< Marko 11 >
1 Walipokaribia Yerusalemu, wakafika Bethfage na Bethania katika Mlima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili wa wanafunzi wake,
And when they come near to Jerusalem, to Bethphage, and Bethany, to the Mount of Olives, He sends forth two of His disciples,
2 akawaambia, “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na hapo mtakapoingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
and says to them, “Go away into the village that is in front of you, and immediately, entering into it, you will find a colt tied, on which no one of men has sat, having loosed it, bring [it]:
3 Kama mtu yeyote akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji, na atamrudisha hapa baada ya muda mfupi.’”
and if anyone may say to you, Why do you do this? Say that the LORD has need of it, and immediately He will send it here.”
4 Wakaenda, wakamkuta mwana-punda amefungwa kando ya barabara, karibu na mlango wa nyumba.
And they went away, and found the colt tied at the door outside, by the two ways, and they loose it,
5 Walipokuwa wanamfungua, watu waliokuwa wamesimama karibu wakawauliza, “Mna maana gani mnapomfungua huyo mwana-punda?”
and certain of those standing there said to them, “What do you—loosing the colt?”
6 Wakawajibu kama vile Yesu alivyokuwa amewaagiza, nao wale watu wakawaruhusu.
And they said to them as Jesus commanded, and they permitted them.
7 Kisha wakamleta huyo mwana-punda kwa Yesu na kutandika mavazi yao juu yake, naye akampanda.
And they brought the colt to Jesus, and cast their garments on it, and He sat on it,
8 Watu wengi wakatandaza mavazi yao barabarani, na wengine wakatandaza matawi waliyokuwa wamekata mashambani.
and many spread their garments in the way, and others were cutting down branches from the trees, and were strewing in the way.
9 Kisha wale waliokuwa wametangulia mbele na wale waliokuwa wakifuata nyuma wakapaza sauti, wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!”
And those going before and those following were crying out, saying, “Hosanna! Blessed [is] He who is coming in the Name of the LORD;
10 “Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!” “Hosana kwake yeye aliye juu!”
blessed is the coming kingdom, in the Name of the LORD, of our father David; Hosanna in the highest!”
11 Yesu akaingia Yerusalemu na kwenda Hekaluni. Akaangalia kila kitu kilichokuwamo, lakini kwa kuwa ilishakuwa jioni, akaenda zake Bethania pamoja na wale kumi na wawili.
And Jesus entered into Jerusalem, and into the temple, and having looked around on all things, it being now evening, He went forth to Bethany with the Twelve.
12 Kesho yake walipokuwa wakitoka Bethania, Yesu alikuwa na njaa.
And on the next day, they having come forth from Bethany, He hungered,
13 Akauona mtini kwa mbali, naye akaenda ili aone kama ulikuwa na matunda. Alipoufikia, akakuta una majani tu, kwa kuwa hayakuwa majira ya tini.
and having seen a fig tree far off having leaves, He came, if perhaps He will find anything in it, and having come to it, He found nothing except leaves, for it was not a time of figs,
14 Akauambia ule mti, “Tangu leo mtu yeyote asile kamwe matunda kutoka kwako.” Wanafunzi wake walimsikia akisema hayo. (aiōn )
and Jesus answering said to it, “No longer from you—throughout the age—may any eat fruit”; and His disciples were hearing. (aiōn )
15 Walipofika Yerusalemu, Yesu akaingia katika eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakinunua na kuuza humo ndani. Akazipindua meza za wale waliokuwa wakibadilisha fedha, na pia viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa,
And they come to Jerusalem, and Jesus having gone into the temple, began to cast forth those selling and buying in the temple, and He overthrew the tables of the money-changers and the seats of those selling the doves,
16 wala hakumruhusu mtu yeyote kuchukua bidhaa kupitia ukumbi wa Hekalu.
and He did not permit that any might carry a vessel through the temple,
17 Naye alipokuwa akiwafundisha, akasema, “Je, haikuandikwa kuwa: “‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote’? Lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
and He was teaching, saying to them, “Has it not been written: My house will be called a house of prayer for all the nations? And you made it a den of robbers!”
18 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria wakapata habari hizi, nao wakaanza kutafuta njia ya kumuua, kwa kuwa walikuwa wakimwogopa, kwa sababu umati wote ulikuwa unashangazwa na mafundisho yake.
And the scribes and the chief priests heard, and they were seeking how they will destroy Him, for they were afraid of Him, because all the multitude was astonished at His teaching;
19 Ilipofika jioni, Yesu na wanafunzi wake wakatoka nje ya mji.
and when evening came, He was going forth outside the city.
20 Asubuhi yake walipokuwa wakipita, wakauona ule mtini umenyauka kutoka juu hadi kwenye mizizi yake.
And in the morning, passing by, they saw the fig tree having been dried up from the roots,
21 Petro akakumbuka na kumwambia Yesu, “Rabi, tazama! Ule mtini ulioulaani umenyauka!”
and Peter having remembered says to Him, “Rabbi, behold, the fig tree that You cursed is dried up.”
22 Yesu akawajibu, “Mwaminini Mungu.
And Jesus answering says to them, “Have faith from God;
23 Amin, nawaambia, mtu yeyote atakayeuambia mlima huu, ‘Ngʼoka ukatupwe baharini,’ wala asione shaka moyoni mwake, bali aamini kwamba hayo asemayo yametukia, atatimiziwa.
for truly I say to you that whoever may say to this mountain, Be taken up, and be cast into the sea, and may not doubt in his heart, but may believe that the things that he says come to pass, it will be to him whatever he may say.
24 Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote mtakayoyaomba mkisali, aminini ya kwamba mmeyapokea, nayo yatakuwa yenu.
Because of this I say to you, all whatever—praying—you ask, believe that you receive, and it will be to you.
25 Nanyi kila msimamapo kusali, sameheni mkiwa na neno na mtu, ili naye Baba yenu aliye mbinguni awasamehe ninyi makosa yenu. [
And whenever you may stand praying, forgive, if you have anything against anyone, that your Father who is in the heavens may also forgive you your trespasses;
26 Lakini kama ninyi msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]”
[[and, if you do not forgive, neither will your Father who is in the heavens forgive your trespasses.”]]
27 Wakafika tena Yerusalemu, na Yesu alipokuwa akitembea Hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wa watu wakamjia.
And they come again to Jerusalem, and in the temple, as He is walking, there come to Him the chief priests, and the scribes, and the elders,
28 Wakamuuliza, “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Na ni nani aliyekupa mamlaka ya kufanya hayo?”
and they say to Him, “By what authority do You do these things? And who gave You this authority that You may do these things?”
29 Yesu akawajibu, “Nitawauliza swali moja. Nijibuni, nami nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.
And Jesus answering said to them, “I will question you—I also—one word; and answer Me, and I will tell you by what authority I do these things;
30 Niambieni, je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
the immersion of John—was it from Heaven or from men? Answer Me.”
31 Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
And they were reasoning with themselves, saying, “If we may say, From Heaven, He will say, Why then did you not believe him?
32 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’…” (Waliwaogopa watu, kwa sababu kila mtu aliamini kwamba Yohana alikuwa nabii wa kweli.)
But if we may say, From men…” They were fearing the people, for all were holding that John was indeed a prophet;
33 Kwa hiyo wakamjibu Yesu, “Hatujui.” Naye Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
and answering they say to Jesus, “We have not known”; and Jesus answering says to them, “Neither do I tell you by what authority I do these things.”