< Marko 11 >
1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage na Bethania katika Mlima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake,
And when they came nye to Hierusalem vnto Bethphage and Bethanie besydes mout olivete he sent forth two of his hisciples
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na hapo mtakapoingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
and sayde vnto the: Goo youre wayes into the toune that is over agaynst you. And assone as ye be entred into it ye shall fynde a coolte bounde wheron never man sate: loose him and bringe him.
3 Kama mtu yeyote akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji, na atamrudisha hapa baada ya muda mfupi.’”
And if eny man saye vnto you: why do ye soo? Saye that the Lorde hath neade of him: and streight waye he will sende him hidder.
4 Wakaenda, wakamkuta mwana-punda amefungwa kando ya barabara, karibu na mlango wa nyumba.
And they wet their waye and foud a coolte tyed by the dore with out in a place where two wayes met and they losed him.
5 Walipokuwa wanamfungua, watu waliokuwa wamesimama karibu wakawauliza, “Mna maana gani mnapomfungua huyo mwana-punda?”
And divers of the that stode there sayde vnto the: what do ye loosinge ye coolte?
6 Wakawajibu kama vile Yesu alivyokuwa amewaagiza, nao wale watu wakawaruhusu.
And they sayd vnto them eve as Iesus had comaunded the. And they let them goo.
7 Kisha wakamleta huyo mwana-punda kwa Yesu na kutandika mavazi yao juu yake, naye akampanda.
And they brought ye coolte to Iesus and caste their garmetes on him: and he sate vpo him.
8 Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakatandaza matawi waliyokuwa wamekata mashambani.
And many sprede there garmetes in the waye. Other cut doune brauches of the trees and strawed them in ye waye.
9 Kisha wale waliokuwa wametangulia mbele na wale waliokuwa wakifuata nyuma wakapaza sauti, wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!”
And they yt went before and they that folowed cryed sayinge: Hos anna: blessed be he that cometh in ye name of ye Lorde.
10 “Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!” “Hosana kwake yeye aliye juu!”
Blessed be ye kingdome that cometh in ye name of him yt is Lorde of oure father David. Hos anna in ye hyest.
11 Yesu akaingia Yerusalemu na kwenda Hekaluni. Akaangalia kila kitu kilichokuwamo, lakini kwa kuwa ilishakuwa jioni, akaenda zake Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
And ye Lorde entred in to Ierusalem and into the teple. And when he had loked roudabout vpon all thinges and now ye eve tyde was come he went out vnto Bethany with ye twelve.
12 Kesho yake walipokuwa wakitoka Bethania, Yesu alikuwa na njaa.
And on the morowe when they were come out fro Bethany he hungred
13 Akauona mtini kwa mbali, naye akaenda ili aone kama ulikuwa na matunda. Alipoufikia, akakuta una majani tu, kwa kuwa hayakuwa majira ya tini.
and spyed a fygge tree a farre of havinge leves and wet to se whether he myght finde eny thinge ther on. But when he came therto he foude no thinge but leves: for the tyme of fygges was not yet.
14 Akauambia ule mti, “Tangu leo mtu yeyote asile kamwe matunda kutoka kwako.” Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo. (aiōn )
And Iesus answered and sayde to it: never man eate frute of the here after whill ye worlde stondith. And his disciples hearde it. (aiōn )
15 Walipofika Yerusalemu, Yesu akaingia katika eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakinunua na kuuza humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,
And they came to Ierusalem. And Iesus wet into the teple and begane to cast out ye sellers and byers in the teple and overthrewe the tables of the money chaungers and the stoles of them that solde doves:
16 wala hakumruhusu mtu yeyote kuchukua bidhaa kupitia ukumbi wa Hekalu.
and wolde not suffre that eny man caried a vessell thorow the temple.
17 Naye alipokuwa akiwafundisha, akasema, “Je, haikuandikwa kuwa: “‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote’? Lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
And he taught sayinge vnto them is it not written: my housse shalbe called the housse of prayer vnto all nacions? But ye have made it a deen of theves.
18 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria wakapata habari hizi, nao wakaanza kutafuta njia ya kumuua, kwa kuwa walikuwa wakimwogopa, kwa sababu umati wote ulikuwa unashangazwa na mafundisho yake.
And the Scribes and hye prestes hearde yt and sought howe to distroye him. For they feared him because all the people marveled at his doctrine.
19 Ilipofika jioni, Yesu na wanafunzi wake wakatoka nje ya mji.
And when eve was come he went out of the cite.
20 Asubuhi yake walipokuwa wakipita, wakauona ule mtini umenyauka kutoka juu hadi kwenye mizizi yake.
And in the mornynge as they passed by they sawe the fygge tree dryed vp by ye rotes.
21 Petro akakumbuka na kumwambia Yesu, “Rabi, tazama! Ule mtini ulioulaani umenyauka!”
And Peter remembred and sayde vnto him: master beholde the fygge tree which thou cursedest is widdred awaye.
22 Yesu akawajibu, “Mwaminini Mungu.
And Iesus answered and sayde vnto them: Have confides in God.
23 Amin, nawaambia, mtu yeyote atakayeuambia mlima huu, ‘Ngʼoka ukatupwe baharini,’ wala asione shaka moyoni mwake, bali aamini kwamba hayo asemayo yametukia, atatimiziwa.
Verely I saye vnto you that whosoever shall saye vnto this mountayne: take awaye thy silfe and cast thy silfe in to the see and shall not waver in his herte but shall beleve yt those thinges which he sayeth shall come to passe what soever he sayeth shalbe done to him.
24 Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote mtakayoyaomba mkisali, aminini ya kwamba mmeyapokea, nayo yatakuwa yenu.
Therfore I saye vnto you what soever ye desyre when ye praye beleve yt ye shall have it and it shalbe done vnto you.
25 Nanyi kila msimamapo kusali, sameheni mkiwa na neno na mtu, ili naye Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu. [
And when ye stod and praye forgeve yf ye have eny thinge agaynste eny man yt youre father also which is in heve maye forgeve you youre trespases.
26 Lakini kama ninyi msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]”
27 Wakafika tena Yerusalemu, na Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wa watu wakamjia.
And they came agayne to Hierusalem. And as he walked in the teple ther came to him ye hye prestes and the Scribes and the elders
28 Wakamuuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka ya kufanya hayo?”
and sayd vnto him: by what auctorite doest thou these thinges? and who gave the this auctorite to do these thinges?
29 Yesu akawajibu, “Nitawauliza swali moja. Nijibuni, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
Iesus answered and sayde vnto them: I will also axe of you a certayne thinge: and answere ye me and I wyll tell you by what auctorite I do these thinges.
30 Niambieni, je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
The baptyme of Iohn was it from heven or of men? Answer me.
31 Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
And they thought in them selves sayinge: yf we shall saye from heven: he will saye why then dyd ye not beleve him?
32 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’…” (Waliwaogopa watu, kwa sababu kila mtu aliamini kwamba Yohana alikuwa nabii wa kweli.)
but if we shall saye of me: then feare we ye people. For all men counted Iohn that he was a verie Prophete.
33 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Hatujui.” Naye Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
And they answered and sayd vnto Iesu: we cannot tell. And Iesus answered and sayd vnto them: nether wyll I tell you by what auctorite I do these thynges.