< Marko 10 >

1 Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
Jeesus lahkus sealt ja tuli Juudamaa aladele sealpool Jordanit. Jälle kogunes hulk rahvast tema juurde ja ta õpetas neid, nagu tal oli kombeks.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
Jeesuse juurde tulid mõned variserid, et teda proovile panna, ja küsisid: „Kas mehel on luba oma naisest lahutada?“
3 Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
Jeesus küsis neilt: „Kuidas Mooses teid käskis?“
4 Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
Nad vastasid: „Mooses lubas kirjutada lahutustunnistuse ja naise minema saata.“
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
Jeesus ütles neile: „Teie kõva südame pärast kirjutas ta teile selle käsu.
6 Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
Aga loomise algul lõi Jumal nad meheks ja naiseks.
7 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
Seepärast jätab mees maha oma isa ja ema ning hoiab oma naise poole
8 Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
ja need kaks saavad üheks. Siis nad ei ole enam kaks, vaid üks liha.
9 Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
Mis nüüd Jumal on ühte pannud, seda ärgu inimene lahutagu!“
10 Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
Kodus küsisid jüngrid uuesti temalt selle kohta
11 Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
ja Jeesus ütles neile: „Kes lahutab oma naisest ja abiellub teisega, rikub temaga abielu.
12 Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
Ja kui naine on maha jätnud oma mehe ja abiellub teisega, rikub ta abielu.“
13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
Jeesuse juurde toodi väikesi lapsi, et ta neid puudutaks. Jüngrid aga tõrelesid toojatega,
14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
kuid Jeesus sai seda nähes pahaseks ja ta ütles neile: „Laske lapsed minu juurde tulla, ärge keelake neid, sest selliste päralt on Jumala riik.
15 Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
Tõesti, ma ütlen teile, kes Jumala riiki vastu ei võta nagu laps, ei pääse sinna sisse.“
16 Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
Ta võttis lapsed sülle ja õnnistas neid, pannes käed nende peale.
17 Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
Kui Jeesus asus teele, jooksis üks mees tema juurde ja langes ta ette põlvili, küsides: „Hea Õpetaja, mida ma pean tegema, et ma päriksin igavese elu?“ (aiōnios g166)
18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
Jeesus vastas talle: „Miks sa nimetad mind heaks? Keegi muu ei ole hea kui üks – Jumal.
19 Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
Käske sa tead: ära tapa, ära riku abielu, ära varasta, ära anna valetunnistust, ära peta, austa oma isa ja ema!“
20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
Mees aga vastas talle: „Õpetaja, seda kõike olen ma pidanud poisieast alates.“
21 Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
Jeesus aga vaatas talle otsa, tundis armastust tema vastu ja ütles: „Üks asi puudub sul. Mine müü ära kõik, mis sul on, ja jaga vaestele, ja sul on siis aare taevas, ning tule, järgne mulle!“
22 Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
Kui noormees neid sõnu kuulis, lahkus ta kurvana, sest tal oli palju vara.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
Jeesus vaatas enda ümber ja ütles oma jüngritele: „Kui raske on rikastel pääseda Jumala riiki!“
24 Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
Aga jüngrid hämmastusid tema sõnade peale; ja Jeesus ütles jälle: „Lapsed, kui raske on minna Jumala riiki!
25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
Hõlpsam on kaamelil minna läbi nõelasilma kui rikkal minna Jumala riiki.“
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
Jüngrid aga jahmusid veelgi enam ja küsisid üksteiselt: „Kes siis võib saada päästetud?“
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
Jeesus ütles neile otsa vaadates: „Inimesel on see võimatu, aga mitte Jumalal. Jumalal on kõik võimalik!“
28 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
Peetrus hakkas rääkima: „Vaata, meie oleme jätnud kõik maha, et järgneda sulle!“
29 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
Jeesus ütles: „Tõesti, ma ütlen teile, ei ole kedagi, kes on maha jätnud maja, vennad või õed, ema, isa või lapsed või põllud minu pärast ja evangeeliumi pärast
30 ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
ega saaks vastu nüüd, praegusel ajal, sajavõrra maju, vendi ja õdesid, emasid ja lapsi ja põlde tagakiusamise kestelgi, ning tuleval ajastul igavest elu. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
Aga paljud esimesed jäävad viimasteks ja viimased saavad esimesteks.“
32 Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
Kui nad olid teel üles Jeruusalemma, kõndis Jeesus nende ees. Jüngrid olid ehmunud, aga kaasaminejaid valdas hirm. Jeesus viis kaksteist jüngrit taas kõrvale ja hakkas neile rääkima, mis teda ees ootab:
33 Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
„Me läheme üles Jeruusalemma ja Inimese Poeg antakse ülempreestrite ja kirjatundjate kätte. Need mõistavad ta surma ja annavad üle uskmatuile.
34 ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
Need mõnitavad teda ja sülitavad ta peale, piitsutavad teda ja tapavad ta ära. Kuid kolme päeva pärast tõuseb ta surnuist üles.“
35 Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
Ja Sebedeuse pojad Jaakobus ja Johannes astusid Jeesuse juurde. „Õpetaja, “ütlesid nad talle, „me tahame, et sa meile teeksid, mida me iganes küsime!“
36 Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
„Mida te tahate, et ma teile teeksin?“küsis Jeesus.
37 Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
Nad vastasid: „Luba meile, et me istuksime sinu auhiilguses üks sinu paremal ja teine sinu vasakul käel!“
38 Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
Kuid Jeesus ütles neile: „Teie ei tea, mida te palute. Kas te võite juua karikast, mida mina joon, või saada ristitud selle ristimisega, millega mind ristitakse?“
39 Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
„Võime küll!“vastasid nad. Jeesus ütles neile: „Küllap te joote karikast, millest mina joon, ja teid ristitakse ristimisega, millega mind ristitakse.
40 lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
Kuid kes istub mu paremal või vasakul käel, ei ole minu määrata, vaid see antakse neile, kellele see on valmistatud.“
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
Kui need kümme sellest kuulsid, vihastasid nad Jaakobuse ja Johannese peale.
42 Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
Jeesus kutsus nad enese juurde ja ütles neile: „Te teate, et rahvaste valitsejad peremehetsevad nende üle ja võimukandjad kasutavad nende kallal jõudu.
43 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
Nõnda ärgu olgu teie seas, vaid kes iganes teie seas tahab saada suureks, olgu teie teenija,
44 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
ning kes iganes teie seas tahab olla esimene, olgu kõigi sulane.
45 Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
Sest ka Inimese Poeg ei ole tulnud, et lasta ennast teenida, vaid et ise teenida ja anda oma elu lunastuseks paljude eest!“
46 Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
Seejärel jõudsid nad Jeerikosse. Kui Jeesus koos jüngrite ja suure rahvahulgaga linnast lahkus, istus tee ääres pime kerjus Bartimeus (mis tähendab Timeuse poega).
47 Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Kui ta kuulis, et Naatsareti Jeesus on lähedal, hakkas ta karjuma: „Jeesus, Taaveti Poeg, halasta minu peale!“
48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Mitmed pahandasid temaga, et ta jääks vait, kuid tema karjus veel kõvemini: „Taaveti Poeg, halasta minu peale!“
49 Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
Jeesus seisatas ja ütles: „Kutsuge ta siia!“Ja nad kutsusid pimedat: „Ole julge! Tõuse üles, tema kutsub sind!“
50 Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
Pime viskas kuue seljast, hüppas püsti ja tuli Jeesuse juurde.
51 Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
Jeesus küsis temalt: „Mida sa tahad, et ma sulle teeksin?“Aga pime vastas: „Rabi, ma tahan näha!“
52 Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.
Jeesus ütles talle: „Mine, sinu usk on su terveks teinud!“Ja kohe nägi pime jälle ning läks Jeesusega teele kaasa.

< Marko 10 >