetakubhona lichukizo lya bhuharibifu lijhemili pala palilondeka lepi kujhema (jhaisoma na amanyayi), ndipo bhabhajhele mugati mwa Yuda bhajumbililayi kukidonda,
15 Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote.
nu muene jha ajhele kunani pa nyumba asiseleli pasi pa nyumba, au kutola kyokyoha kyekijhele kwibhala,
16 Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.
na jhaajhele kun'gonda asikerebhuki kulota liguanda lya muene.
17 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!
Lakini ole bhabhi bhadala bha bhajhele ni luleme ni bhabhijhong'esya mu magono aghu!
18 Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi.
Mus'omelayi kujha jhisih'omeli wakati bhwa mepu.
19 Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe.
Kwani pibeta kujha ni malombosi mabhaha, ambagho ghabhwayilepi kuh'omela, kuhomela K'yara abhubhombili bhulimwengu, mpaka henu, ijhelepi, wala jhibetalepi kuh'omela kabhele.
20 Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo.
Mpaka Bwana paibetakup'ongosya magono, ghujhelepi mb'ele ghwa ghwibeta kuokoka, lakini kwa ndabha jha bhateule, jhaibeta kubhahagula, ibetakup'ongosya namba sya magono.
21 Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristohuyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki.
Wakati obhu kama munu jhejhioha ibetakubhajobhela, langai, Kristu ajhele apa!' au 'Langai, ajhe pala!' musiamini.
22 Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule.
Kwani bhakristu bha bhudesi ni manabii bha bhudesi bhibeta kuh'omela ni kulasya ishara ni maajabu ili kwamba, bhabhakofiajhi, yamkini hata bhateule.
23 Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.
Mujhiaji mihu! Nimelikubhajobhela agha ghoha kabla jha bhwakati.
24 “Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki, “‘jua litatiwa giza nao mwezi hautatoa nuru yake;
Lakini baada jha mal'ombosi gha magono aghu, lijobha libeta kus'opibhwa ngisi, muesi ghwibeta lepi kupisya mwanga ghwake,
25 nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’
Matondo ghibeta kubina kuh'omela kunani ni nghofu syasijhele kumbinguni sibetakutikisika.
26 “Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu.
Ndipo pabhibeta kumbona mwana ghwa Adamu ihida mumabhengu kwa nghofu mbaha ni bhutukufu.
27 Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.
Ndipo paibeta kutuma malaika bha muene na ibeta kubhabhonganya pamonga bhateule bha muene kuh'omela pande mbaha nne sya dunia, kuh'omela mwisho ghwa dunia mpaka mwisho ghwa mbingu.
28 “Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
Kwa mtini mwikimanyisijhi. Kama tawi kyalibhwesya kupisya ni kubheka haraka mat'ondo ghake, ndipo mwibeta kumanya kujha kilolelu kijhe karibu.
29 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni.
Ndo kyajhijhele pamwibetakubhona mambo agha ghih'omela, mumanyayi kujha ajhele karibu, ni malango.
30 Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Bhokweli, nikabhajobhela, kizazi ekhe kibetap'etalepi patali kabla mambo agha ghah'omili lepi.
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Mbingu ni nchi sibeta kup'eta, lakini malobhi ghangu ghibeta lepi kup'eta kamwe.
32 “Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake.
Lakini kuhusu ligono elu au saa ajhelepi jha ibeta kumanya, hata malaika bha kumbinguni, wala mwana, ila Dadi.
33 Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia.
Mujhelayi mihu Langayi, kwa ndabha mumanyilepi ni muda bholoki ghibeta kuh'omela. (zingatilayi: N'sitari obho, “Mujhelayi bhaangalifu, mulangayi na mus'okayi kwa ndabha...” bhujhelepi mu nakala sya muandi).
34 Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.
Ni kama munu jhailota ku safuari: alekili nyumba jha muene, ni kumbeka n'tumwa ghwa muene kujha ntawala ghwa nyumba, khila mmonga ni mbombo jha muene. Ni kumwamuru mlinzi kutama mihu.
35 “Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko.
Henu mujhelayi mihu! kwani mumanyilepi bwana ghwa nyumba pa ibeta kubhujhe kunyumba, jhibhwesekana kimihi kilukya manane, wakati likongobha palibeta kubheka, au lukhela.
36 Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala.
Kama ahidili ghafla, asikukoleli ugonili.
37 Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’”
Khela kyanikakijobha kwa bhebhe, nikakijobha kwa kila munu: Mukeshayi”!

< Marko 13 >