< Marko 1 >

1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
Here is the beginning of the good news about Jesus Christ, the Son of God.
2 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
Just as the prophet Isaiah wrote, “I'm sending my messenger ahead of you to prepare your way.
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
A voice is calling in the desert, ‘Prepare the Lord's way! Make his paths straight.’”
4 Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
John came, baptizing in the desert, announcing a baptism of repentance for the forgiveness of sins.
5 Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
Everybody from the country of Judea and from Jerusalem went to him. They admitted their sins publicly and were baptized in the Jordan River.
6 Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
John wore clothes made of camel hair, with a leather belt around his waist. He ate locusts and wild honey.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
This is what he had to say: “After me someone is coming who is greater than I am. I'm not worthy to bend down and untie his sandals.
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I baptized you in water but he will baptize you in the Holy Spirit.”
9 Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
Then Jesus came from Nazareth in Galilee and was baptized by John in the Jordan River.
10 Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
As Jesus came out of the water, he saw the heavens split apart and the Spirit like a dove descending upon him.
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
A voice from heaven said, “You are my son, the one I love. I am very pleased with you.”
12 Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
Right after this the Spirit sent him away into the desert
13 naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
where he was tempted by Satan for forty days. He was with the wild animals, and angels took care of him.
14 Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
Later, after John was arrested, Jesus went to Galilee, announcing God's good news.
15 akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
“The time predicted has come,” he said. “God's kingdom has arrived! Repent and believe in the good news.”
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
As he was walking beside the Sea of Galilee, Jesus saw Simon and his brother Andrew throwing a net into the water, for they made their living by fishing.
17 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
“Come and follow me,” he told them, “and I will have you fishing for people.”
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
They left their nets at once and followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
He went a little farther and saw James and his brother John, the sons of Zebedee. They were in a boat mending their nets.
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
Immediately he called them to follow him, and they left their father Zebedee in the boat with the hired workers, and followed Jesus.
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
They left for Capernaum, and on Sabbath Jesus went into the synagogue and taught there.
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
The people were amazed at his teaching, for he spoke with authority, unlike the religious teachers.
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
Suddenly, right there in the synagogue, a man with an evil spirit started shouting out,
24 naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
“Jesus of Nazareth, why are you bothering us? Have you come to destroy us? I know who you are! You're God's Holy One!”
25 Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
Jesus interrupted the evil spirit, telling him, “Be quiet! Come out of him.”
26 Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
The evil spirit screamed, threw the man into convulsions, and came out of him.
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
Everyone was amazed at what happened. “What is this?” they asked each other. “What is this new teaching that has such authority? Even evil spirits do what he tells them!”
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
News about him spread quickly throughout the whole region of Galilee.
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
Then they left the synagogue and went to the home of Simon and Andrew, along with James and John.
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
Simon's mother-in-law was sick in bed with a fever, so they told Jesus about her.
31 Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
He went to her, took her by the hand, and helped her up. The fever immediately left her. Then she made them a meal.
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
After sunset that evening, those who were sick and demon-possessed were brought to Jesus.
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
The whole of the town gathered outside.
34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
He healed many people who had various diseases, and threw out many demons. He did not permit the demons to speak, for they knew who he was.
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
Very early in the morning, while it was still dark, Jesus got up and went alone to a quiet place to pray.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
Simon and the others went to search for him.
37 nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
When they found him, they told him, “Everybody's looking for you.”
38 Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
But Jesus replied, “We have to go to the other towns around here so that I can tell them the good news as well—for that's why I came.”
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
So he went all over Galilee, speaking in the synagogues and expelling demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
A leper came to him asking for help. The man kneeled down before Jesus, saying, “Please, if you're willing, you can heal me!”
41 Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
With compassion Jesus reached out and touched the man, and said, “I am willing. Be healed!”
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
The leprosy left him immediately, and he was healed.
43 Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
Jesus sent him away with a strong warning.
44 akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
“Make sure you don't tell anybody anything about this,” he told him. “Go to the priest and show yourself to him. Give the offering which is required by the law of Moses for such cleansing, so that people will have proof.”
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
But the healed leper went out and told everyone what had happened. As a result Jesus could not openly go into the cities anymore, but had to stay out in the country where people came to him from everywhere around.

< Marko 1 >