< Marko 11 >
1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage na Bethania katika Mlima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake,
When they were getting near Jerusalem and had arrived at Bethphage and Bethany, on the Mount of Olives, Jesus sent two of his disciples on in front, with these instructions.
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na hapo mtakapoingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
"Go," He said, "to the village facing you, and immediately on entering it you will find an ass's foal tied up which no one has ever yet ridden: untie him and bring him here.
3 Kama mtu yeyote akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji, na atamrudisha hapa baada ya muda mfupi.’”
And if any one asks you, 'Why are you doing that?' say, 'The Master needs it, and will send it back here without delay.'"
4 Wakaenda, wakamkuta mwana-punda amefungwa kando ya barabara, karibu na mlango wa nyumba.
So they went and found a young ass tied up at the front door of a house. They were untying it,
5 Walipokuwa wanamfungua, watu waliokuwa wamesimama karibu wakawauliza, “Mna maana gani mnapomfungua huyo mwana-punda?”
when some of the bystanders called out, "What are you doing, untying the foal?"
6 Wakawajibu kama vile Yesu alivyokuwa amewaagiza, nao wale watu wakawaruhusu.
But on their giving the answer that Jesus had bidden them give, they let them take it.
7 Kisha wakamleta huyo mwana-punda kwa Yesu na kutandika mavazi yao juu yake, naye akampanda.
So they brought the foal to Jesus, and threw their outer garments over him; and Jesus mounted.
8 Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakatandaza matawi waliyokuwa wamekata mashambani.
Then many spread their outer garments to carpet the road, and others leafy branches which they had cut down in the fields;
9 Kisha wale waliokuwa wametangulia mbele na wale waliokuwa wakifuata nyuma wakapaza sauti, wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!”
while those who led the way and those who followed kept shouting "God save Him!" Blessed be He who comes in the Lord's name.
10 “Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!” “Hosana kwake yeye aliye juu!”
Blessings on the coming Kingdom of our forefather David! God in the highest Heavens save Him!"
11 Yesu akaingia Yerusalemu na kwenda Hekaluni. Akaangalia kila kitu kilichokuwamo, lakini kwa kuwa ilishakuwa jioni, akaenda zake Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
So He came into Jerusalem and into the Temple; and after looking round upon everything there, the hour being now late He went out to Bethany with the Twelve.
12 Kesho yake walipokuwa wakitoka Bethania, Yesu alikuwa na njaa.
The next day, after they had left Bethany, He was hungry.
13 Akauona mtini kwa mbali, naye akaenda ili aone kama ulikuwa na matunda. Alipoufikia, akakuta una majani tu, kwa kuwa hayakuwa majira ya tini.
But in the distance He saw a fig-tree in full leaf, and went to see whether perhaps He could find some figs on it. When however He came to it, He found nothing but leaves (for it was not fig time);
14 Akauambia ule mti, “Tangu leo mtu yeyote asile kamwe matunda kutoka kwako.” Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo. (aiōn )
and He said to the tree, "Let no one ever again eat fruit from thee!" And His disciples heard this. (aiōn )
15 Walipofika Yerusalemu, Yesu akaingia katika eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakinunua na kuuza humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,
They reached Jerusalem, and entering the Temple He began to drive out the buyers and sellers, and upset the money-changers' tables and the stools of the pigeon-dealers,
16 wala hakumruhusu mtu yeyote kuchukua bidhaa kupitia ukumbi wa Hekalu.
and would not allow any one to carry anything through the Temple.
17 Naye alipokuwa akiwafundisha, akasema, “Je, haikuandikwa kuwa: “‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote’? Lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
And He remonstrated with them. "Is it not written," He said, "'My House shall be called The House of Prayer for all the nations?' But you have made it what it now is--a robbers' cave."
18 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria wakapata habari hizi, nao wakaanza kutafuta njia ya kumuua, kwa kuwa walikuwa wakimwogopa, kwa sababu umati wote ulikuwa unashangazwa na mafundisho yake.
This the High Priests and Scribes heard, and they began to devise means to destroy Him. For they were afraid of Him, because of the deep impression produced on all the people by His teaching.
19 Ilipofika jioni, Yesu na wanafunzi wake wakatoka nje ya mji.
When evening came on, Jesus and His disciples used to leave the city.
20 Asubuhi yake walipokuwa wakipita, wakauona ule mtini umenyauka kutoka juu hadi kwenye mizizi yake.
In the early morning, as they passed by, they saw the fig-tree withered to the roots;
21 Petro akakumbuka na kumwambia Yesu, “Rabi, tazama! Ule mtini ulioulaani umenyauka!”
and Peter, recollecting, said to Him, "Look, Rabbi, the fig-tree which you cursed is withered up."
22 Yesu akawajibu, “Mwaminini Mungu.
Jesus said to them, "Have faith in God.
23 Amin, nawaambia, mtu yeyote atakayeuambia mlima huu, ‘Ngʼoka ukatupwe baharini,’ wala asione shaka moyoni mwake, bali aamini kwamba hayo asemayo yametukia, atatimiziwa.
In solemn truth I tell you that if any one shall say to this mountain, 'Remove, and hurl thyself into the sea,' and has no doubt about it in his heart, but stedfastly believes that what he says will happen, it shall be granted him.
24 Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote mtakayoyaomba mkisali, aminini ya kwamba mmeyapokea, nayo yatakuwa yenu.
That is why I tell you, as to whatever you pray and make request for, if you believe that you have received it it shall be yours.
25 Nanyi kila msimamapo kusali, sameheni mkiwa na neno na mtu, ili naye Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu. [
But whenever you stand praying, if you have a grievance against any one, forgive it, so that your Father in Heaven may also forgive you your offences."
26 Lakini kama ninyi msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]”
27 Wakafika tena Yerusalemu, na Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wa watu wakamjia.
They came again to Jerusalem; and as He was walking in the Temple, the High Priests, Scribes and Elders came to Him
28 Wakamuuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka ya kufanya hayo?”
and asked, "By what authority are you doing these things? and who gave you authority to do them?"
29 Yesu akawajibu, “Nitawauliza swali moja. Nijibuni, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
"And I will put a question to you," replied Jesus; "answer me, and then I will tell you by what authority I do these things.
30 Niambieni, je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
John's Baptism--was it of Heavenly or of human origin? Answer me."
31 Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
So they debated the matter with one another. "Suppose we say, 'Heavenly,'" they argued, "he will ask, 'Why then did you not believe him?'
32 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’…” (Waliwaogopa watu, kwa sababu kila mtu aliamini kwamba Yohana alikuwa nabii wa kweli.)
Or should we say, 'human?'" They were afraid of the people; for all agreed in holding John to have been really a Prophet.
33 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Hatujui.” Naye Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
So they answered Jesus, "We do not know." "Nor do I tell you," said Jesus, "by what authority I do these things."