< Marko 10 >

1 Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
And He arose from thence and came into the coasts of Judea, through the country beyond Jordan: and the people resorted to Him again; and, as He was wont, He taught them again.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
And the pharisees came to Him and asked Him, "if it were lawful for a man to put away his wife," tempting Him.
3 Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
And he answered and said unto them, What did Moses command you?
4 Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
And they said, Moses permitted a man to write a bill of divorce, and to put her away.
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
And Jesus replied, He wrote this precept on account of your cruel tempers:
6 Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
but from the beginning of the world, God created them male and female.
7 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
For this cause shall a man leave his father and mother,
8 Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
and be joined to his wife, and they two shall be one flesh: so that they are no longer two, but one flesh.
9 Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
Therefore let not man separate what God hath joined together.
10 Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
And when they were in the house his disciples asked Him again about it:
11 Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
and He told them, Whoever putteth away his wife and marrieth another, committeth adultery against her.
12 Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
And if a woman be divorced from her husband, and be married to another, she committeth adultery.
13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
And they brought to Him little children that He might touch them: and the disciples rebuked those that brought them.
14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
Which Jesus observing, was much displeased, and said to them, Let the children come to me; and hinder them not; for of such is the kingdom of God.
15 Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
Verily I tell you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child, shall by no means enter into it.
16 Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
And He took them in his arms, and put his hands upon them, and blessed them.
17 Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
And as he went out into the way, there came one running and kneeling to Him, and asked Him, Good master, what shall I do, that I may inherit eternal life? (aiōnios g166)
18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
And Jesus said unto him, Why dost thou call me good? there is none good, but one, that is God.
19 Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
Thou knowest the commandments, Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Do not defraud, Honour thy father and thy mother.
20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
And he answered and said unto Him, Master, all these have I kept from my youth.
21 Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
Then Jesus looked upon him with affection, and said to him, One thing thou wantest; go, sell all that thou hast, and give it to the poor; and thou shalt have treasure in heaven; and come, take up the cross and follow me.
22 Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
But he was sad at that saying, and went away sorrowful; for he had great possessions.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
And Jesus looking round about saith to his disciples, How difficultly shall they that have riches enter into the kingdom of God!
24 Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
And the disciples were astonished at his words. But Jesus repeating it, saith unto them, Children, how hard is it for them, that trust in riches, to enter into the kingdom of God!
25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
It is easier for a camel to pass through the eye of a needle, than for a rich man to enter into the kingdom of God.
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
And they were exceedingly amazed, saying one to another, Who then can be saved?
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
But Jesus looking upon them saith, With men it is impossible, but not with God; for with God all things are possible.
28 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
Then Peter said to Him, Behold we have left all, and followed thee.
29 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
And Jesus answered and said, Verily I tell you, there is no one that hath left house, or brethren, or sisters, or father, or mother, or wife, or children,
30 ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
or lands for my sake and the gospel's, but he shall receive an hundred-fold: now in this time indeed, houses, and brethren, and sisters, and mothers, and children, and lands with persecutions; but in the world to come life everlasting. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many that are first shall be last, and the last first.
32 Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
And they were in the way going up to Jerusalem, and Jesus went before them: and they were amazed at it, and afraid to follow Him. And again taking the twelve aside, He began to tell them what things should befal Him,
33 Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
saying, Behold, we are going up to Jerusalem, and the Son of man shall be delivered to the chief priests, and the scribes, and they will condemn Him to death, and deliver Him to the Gentiles;
34 ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
and they will insult Him, and scourge Him, and spit upon Him, and put Him to death: but on the third day He shall rise again.
35 Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
Then come to Him James and John, the sons of Zebedee, saying, Master, we desire that thou wouldest do for us what we shall request:
36 Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
and He said to them, What do ye desire me to do for you?
37 Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
they said unto Him, Grant that we may sit, one on thy right hand, and the other on thy left, in thy glory.
38 Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
But Jesus said unto them, Ye know not what ye ask. Can ye drink of the cup, that I drink of? and be baptized with the baptism that I am baptized with?
39 Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
And they said, We can. And Jesus said unto them, The cup indeed which I drink, ye shall drink of; and with the baptism, that I am baptized with, shall ye be baptized:
40 lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
but to sit on my right hand and on my left, is not mine to give, but for whom it is prepared.
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
And when the other ten heard it, they were provoked at James and John.
42 Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
But Jesus called them to Him, and said unto them, Ye know that those who rule among the Gentiles, lord it over them, and their grandees exercise authority upon them.
43 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
But it shall not be so among you: but whoever would be great among you shall be your minister;
44 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
and whoever of you would be first shall be servant of all.
45 Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
For the Son of man came not to be ministred unto, but to minister and to give his life a ransom for many.
46 Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
And they came to Jericho: and as He was going out of Jericho, with his disciples and a great multitude, blind Bartimeus, the son of Timeus, sat by the way-side begging.
47 Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
And hearing that it was Jesus of Nazareth, he began to cry out, and say, Jesus, thou son of David, have mercy on me.
48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
And many rebuked him, that he might hold his peace: but he cried out so much the more, Thou son of David, have pity on me.
49 Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
And Jesus stopt, and ordered him to be called: so they called the blind man, and said to him, Be of good courage, rise up, He calleth thee.
50 Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
And he threw off his outer garment, and arose, and came to Jesus.
51 Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
And Jesus said to him, What dost thou desire that I should do for thee? And the blind man said to Him, Lord, that I may recover my sight.
52 Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.
And Jesus said unto him, Go thy way, thy faith has cured thee. And he immediately recovered his sight, and followed Jesus in the way.

< Marko 10 >