< Marko 1 >
1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the Good News of Jesus Christ, the Son of God.
2 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
As it is written in Isaiah the prophet, "Look, I send my messenger ahead of you, who will prepare your way before you.
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
The voice of one crying in the wilderness, 'Prepare the way of the Lord. Make his roads straight.'"
4 Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
John came baptizing in the wilderness and preaching a baptism of repentance for forgiveness of sins.
5 Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
And all the country of Judea went out to him and all those from Jerusalem, and they were baptized by him in the Jordan river, confessing their sins.
6 Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
And John was clothed with camel's hair and a leather belt around his waist. He ate locusts and wild honey.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
And he preached, saying, "After me comes he who is mightier than I, the strap of whose sandals I am not worthy to stoop down and loosen.
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I baptized you in water, but he will baptize you in the Holy Spirit."
9 Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
And it happened in those days, that Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by John in the Jordan.
10 Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
Immediately coming up from the water, he saw the heavens parting, and the Spirit descending on him like a dove.
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
And a voice came out of the sky, "You are my beloved Son, with you I am well pleased."
12 Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
And immediately the Spirit drove him out into the wilderness.
13 naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
He was in the wilderness forty days tempted by Satan. He was with the wild animals; and the angels were serving him.
14 Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
Now after John was taken into custody, Jesus came into Galilee, proclaiming the Good News of God,
15 akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
and saying, "The time is fulfilled, and the Kingdom of God is near. Repent, and believe in the Good News."
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
And passing along by the sea of Galilee, he saw Simon and Andrew the brother of Simon casting a net into the sea, for they were fishermen.
17 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
Jesus said to them, "Come, follow me, and I will make you into fishers of people."
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
And immediately they left the nets, and followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And going on a little further, he saw James the son of Zebedee, and John, his brother, who were also in the boat mending the nets.
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
And immediately he called them, and they left their father, Zebedee, in the boat with the hired servants, and went after him.
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
And they went into Capernaum, and immediately on the Sabbath day he entered into the synagogue and taught.
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
And they were astonished at his teaching, for he taught them as having authority, and not as the scribes.
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
And just then there was in their synagogue a man with an unclean spirit, and he shouted,
24 naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
saying, "What do we have to do with you, Jesus, Nazarene? Have you come to destroy us? I know you who you are: the Holy One of God."
25 Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
And Jesus rebuked him, saying, "Be quiet, and come out of him."
26 Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
And the unclean spirit, convulsing him and crying with a loud voice, came out of him.
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
And they were all amazed, so that they questioned among themselves, saying, "What is this? A new teaching? For with authority he commands even the unclean spirits, and they obey him."
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
And at once the news of him went out everywhere into all the region of Galilee and its surrounding area.
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
And Immediately, when they had come out of the synagogue, they came into the house of Simon and Andrew, with James and John.
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
Now Simon's mother-in-law was sick in bed with a fever, and immediately they told him about her.
31 Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
And he came and took her by the hand, and raised her up. The fever left her, and she served them.
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
At evening, when the sun had set, they brought to him all who were sick, and those who were possessed by demons.
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
And all the city was gathered together at the door.
34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
And he healed many who were sick with various diseases, and cast out many demons. He did not allow the demons to speak, because they knew him.
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
And early in the morning, while it was still dark, he rose up and went out, and departed into a deserted place, and prayed there.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
And Simon and those who were with him followed after him;
37 nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
and they found him, and told him, "Everyone is looking for you."
38 Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
And he said to them, "Let us go somewhere else into the next towns, that I may preach there also, because I came out for this reason."
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
And he went into their synagogues throughout all Galilee, preaching and casting out demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
And a leper came to him, begging him, and knelt down and said to him, "Lord, if you want to, you can make me clean."
41 Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
And being moved with compassion, he stretched out his hand, and touched him, and said to him, "I am willing. Be cleansed."
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
And immediately the leprosy departed from him, and he was made clean.
43 Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
And he strictly warned him, and immediately sent him out,
44 akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
and said to him, "See you say nothing to anyone, but go show yourself to the priest, and offer for your cleansing the things which Moses commanded, for a testimony to them."
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
But he went out, and began to proclaim it freely, and to spread about the matter, so that Jesus could no more openly enter into a city, but was outside in desert places: and they came to him from everywhere.