< Marko 12 >

1 Yesu akaanza kusema nao kwa mifano, akawaambia: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akachimba shimo ndani yake kwa ajili ya shinikizo la kusindika divai, na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha shamba hilo la mizabibu kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwenda nchi nyingine.
And He began to them in parables (to speak: *N(k)O*) A vineyard a man planted and he placed around [it] a fence and dug a wine vat and built a tower and rented out it to farmers and traveled abroad
2 Wakati wa mavuno ulipofika, mwenye shamba akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili kuchukua sehemu yake ya mavuno ya shamba la mizabibu kutoka kwa hao wapangaji.
And he sent to the farmers at the due time a servant that from the farmers he may receive from (the fruits *N(k)O*) of the vineyard.
3 Lakini wale wakulima walimkamata yule mtumishi, wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
(*k*) (But *N(k)O*) having taken him they beat [him] and they sent [him] away empty-handed.
4 Kisha yule mwenye shamba akamtuma mtumishi mwingine kwao; nao wale wakulima wakampiga kichwani na kumfanyia mambo ya aibu.
And again he sent to them another servant; and him and him (stoning *K*) they struck on the head and (sent *K*) (dishonored. *N(k)O*)
5 Kisha akamtuma mtumishi mwingine, naye huyo wakamuua. Akawatuma wengine wengi; baadhi yao wakawapiga, na wengine wakawaua.
And (again *k*) another He sent; and him and him they killed, also many others, (some *N(k)O*) indeed beating, (some *N(k)O*) however killing.
6 “Mwenye shamba alikuwa bado na mmoja wa kumtuma, mwanawe aliyempenda. Hatimaye akamtuma akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
Yet (therefore *K*) one (did have *N(k)O*) son beloved (of him; *k*) he sent (and *k*) him last to them saying that They will have respect for the son of mine.
7 “Lakini wale wapangaji wakasemezana pamoja, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, nao urithi utakuwa wetu.’
Those however farmers to themselves they said that This is the heir; come let us kill him, and ours will be the inheritance.
8 Hivyo wakamchukua na kumuua, wakamtupa nje ya lile shamba la mizabibu.
And having taken they killed him and cast forth him outside the vineyard.
9 “Sasa basi yule mwenye shamba atafanya nini? Atakuja na kuwaua hao wapangaji, kisha atawapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.
What therefore will do the master of the vineyard? he will come and he will destroy the farmers and will give the vineyard to others.
10 Je, hamjasoma Andiko hili: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni;
Not even Scripture this have you read: [The] stone which rejected those building, this has become the chief of [the] corner;
11 Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni ajabu machoni petu’?”
from [the] Lord was this, and it is marvelous in [the] eyes of us.’?
12 Walipotambua kuwa amesema mfano huo kwa ajili yao, wakataka kumkamata, lakini wakaogopa ule umati wa watu. Wakamwacha, wakaondoka, wakaenda zao.
And they were seeking Him to lay hold of and they feared the crowd; they knew for that against them the parable He had spoken. And having left Him they went away.
13 Baadaye wakawatuma baadhi ya Mafarisayo na Maherode ili kwenda kumtega Yesu katika yale anayosema.
And they send to Him some of the Pharisees and of the Herodians that Him they may catch in discourse.
14 Wakamjia, wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu. Wewe huyumbishwi na wanadamu, kwa kuwa huna upendeleo. Lakini wewe huifundisha njia ya Mungu katika kweli. Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?
(*k*) (And *N(k)O*) having come they say to Him; Teacher, we know that true You are and not there is care to You about no [one]; not for You look on [the] appearance of men but on the basis of [the] truth the way of God teach. Is it lawful to give tribute to Caesar or not?
15 Je, tulipe kodi au tusilipe?” Lakini Yesu alijua unafiki wao. Akawauliza “Mbona mnajaribu kunitega? Nileteeni hiyo dinariniione.”
shall we pay or not shall we pay? And knowing of them the hypocrisy He said to them; Why Me do you test? do bring Me a denarius that I may see [it].
16 Wakamletea hiyo sarafu. Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?” Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.”
And they brought [it]. And He says to them; Of whom [is] likeness this and the inscription? And they said to Him; Caesar’s.
17 Ndipo Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.” Nao wakamstaajabia sana.
(and answering *k*) (And *no*) Jesus said to them; the [things] of Caesar do give back to Caesar and the [things] of God to God. And (they were amazed *N(k)(o)*) at Him.
18 Kisha Masadukayo, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu,
And come Sadducees to Him who say a resurrection not being and (they were questioning *N(k)O*) Him saying;
19 wakasema, “Mwalimu, Mose alituandikia kuwa kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
Teacher, Moses wrote for us that if of anyone a brother shall die and he may leave behind a wife and not may leave (child *N(K)O*) that shall take the brother of him the wife (of him *k*) and may raise up seed for the brother of him.
20 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa pasipo kuwa na mtoto yeyote.
Seven brothers there were; and the first took a wife and dying not he left seed.
21 Wa pili akamwoa yule mjane, lakini naye akafa bila kuacha mtoto yeyote. Ikawa vivyo hivyo kwa yule wa tatu.
And the second took her and died (and *k*) (not *N(k)O*) (he himself *k*) (having left *N(k)O*) seed and the third likewise;
22 Hakuna hata mmojawapo wa hao ndugu wote saba aliyeacha mtoto. Hatimaye yule mwanamke naye akafa.
And (took her *k*) the seven (and *k*) not left offspring. (Last *N(k)O*) of all also the woman died.
23 Kwa hiyo wakati wa ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
In the (therefore *K*) resurrection when they may rise of which of them will she be wife? For the seven had her as wife.
24 Yesu akawajibu, “Je, hampotoki kwa sababu hamfahamu Maandiko wala uweza wa Mungu?
(and *k*) (Was saying *N(k)O*) to them Jesus (said: *k*) Surely because of this do you err not knowing the Scriptures nor [knowing] the power of God?
25 Wafu watakapofufuka, hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
When for out from [the] dead they may rise, neither do they marry nor are given in marriage but are like angels (*ko*) in the heavens.
26 Basi kuhusu wafu kufufuliwa, je hamjasoma katika Kitabu cha Mose jinsi Mungu alivyosema na Mose kutoka kile kichaka akisema, ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, na Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo?’
Concerning now the dead that they rise, surely you have read in the book of Moses on (the *N(k)O*) bush (how *N(k)O*) spoke to him God saying; I myself [am] the God of Abraham and the God of Isaac and the God of Jacob’?
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai. Kwa hiyo mmekosea kabisa.”
Not He is (the *k*) God of [the] dead but (God *k*) of [the] living; (you yourselves therefore *KO*) Greatly you err.
28 Mwalimu mmoja wa sheria akaja, akawasikia wakijadiliana. Akiona kwamba Yesu amewajibu vyema, naye akamuuliza, “Katika amri zote, ni ipi iliyo kuu?”
And having come up one of the scribes, having heard when they are reasoning together, (seeing *N(k)O*) that well He answered them he questioned Him; Which is commandment [the] first (of all *N(k)O*)
29 Yesu akajibu, “Amri iliyo kuu ndiyo hii: ‘Sikia ee Israeli. Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
(now *k*) Answered Jesus (to him *ko*) The first (is *no*) (of all *K(o)*) (commandments: *K*) do listen O Israel: [The] Lord the God of us [the] Lord One is;
30 Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.’
and you will love [the] Lord the God of you with all the heart of you and with all the soul of you and with all the mind of you and with all the strength of you.’ (this first commandment. *KO*)
31 Ya pili ndiyo hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.”
(and *ko*) [The] second (like *KO*) this: You will love the neighbour of you as yourself.’ Greater than these another commandment not there is.
32 Yule mwalimu wa sheria akamwambia Yesu, “Mwalimu, umejibu vyema kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye.
And said to Him the scribe; Right, Teacher, according to truth You have spoken that One He is (God *K*) and not there is another besides Him.
33 Kumpenda Mungu kwa moyo wote na kwa akili zote na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama mtu anavyojipenda mwenyewe ni bora zaidi kuliko kutoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu zote.”
and to love Him with all the heart and with all the understanding (and from all soul *KO*) and with all the strength and to love the neighbour as oneself (more excessive *N(K)O*) is than all the burnt offerings and (*k*) sacrifices.
34 Yesu alipoona kwamba amejibu kwa busara, akamwambia, “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.” Tangu wakati huo, hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
And Jesus having seen him that wisely he answered He said to him; Not far are you from the kingdom of God. And no [one] no longer no longer was daring Him to question.
35 Yesu alipokuwa akifundisha Hekaluni, akauliza, “Imekuwaje walimu wa sheria wanasema kwamba Kristoni Mwana wa Daudi?
And answering Jesus was saying teaching in the temple; How say the scribes that the Christ [the] son of David is?
36 Kwa maana Daudi mwenyewe, akinena kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu, alisema: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
Himself (for *ko*) David said by the Spirit Holy: (Said *NK(o)*) (the *ko*) Lord to the Lord of me; (do sit *NK(o)*) at [the] right hand of Me until when I may place of the enemies of You (under *N(k)O*) of the feet of You.’
37 Kwa hiyo Daudi mwenyewe anamwita ‘Bwana.’ Awezaje basi yeye kuwa mwanawe?” Ule umati wote wa watu wakamsikiliza kwa furaha.
Himself (therefore *K*) David names Him Lord, then how of him is He son? And the great crowd was listening to Him gladly.
38 Alipokuwa akifundisha, Yesu alisema, “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni.
And (to them *k*) in the teaching of Him He was saying; do beware of the scribes who are desiring in robes to walk about and greetings in the marketplaces
39 Pia wao hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kupewa nafasi za heshima katika karamu.
and first seats in the synagogues and first places at the feasts,
40 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
those devouring the houses of the widows and as a pretext at great length praying, These will receive more excessive judgment.
41 Kisha Yesu akaketi mkabala na sehemu ambapo sadaka zilikuwa zinawekwa na kuangalia umati wa watu wakiweka fedha zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu. Matajiri wengi wakaweka kiasi kikubwa cha fedha.
And having sat down (Jesus *k*) (opposite *NK(o)*) the treasury He was watching how the crowd cast money into the treasury. and many rich were casting [in] much;
42 Lakini mjane mmoja maskini akaja na kuweka sarafu mbili ndogo za shaba zenye thamani ya senti mbili.
And having come one widow poor she cast [in] lepta two which is a kodrantes.
43 Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka katika sanduku la hazina zaidi ya watu wengine wote.
And having called to [Him] the disciples of Him (He says *N(k)O*) to them; Amen I say to you that widow this poor more than all (has cast [in] *N(k)O*) of those (casting *N(k)O*) into the treasury;
44 Wengine wote wametoa kutokana na ziada ya mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake, akaweka kila kitu alichokuwa nacho, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
All for out of that which is abounding to them cast [in], she however out of the poverty of her all as much as she had cast [in], all the livelihood of her.

< Marko 12 >