< Marko 10 >

1 Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
On leaving that place, Jesus went into the district of Judea on the other side of the Jordan. Crowds gathered about him again; and again, as usual, he began teaching them.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
Presently some Pharisees came up and, to test him, asked, ‘Has a husband the right to divorce his wife?’
3 Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
‘What direction did Moses give you?’ replied Jesus.
4 Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
‘Moses,’ they said, ‘permitted a man to draw up in writing a notice of separation and divorce his wife.’
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
‘It was owing to the hardness of your hearts,’ said Jesus, ‘that Moses gave you this direction;
6 Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
but, at the beginning of the Creation, “God made them male and female.”
7 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
“For this reason a man will leave his father and mother,
8 Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
and the man and his wife will become one;” so that they are no longer two, but one.
9 Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
What God himself, then, has yoked together no one must separate.’
10 Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
When they were indoors, the disciples asked him again about this,
11 Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
and he said, ‘Anyone who divorces his wife and marries another woman is guilty of adultery against his wife;
12 Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
and, if the woman divorces her husband and marries another man, she is guilty of adultery.’
13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
Some of the people were bringing little children to Jesus, for him to touch them; but the disciples rebuked those who had brought them.
14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
When, however, Jesus saw this, he was indignant. ‘Let the little children come to me,’ he said, ‘do not hinder them; for it is to the childlike that the kingdom of God belongs.
15 Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
I tell you, unless a person receives the kingdom of God like a child, they will not enter it at all.’
16 Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
Then he embraced the children, and, placing his hands on them, gave them his blessing.
17 Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
As Jesus was resuming his journey, a man came running up to him, and threw himself on his knees before him. ‘Good teacher,’ he asked, ‘what must I do to gain eternal life?’ (aiōnios g166)
18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
‘Why do you call me good?’ answered Jesus. ‘No one is good but God.
19 Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
You know the commandments – “Do not kill. Do not commit adultery. Do not steal. Do not say what is false about others. Do not cheat. Honour your father and your mother.”’
20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
‘Teacher,’ he replied, ‘I have observed all these from my childhood.’
21 Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
Jesus looked at the man, and his heart went out to him, and he said, ‘There is still one thing wanting in you; go and sell all that you have, and give to the poor, and you will have wealth in heaven; then come and follow me.’
22 Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
But the man’s face clouded at these words, and he went away distressed, for he had great possessions.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
Then Jesus looked round, and said to his disciples, ‘How hard it will be for people of wealth to enter the kingdom of God!’
24 Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
The disciples were amazed at his words. But Jesus said again, ‘My children, how hard a thing it is to enter the kingdom of God!
25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
It is easier for a camel to get through a needle’s eye, than for a rich person to enter the kingdom of God.’
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
‘Then who can be saved?’ they exclaimed in the greatest astonishment.
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
Jesus looked at them, and answered, ‘With people it is impossible, but not with God; for everything is possible with God.’
28 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
‘But we,’ began Peter, ‘we left everything and have followed you.’
29 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
‘I tell you,’ said Jesus, ‘there is no one who has left house, or brothers, or sisters, or mother, or father, or children, or land, for my sake and for the good news,
30 ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
who will not receive a hundred times as much, even now in the present – houses, and brothers, and sisters, and mothers, and children, and land, though not without persecutions – and in the age that is coming, eternal life. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many who are first now will then be last, and the last will be first.’
32 Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
They were on the road going up to Jerusalem, with Jesus walking in front of them. The disciples were filled with awe, while those who were following behind were overwhelmed with fear. Gathering the Twelve round him once more, Jesus began to tell them what was about to happen to him.
33 Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
‘Listen!’ he said. ‘We are going up to Jerusalem; and there the Son of Man will be betrayed to the chief priests and the teachers of the Law, and they will condemn him to death, and they will give him up to the Gentiles,
34 ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
who will mock him, spit on him, and scourge him, and put him to death; and after three days he will rise again.’
35 Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
James and John, the two sons of Zebedee, went to Jesus, and said, ‘Teacher, we want you to do for us whatever we ask.’
36 Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
‘What do you want me to do for you?’ he asked.
37 Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
‘Grant us this,’ they answered, ‘to sit, one on your right, and the other on your left, when you come in glory.’
38 Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
‘You do not know what you are asking,’ Jesus said to them. ‘Can you drink the cup that I am to drink? Or receive the baptism that I am to receive?’
39 Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
‘Yes,’ they answered, ‘we can.’ ‘You will indeed drink the cup that I am to drink,’ Jesus said, ‘and receive the baptism that I am to receive,
40 lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
but as to a seat at my right or at my left – that is not mine to give, but it is for those for whom it has been prepared.’
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
On hearing of this, the ten others were at first very indignant about James and John.
42 Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
But Jesus called the ten to him, and said, ‘Those who are regarded as ruling among the Gentiles lord it over them, as you know, and their great men oppress them.
43 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
But among you it is not so. No, whoever wants to become great among you must be your servant,
44 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
and whoever wants to take the first place among you must be the servant of all;
45 Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
for even the Son of Man came, not be served, but to serve, and to give his life as a ransom for many.’
46 Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
They came to Jericho. When Jesus was going out of the town with his disciples and a large crowd, Bartimaeus, the son of Timaeus, a blind beggar, was sitting by the roadside.
47 Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Hearing that it was Jesus the Nazarene, he began to call out, ‘Jesus, Son of David, take pity on me.’
48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Many of the people kept telling him to be quiet; but the man continued to call out all the louder, ‘Son of David, take pity on me.’
49 Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
Then Jesus stopped. ‘Call him,’ he said. So they called the blind man. ‘Have courage!’ they exclaimed. ‘Get up; he is calling you.’
50 Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
The man threw off his cloak, sprang up, and came to Jesus.
51 Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
‘What do you want me to do for you?’ said Jesus, addressing him. ‘Rabboni,’ the blind man answered, ‘I want to recover my sight.’
52 Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.
‘You may go,’ Jesus said, ‘Your faith has delivered you.’ Immediately he recovered his sight, and began to follow Jesus along the road.

< Marko 10 >