< Marko 12 >

1 Yesu akaanza kusema nao kwa mifano, akawaambia: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akachimba shimo ndani yake kwa ajili ya shinikizo la kusindika divai, na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha shamba hilo la mizabibu kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwenda nchi nyingine.
And Jhesus bigan to speke to hem in parablis. A man plauntide a vynyerd, and sette an hegge aboute it, and dalf a lake, and bildide a toure, and hiryde it to tilieris, and wente forth in pilgrimage.
2 Wakati wa mavuno ulipofika, mwenye shamba akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili kuchukua sehemu yake ya mavuno ya shamba la mizabibu kutoka kwa hao wapangaji.
And he sente to the erthe tilieris in tyme a seruaunt, to resseyue of the erthe tilieris of the fruyt of the vynyerd.
3 Lakini wale wakulima walimkamata yule mtumishi, wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
And thei token hym, and beeten, and leften hym voide.
4 Kisha yule mwenye shamba akamtuma mtumishi mwingine kwao; nao wale wakulima wakampiga kichwani na kumfanyia mambo ya aibu.
And eftsoone he sente to hem anothir seruaunt, and thei woundiden hym in the heed, and turmentiden hym.
5 Kisha akamtuma mtumishi mwingine, naye huyo wakamuua. Akawatuma wengine wengi; baadhi yao wakawapiga, na wengine wakawaua.
And eftsoone he sente another, and thei slowen hym, and othir mo, betynge summe, and sleynge othere.
6 “Mwenye shamba alikuwa bado na mmoja wa kumtuma, mwanawe aliyempenda. Hatimaye akamtuma akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
But yit he hadde a moost derworth sone, and he sente hym last to hem, and seide, Perauenture thei schulen drede my sone.
7 “Lakini wale wapangaji wakasemezana pamoja, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, nao urithi utakuwa wetu.’
But the erthetilieris seiden togidere, This is the eire; come ye, sle we hym, and the eritage schal be ourun.
8 Hivyo wakamchukua na kumuua, wakamtupa nje ya lile shamba la mizabibu.
And thei tokun hym, and killiden, and castiden out without the vynyerd.
9 “Sasa basi yule mwenye shamba atafanya nini? Atakuja na kuwaua hao wapangaji, kisha atawapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.
Thanne what schal the lord of the vynyerd do? He schal come, and lese the tilieris, and yyue the vynyerd to othere.
10 Je, hamjasoma Andiko hili: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni;
Whether ye han not red this scripture, The stoon which the bilderis han disspisid, this is maad in to the heed of the corner?
11 Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni ajabu machoni petu’?”
This thing is doon of the Lord, and is wondirful in oure iyen.
12 Walipotambua kuwa amesema mfano huo kwa ajili yao, wakataka kumkamata, lakini wakaogopa ule umati wa watu. Wakamwacha, wakaondoka, wakaenda zao.
And thei souyten to holde hym, and thei dredden the puple; for thei knewen that to hem he seide this parable; and thei leften hym,
13 Baadaye wakawatuma baadhi ya Mafarisayo na Maherode ili kwenda kumtega Yesu katika yale anayosema.
and thei wenten awei. And thei senten to hym summe of the Farisees and Erodians, to take hym in word.
14 Wakamjia, wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu. Wewe huyumbishwi na wanadamu, kwa kuwa huna upendeleo. Lakini wewe huifundisha njia ya Mungu katika kweli. Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?
Whiche camen, and seien to hym, Maistir, we witen that thou art sothfast, and reckist not of ony man; for nethir thou biholdist in to the face of man, but thou techist the weie of God in treuthe. Is it leeueful that tribute be youun to the emperoure, or we schulen not yyue?
15 Je, tulipe kodi au tusilipe?” Lakini Yesu alijua unafiki wao. Akawauliza “Mbona mnajaribu kunitega? Nileteeni hiyo dinariniione.”
Which witynge her pryuei falsnesse, seide to hem, What tempten ye me? brynge ye to me a peny, that Y se.
16 Wakamletea hiyo sarafu. Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?” Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.”
And thei brouyten to hym. And he seide to hem, Whos is this ymage, and the writyng? Thei seien to him, The emperouris.
17 Ndipo Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.” Nao wakamstaajabia sana.
And Jhesus answeride and seide to hem, Thanne yelde ye to the emperour tho thingis that ben of the emperours; and to God tho thingis that ben of God.
18 Kisha Masadukayo, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu,
And thei wondriden of hym. And Saduces, that seien that ther is no ressurreccioun, camen to hym, and axeden hym,
19 wakasema, “Mwalimu, Mose alituandikia kuwa kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
and seiden, Maister, Moyses wroot to vs, that if the brother of a man were deed, and lefte his wijf, and haue no sones, his brother take his wijf, and reise vp seed to his brother.
20 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa pasipo kuwa na mtoto yeyote.
Thanne seuene britheren ther weren; and the firste took a wijf, and diede, and lefte no seed.
21 Wa pili akamwoa yule mjane, lakini naye akafa bila kuacha mtoto yeyote. Ikawa vivyo hivyo kwa yule wa tatu.
And the secounde took hir, and he diede, and nether this lefte seed.
22 Hakuna hata mmojawapo wa hao ndugu wote saba aliyeacha mtoto. Hatimaye yule mwanamke naye akafa.
And the thridde also. And in lijk manere the seuene token hir, and leften not seed. And the womman the laste of alle `is deed.
23 Kwa hiyo wakati wa ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
Thanne in the resurreccioun, whanne thei schulen rise ayen, whos wijf of these schal sche be? for seuene hadden hir to wijf.
24 Yesu akawajibu, “Je, hampotoki kwa sababu hamfahamu Maandiko wala uweza wa Mungu?
And Jhesus answeride, and seide to hem, Whether ye erren not therfor, that ye knowe not scripturis, nethir the vertu of God?
25 Wafu watakapofufuka, hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
For whanne thei schulen rise ayen fro deeth, nether thei schulen wedde, nethir schulen be weddid, but thei schulen be as aungels of God in heuenes.
26 Basi kuhusu wafu kufufuliwa, je hamjasoma katika Kitabu cha Mose jinsi Mungu alivyosema na Mose kutoka kile kichaka akisema, ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, na Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo?’
And of deed men, that thei risen ayen, han ye not red in the book of Moises, on the buysch, hou God spak to hym, and seide, Y am God of Abraham, and God of Isaac, and God of Jacob?
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai. Kwa hiyo mmekosea kabisa.”
He is not God of deed men, but of lyuynge men; therfor ye erren myche.
28 Mwalimu mmoja wa sheria akaja, akawasikia wakijadiliana. Akiona kwamba Yesu amewajibu vyema, naye akamuuliza, “Katika amri zote, ni ipi iliyo kuu?”
And oon of the scribis, that hadde herde hem dispuytynge togidir, cam nyy, and saiy that Jhesus had wel answeride hem, and axide hym, which was the firste maundement of alle.
29 Yesu akajibu, “Amri iliyo kuu ndiyo hii: ‘Sikia ee Israeli. Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
And Jhesus answeride to him, that the firste maundement of alle is, Here thou, Israel, thi Lord God is o God;
30 Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.’
and thou schalt loue thi Lord God of al thin herte, and of al thi soule, and of al thi mynde, and of al thi myyt.
31 Ya pili ndiyo hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.”
This is the firste maundement. And the secounde is lijk to this, Thou schalt loue thi neiybore as thi silf. Ther is noon other maundement gretter than these.
32 Yule mwalimu wa sheria akamwambia Yesu, “Mwalimu, umejibu vyema kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye.
And the scribe seide to hym, Maister, in treuthe thou hast wel seid; for o God is, and ther is noon other, outakun hym;
33 Kumpenda Mungu kwa moyo wote na kwa akili zote na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama mtu anavyojipenda mwenyewe ni bora zaidi kuliko kutoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu zote.”
that he be loued of al the herte, and of al the mynde, and of al the vndurstondynge, and of al the soule, and of al strengthe, and to loue the neiybore as hym silf, is gretter than alle brent offryngis and sacrifices.
34 Yesu alipoona kwamba amejibu kwa busara, akamwambia, “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.” Tangu wakati huo, hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
And Jhesus seynge that he hadde answerid wiseli, seide to hym, Thou art not fer fro the kyngdom of God.
35 Yesu alipokuwa akifundisha Hekaluni, akauliza, “Imekuwaje walimu wa sheria wanasema kwamba Kristoni Mwana wa Daudi?
And thanne no man durste axe hym no more ony thing. And Jhesus answeride and seide, techynge in the temple, Hou seien scribis, that Crist is the sone of Dauid?
36 Kwa maana Daudi mwenyewe, akinena kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu, alisema: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
For Dauid hym silf seide in the Hooli Goost, the Lord seide to my lord, Sitte on my riythalf, til Y putte thin enemyes the stool of thi feet.
37 Kwa hiyo Daudi mwenyewe anamwita ‘Bwana.’ Awezaje basi yeye kuwa mwanawe?” Ule umati wote wa watu wakamsikiliza kwa furaha.
Thanne Dauid hym silf clepith him lord, hou thanne is he his sone? And myche puple gladli herde hym.
38 Alipokuwa akifundisha, Yesu alisema, “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni.
And he seide to hem in his techyng, Be ye war of scribis, that wolen wandre in stolis,
39 Pia wao hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kupewa nafasi za heshima katika karamu.
and be salutid in chepyng, and sitte in synagogis in the firste chaieris, and the firste sittyng placis in soperis;
40 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
whiche deuouren the housis of widewis vndur colour of long preier; thei schulen take the longer doom.
41 Kisha Yesu akaketi mkabala na sehemu ambapo sadaka zilikuwa zinawekwa na kuangalia umati wa watu wakiweka fedha zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu. Matajiri wengi wakaweka kiasi kikubwa cha fedha.
And Jhesus sittynge ayens the tresorie, bihelde hou the puple castide monei in to the tresorie; and many riche men castiden many thingis.
42 Lakini mjane mmoja maskini akaja na kuweka sarafu mbili ndogo za shaba zenye thamani ya senti mbili.
But whanne a pore widewe was comun, sche keste two mynutis, that is, a ferthing.
43 Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka katika sanduku la hazina zaidi ya watu wengine wote.
And he clepide togidere hise disciplis, and seide to hem, Treuli Y seie to you, that this pore widewe keste more thanne alle, that kesten in to the tresorie.
44 Wengine wote wametoa kutokana na ziada ya mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake, akaweka kila kitu alichokuwa nacho, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
For alle kesten of that thing that thei hadden plente of; but this of her pouert keste alle thingis that sche hadde, al hir lyuelode.

< Marko 12 >