< Marko 12 >
1 Yesu akaanza kusema nao kwa mifano, akawaambia: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka, akachimba shimo ndani yake kwa ajili ya shinikizo la kusindika divai, na akajenga mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha shamba hilo la mizabibu kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwenda nchi nyingine.
मंग येशु दृष्टांत दिसन त्यासनासंगे बोलु लागणा, एक माणुसनी द्राक्षमया बनाडा, त्याना आजुबाजू वडांग करी, द्राक्षरसकरता कुंडी बनाडी, ध्यान देवाले माळा बांधा अनी दुसरा शेतकरीसले बटाईवर सोपीन परदेशले निंघी गया.
2 Wakati wa mavuno ulipofika, mwenye shamba akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili kuchukua sehemu yake ya mavuno ya shamba la mizabibu kutoka kwa hao wapangaji.
मंग द्राक्षना हंगाममा वाटा लेवाले त्यानी आपला दासले त्या शेतकरीसकडे धाडं.
3 Lakini wale wakulima walimkamata yule mtumishi, wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
त्याले त्यासनी धरीन मारं अनी रिकामं धाडी दिधं.
4 Kisha yule mwenye shamba akamtuma mtumishi mwingine kwao; nao wale wakulima wakampiga kichwani na kumfanyia mambo ya aibu.
त्यानी परत दुसरा दासले धाडं; त्यासनी त्यानं डोकं फोडीसन त्याना अपमान करा.
5 Kisha akamtuma mtumishi mwingine, naye huyo wakamuua. Akawatuma wengine wengi; baadhi yao wakawapiga, na wengine wakawaua.
मालकनी आखो एकजणले धाडं, त्यासनी त्याले मारी टाकं; अनी नंतरना बराच जणससंगे तसच करं, म्हणजे त्यामाईन बाकीनासले मारं अनी बाकीनासना जीव लिधा.
6 “Mwenye shamba alikuwa bado na mmoja wa kumtuma, mwanawe aliyempenda. Hatimaye akamtuma akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’
अजुन त्यानाजोडे एकजण राहेल व्हता. तो म्हणजे त्यानाच प्रिय पोऱ्या, आपला पोऱ्याना तरी त्या मान ठेवतीन अस म्हणीन शेवट त्याले त्यानी त्यासनाकडे धाडं.
7 “Lakini wale wapangaji wakasemezana pamoja, ‘Huyu ndiye mrithi. Njooni tumuue, nao urithi utakuwa wetu.’
त्याले येतांना दखीसन त्या एकमेकसले बोलणात, हाऊ तर वारीस शे. चला आपण ह्याले मारी टाकुत म्हणजे मळाना मालक आपणच व्हई जासूत.
8 Hivyo wakamchukua na kumuua, wakamtupa nje ya lile shamba la mizabibu.
मंग त्यासनी त्याले धरीन मारी टाकं अनी द्राक्षमयाना बाहेर फेकी दिधं.
9 “Sasa basi yule mwenye shamba atafanya nini? Atakuja na kuwaua hao wapangaji, kisha atawapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.
मंग द्राक्षमयाना मालक काय करी? तो ईसन त्या शेतकरीसना नाश करी टाकी अनं द्राक्षमया दुसराले दि.
10 Je, hamjasoma Andiko hili: “‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni;
काय तुम्हीन शास्त्रमा हाई वचन वाचं नही का? “ज्या दगडले बांधणारासनी नापसंत करं तोच दगड कोणशीला व्हयना.”
11 Bwana ndiye alitenda jambo hili, nalo ni ajabu machoni petu’?”
हाई प्रभुकडतीन व्हयनं; अनी हाई आमना नजरमा आश्चर्यकारक कृत्य शे!
12 Walipotambua kuwa amesema mfano huo kwa ajili yao, wakataka kumkamata, lakini wakaogopa ule umati wa watu. Wakamwacha, wakaondoka, wakaenda zao.
येशु हाऊ दृष्टांत आपले लाईन बोलना हाई त्यासना ध्यानमा वनं. तवय शास्त्री त्याले धराले दखी राहींतात पण लोकसनी गर्दीनी त्यासले भिती वाटनी त्यामुये त्या त्याले सोडीन निंघी गयात.
13 Baadaye wakawatuma baadhi ya Mafarisayo na Maherode ili kwenda kumtega Yesu katika yale anayosema.
नंतर त्यानाच बोलनामा त्याले फसाडा करता त्यासनी परूशी अनी हेरोदी पक्षना पुढारीसले येशुकडे धाडं.
14 Wakamjia, wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu mwadilifu. Wewe huyumbishwi na wanadamu, kwa kuwa huna upendeleo. Lakini wewe huifundisha njia ya Mungu katika kweli. Je, ni halali kulipa kodi kwa Kaisari, au la?
त्या ईसन त्याले बोलणात, गुरजी, आमले माहित शे तुम्हीन खरा शेतस, तुम्हीन मनुष्यसना मत अनी ईच्छासघाई प्रभावित होतस नही, तुम्हीन लोकसनं तोंड दखीन बोलतस नही तर देवना खरा मार्ग शिकाडतस पण आमले सांगा रोमना राजाले कर देवानं हाई आमना नियमप्रमाणे योग्य शे का अयोग्य शे? आम्हीन देवानं का नही देवानं?
15 Je, tulipe kodi au tusilipe?” Lakini Yesu alijua unafiki wao. Akawauliza “Mbona mnajaribu kunitega? Nileteeni hiyo dinariniione.”
त्यानी त्यासनं ढोंग वळखीन त्यासले सांगं, “का बर मनी परिक्षा दखी राहीनात? माले एक नाणं दखाडा.”
16 Wakamletea hiyo sarafu. Naye akawauliza, “Sura hii ni ya nani? Na maandishi haya ni ya nani?” Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.”
त्यासनी ते दखाडं तवय त्यानी त्यासले सांगं, “यावर कोण चित्र अनी लेख शे?” त्या बोलणात, रोमना राजानं.
17 Ndipo Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.” Nao wakamstaajabia sana.
येशुनी त्यासले सांगं, तर जे राजानं शे ते राजाले द्या अनी जे देवनं शे ते देवले द्या. येशुनं उत्तर ऐकीन त्या आश्चर्यचकीत व्हयनात.
18 Kisha Masadukayo, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu,
मंग पुनरूत्थान व्हस नही असा म्हनणारा सदुकी लोके येशुकडे वनात अनी त्याले ईचारं,
19 wakasema, “Mwalimu, Mose alituandikia kuwa kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
“गुरजी, मोशेनी आमनाकरता अस लिखी ठेल शे की, ‘एखादाना भाऊ मरना’ अनी त्यानी बायको बिगर लेकरंसनी शे, तर त्याना भाऊनी तिनासंगे लगीन करीसन भाऊना वंश चालावाना.”
20 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa mke, naye akafa pasipo kuwa na mtoto yeyote.
एक ठिकाणे सात भाऊ व्हतात; त्यासनामा मोठानी लगीन करं अनी तो लेकरं नही व्हताच मरी गया.
21 Wa pili akamwoa yule mjane, lakini naye akafa bila kuacha mtoto yeyote. Ikawa vivyo hivyo kwa yule wa tatu.
मंग दुसरा भाऊनी तिनासंगे लगीन करं अनी तो बी संतती नही व्हताच मरी गया. तिसरा बी तसाच मरना
22 Hakuna hata mmojawapo wa hao ndugu wote saba aliyeacha mtoto. Hatimaye yule mwanamke naye akafa.
तसाच सातही जण संतती नही व्हताच मरी गयात. सर्वासना शेवट ती बाई बी मरी गई.
23 Kwa hiyo wakati wa ufufuo, yeye atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
तर पुनरूत्थान व्हई तवय ती कोणी बायको व्हई? कारण ती साती जणसनी बायको व्हयेल व्हती.
24 Yesu akawajibu, “Je, hampotoki kwa sababu hamfahamu Maandiko wala uweza wa Mungu?
येशुनी त्यासले उत्तर दिधं, “तुम्हीन शास्त्र अनी देवनं सामर्थ्यले वळखेल नही म्हणीन तुम्हीन चुकतस ना?
25 Wafu watakapofufuka, hawataoa wala kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
कारण त्या मरणमातीन ऊठानंतर लगीन करतस नही अनी करी बी देतस नही, तर त्या स्वर्गमधला देवदूतसना मायक राहतस.”
26 Basi kuhusu wafu kufufuliwa, je hamjasoma katika Kitabu cha Mose jinsi Mungu alivyosema na Mose kutoka kile kichaka akisema, ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, na Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo?’
मरेल ऊठाडाई जातस यानाबद्दल मोशेना पुस्तकमाधला जळता झुडूपना प्रकरणमा देवनी त्याले सांगं, “मी अब्राहामना देव, इसहाकना देव अनी याकोबना देव शे,” हाई तुमना वाचामा वनं नही का?
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai. Kwa hiyo mmekosea kabisa.”
तो मरेलसना देव नही तर जिवतसना देव शे; तुम्हीन पुराच चुकेल शेतस.
28 Mwalimu mmoja wa sheria akaja, akawasikia wakijadiliana. Akiona kwamba Yesu amewajibu vyema, naye akamuuliza, “Katika amri zote, ni ipi iliyo kuu?”
तवय शास्त्रीसमाधला एकजणनी ईसन त्यासना वादविवाद ऐका, अनी येशुनी सदुकीसले कसं सुंदर पध्दतमा उत्तर दिधं हाई दखीन, त्यानी त्याले ईचारं, “सर्वात मोठी आज्ञा कोणती?”
29 Yesu akajibu, “Amri iliyo kuu ndiyo hii: ‘Sikia ee Israeli. Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
येशुनी उत्तर दिधं, “मोठी आज्ञा हाई की, हे इस्त्राएलना लोकसवन! ऐका, प्रभु आपला देव एकमेव देव शे.
30 Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.’
तु आपला देव परमेश्वर यानावर पुर्ण मनतीन, पुर्ण जिवतीन, पुर्ण बुध्दीतीन अनं पुर्ण शक्तितीन प्रिती कर.”
31 Ya pili ndiyo hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.”
दुसरी हाई की “जशी स्वतःवर तशी आपला शेजारीसवर प्रिती कर.” या दोन्ही आज्ञापेक्षा दुसरी कोणतीच मोठी आज्ञा नही.
32 Yule mwalimu wa sheria akamwambia Yesu, “Mwalimu, umejibu vyema kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye.
तो त्याले बोलना, “गुरजी, तुम्हीन खरोखर बोलणात की, ‘तो एकच देव शे अनी त्यानाशिवाय दुसरा कोणीच नही.’
33 Kumpenda Mungu kwa moyo wote na kwa akili zote na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama mtu anavyojipenda mwenyewe ni bora zaidi kuliko kutoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu zote.”
अनी ‘पुर्ण मनतीन, पुर्ण बुध्दितीन अनी पुर्ण शक्तितीन त्यानावर प्रिती करानी अनी जशी स्वतःवर तशी शेजारीसवर प्रिती करानी’ हाई सर्व ‘होम अनं यज्ञ’ यानापेक्षा मोठं शे.”
34 Yesu alipoona kwamba amejibu kwa busara, akamwambia, “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.” Tangu wakati huo, hakuna mtu yeyote aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
त्यानी समजदारीमा उत्तर दिधं हाई दखीसन येशुनी त्याले सांगं, “तु देवना राज्यपाईन दुर नही.” त्यानानंतर त्याले आखो काही ईचारानी कोणीच हिम्मत व्हयनी नही.
35 Yesu alipokuwa akifundisha Hekaluni, akauliza, “Imekuwaje walimu wa sheria wanasema kwamba Kristoni Mwana wa Daudi?
नंतर येशुनी मंदिरमा शिक्षण देतांना सांगं, “ख्रिस्त दावीदना वंशज शे हाई शास्त्री कसं काय म्हणतस?”
36 Kwa maana Daudi mwenyewe, akinena kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu, alisema: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
“कारण दावीद स्वतः पवित्र आत्माना प्रेरणातीन म्हणस; प्रभु परमेश्वरनी मना प्रभुले सांगं; तु मना उजवीकडे बैस, जोपावत मी तुना शत्रुसले तुना पायसनं आसन करस नही.”
37 Kwa hiyo Daudi mwenyewe anamwita ‘Bwana.’ Awezaje basi yeye kuwa mwanawe?” Ule umati wote wa watu wakamsikiliza kwa furaha.
दावीद स्वतः त्याले प्रभु म्हणस, मंग ख्रिस्त त्याना वंशज शे हाई कसं काय? हाई येशुनं बोलणं लोकसमुदाय आनंदमा ऐकी राहिंता.
38 Alipokuwa akifundisha, Yesu alisema, “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni.
येशु लोकसले शिकाडतांना बोलणा, “शास्त्रीसपाईन जपी ऱ्हा, त्यासले लांब झगा घालीन फिराले, बजारमा लोकसकडतीन नमस्कार करी लेवाले,
39 Pia wao hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kupewa nafasi za heshima katika karamu.
अनी सभास्थानमा मुख्य आसन अनी मेजवानीमा चांगली जागा ह्या त्यासले आवडतस.
40 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
ह्याच त्या शेतस ज्या विधवासनी संपत्ती फसाडीन खाई टाकतस अनी दिखावाकरता लांबलांब प्रार्थना करतस. सर्वात जास्त त्यासले शिक्षा व्हई!”
41 Kisha Yesu akaketi mkabala na sehemu ambapo sadaka zilikuwa zinawekwa na kuangalia umati wa watu wakiweka fedha zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu. Matajiri wengi wakaweka kiasi kikubwa cha fedha.
येशु मंदिरमधला दानपेटी समोर बशीन लोक दानपेटीमा पैसा कशा टाकतस हाई तो दखी राहिंता. बराच श्रीमंत लोकसनी बराच पैसा टाकात;
42 Lakini mjane mmoja maskini akaja na kuweka sarafu mbili ndogo za shaba zenye thamani ya senti mbili.
अनी एक गरीब विधवानी ईसन दोन तांबाना नाणा टाकात त्यानी किंमत काहीच नव्हती.
43 Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka katika sanduku la hazina zaidi ya watu wengine wote.
तवय येशुनी शिष्यसले जोडे बलाईन सांगं, “मी तुमले सत्य सांगस की, ज्या दानपेटीमा टाकी राहिनात त्या सर्वासपेक्षा हाई गरीब विधवानी जास्त टाकेल शे.
44 Wengine wote wametoa kutokana na ziada ya mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake, akaweka kila kitu alichokuwa nacho, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
कारण त्या सर्वासनी त्यासना समृध्दीमातीन टाकात; पण हिनी तिना गरिबीमातीन जितलं तिनं व्हतं तितलं म्हणजे सर्वी कमाई टाकी दिधी.”