< Marko 10 >

1 Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
And he arose from thence, and went into the coastes of Iudea by the farre side of Iordan, and the people resorted vnto him againe, and as he was wont, he taught them againe.
2 Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
Then the Pharises came and asked him, if it were lawfull for a man to put away his wife, and tempted him.
3 Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
And he answered, and sayde vnto them, What did Moses commaund you?
4 Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
And they sayd, Moses suffered to write a bill of diuorcement, and to put her away.
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
Then Iesus answered, and sayd vnto them, For the hardnesse of your heart he wrote this precept vnto you.
6 Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
But at the beginning of the creation God made them male and female:
7 Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
For this cause shall man leaue his father and mother, and cleaue vnto his wife.
8 Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
And they twaine shalbe one flesh: so that they are no more twaine, but one flesh.
9 Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
Therefore, what God hath coupled together, let not man separate.
10 Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
And in the house his disciples asked him againe of that matter.
11 Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
And he sayd vnto them, Whosoeuer shall put away his wife and marrie another, committeth adulterie against her.
12 Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
And if a woman put away her husband, and be married to another, she committeth adulterie.
13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
Then they brought litle children to him, that he should touch them, and his disciples rebuked those that brought them.
14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
But when Iesus sawe it, he was displeased, and said to them, Suffer the litle children to come vnto me, and forbid them not: for of such is the kingdome of God.
15 Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
Verely I say vnto you, Whosoeuer shall not receiue the kingdome of God as a litle childe, he shall not enter therein.
16 Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
And he tooke them vp in his armes, and put his hands vpon them, and blessed them.
17 Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
And when hee was gone out on the way, there came one running, and kneeled to him, and asked him, Good Master, what shall I doe, that I may possesse eternall life? (aiōnios g166)
18 Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
Iesus sayde to him, Why callest thou me good? there is none good but one, euen God.
19 Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
Thou knowest the comandements, Thou shalt not commit adulterie. Thou shalt not kill. Thou shalt not steale. Thou shalt not beare false witnesse. Thou shalt hurt no man. Honour thy father and mother.
20 Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
Then he answered, and said to him, Master, all these things I haue obserued from my youth.
21 Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
And Iesus looked vpon him, and loued him, and sayde vnto him, One thing is lacking vnto thee. Go and sell all that thou hast, and giue to the poore, and thou shalt haue treasure in heauen, and come, follow me, and take vp the crosse.
22 Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
But hee was sad at that saying, and went away sorowfull: for he had great possessions.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
And Iesus looked round about, and sayd vnto his disciples, Howe hardly doe they that haue riches, enter into the kingdome of God!
24 Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
And his disciples were afraide at his words. But Iesus answered againe, and sayd vnto them, Children, how hard is it for them that trust in riches, to enter into the kingdome of God!
25 Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
It is easier for a camel to goe through the eye of a needle, then for a riche man to enter into the kingdome of God.
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
And they were much more astonied, saying with themselues, Who then can be saued?
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
But Iesus looked vpon them, and sayd, With men it is impossible, but not with God: for with God all things are possible.
28 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
Then Peter began to say vnto him, Loe, we haue forsaken all, and haue folowed thee.
29 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
Iesus answered, and sayd, Verely I say vnto you, there is no man that hath forsaken house, or brethren, or sisters, or father, or mother, or wife, or children, or lands for my sake and the Gospels,
30 ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
But he shall receiue an hundred folde, now at this present, houses, and brethren, and sisters, and mothers, and children, and lands with persecutions, and in the world to come, eternall life. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many that are first, shall be last, and the last, first.
32 Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
And they were in the way going vp to Hierusalem, and Iesus went before them and they were troubled, and as they followed, they were afraide, and Iesus tooke the twelue againe, and began to tell them what things should come vnto him,
33 Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
Saying, Beholde, we goe vp to Hierusalem, and the Sonne of man shall be deliuered vnto the hie Priests, and to the Scribes, and they shall condemne him to death, and shall deliuer him to the Gentiles.
34 ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
And they shall mocke him, and scourge him, and spit vpon him, and kill him: but the third day he shall rise againe.
35 Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
Then Iames and Iohn the sonnes of Zebedeus came vnto him, saying, Master, we would that thou shouldest doe for vs that we desire.
36 Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
And he sayd vnto them, What would ye I should doe for you?
37 Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
And they said to him, Graunt vnto vs, that we may sit, one at thy right hand, and the other at thy left hand in thy glory.
38 Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
But Iesus sayd vnto them, Ye knowe not what ye aske. Can ye drinke of the cup that I shall drinke of, and be baptized with the baptisme that I shall be baptized with?
39 Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
And they said vnto him, We can. But Iesus sayd vnto them, Ye shall drinke in deede of the cup that I shall drinke of, and be baptized with the baptisme wherewith I shalbe baptized:
40 lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
But to sit at my right hand, and at my left, is not mine to giue, but it shalbe giuen to them for whome it is prepared.
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
And when the ten heard that, they began to disdaine at Iames and Iohn.
42 Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
But Iesus called them vnto him, and sayd to them, Ye know that they which are princes among the Gentiles, haue domination ouer them, and they that be great among them, exercise authoritie ouer them.
43 Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
But it shall not be so among you: but whosoeuer will be great among you, shall be your seruant.
44 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
And whosoeuer will be chiefe of you, shall be the seruant of all.
45 Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
For euen the Sonne of man came not to be serued, but to serue, and to giue his life for the raunsome of many.
46 Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
Then they came to Iericho: and as he went out of Iericho with his disciples, and a great multitude, Bartimeus the sonne of Timeus, a blinde man, sate by the wayes side, begging.
47 Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
And when hee heard that it was Iesus of Nazareth, he began to crye, and to say, Iesus the Sonne of Dauid, haue mercy on me.
48 Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
And many rebuked him, because he should holde his peace: but hee cryed much more, O Sonne of Dauid, haue mercy on me.
49 Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
Then Iesus stood still, and commanded him to be called: and they called the blind, saying vnto him, Be of good comfort: arise, he calleth thee.
50 Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
So he threwe away his cloke, and rose, and came to Iesus.
51 Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
And Iesus answered, and said vnto him, What wilt thou that I doe vnto thee? And the blinde sayd vnto him, Lord, that I may receiue sight.
52 Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.
Then Iesus sayde vnto him, Goe thy way: thy fayth hath saued thee. And by and by, he receiued his sight, and folowed Iesus in the way.

< Marko 10 >