< Marko 1 >
1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
Hin hin Pamhnama Capa Jesuh Khritawa mawng Thangkdaw ni.
2 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
“Pamhnam naw, ‘na maa ka ngsä, lam pyang khaia ka tüi law khai.’
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
Khyang mat, khawkhyawng khawa ngpyangki naw, ‘Bawipa a lam pyang ua; a cehnak vai lam ngdüngsak ua!’ a ti” tia, akphyüma sahma Hesajah naw, a yuka kba.
4 Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
Acunüng, Johan khawkhyawng khawa ngdang law lü, baptican jah pe law lü, jah mtheimthang law lü, “Nami katnak nghlata u lü Baptican khan ua, Pamhnam naw nami katnak he ning jah mhlät khai ni,” a ti.
5 Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
Acunüng, Judah khaw la Jerusalem mlüha khyang he ngthu ngai khaia Johana veia citki he. Ami katnak he jah phyeh u se Jordan tuinu üng Johan naw baptican a jah khansak.
6 Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
Johan cun samu am ami pyan suisak suisa lü, savunksawmyüi a kcawi üng vawp lü, mkhaü he la mawkpyawnga khawitui jah ei awki.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
Johan naw sang lü, “Ka hnua law khaia khyang ta keia kthaka kyäp bawk ve, kei cun kawp lü a khawdawkyüi ka kphyan pe khaia pi am ka ngkawihki ni.
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
Kei naw tui am baptican ka ning jah peki, cunsepi ani naw Ngmüimkhya Ngcim am Baptican ning jah pe khai,” a ti.
9 Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
Acun käna ivei am ngsawk se, Jesuh Kalile khaw Nazaret üngka naw law se, Johan naw Jordan tuinu üng baptican a pet.
10 Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
Tui üngka naw angxita a thawh law be üng, khankhaw nghmawng law lü, Ngmüimkhya cun mümca kba a khana kyum law se a hmuh.
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
Acunüng khankhaw üngka kthai naw, “Nang, ka ning jawng'engnak kcanga ka Capa, na khana ka je leng lengki,” tia, ngthang lawki.
12 Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
Acun la Ngmüimkhya naw khawkhyawng khawa a tüih.
13 naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
Acuia khawmhmüp kphyükip khawyam naw hlawhlep se awmki. Khisa he pi awmki he, acunüngpi khankhawngsä he naw law u lü ami msümcei law.
14 Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
Johan thawngim üng ami khyum käna, Jesuh Kalile khawa cit lü, Mhnama Thangkdaw pyen hü lü,
15 akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
“Akcün pha lawpäng ve, Mhnama khaw ng’et law ve! Nami katnak he jah nghlata u lü, thangkdaw jum ua!” a ti.
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
Kalile tuili kama Jesuh a ceh üng, Sihmon la a na Andru ngvai vawiki xawi jah hmu lü,
17 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
Jesuh naw, “Na läk law nia, kei naw khyang man khaia ka ning jah mthei khai,” a ti.
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
Acunüng angxita ani ngvai jah yawk hüt ni lü, Jesuha hnu läki xawi.
19 Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
Acun üngka naw, asäng va cit lü, Zebedea capa Jakuk la a na Johan, mlawnga khana ani ngvai jah na pyangei ni se a jah hmuh.
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
Jesuh naw a jah hmuh la jah khü se, ani pa Zebede la mlawnga khana ani jah ngvaha khyang he jah yawk hüt ni lü, Jesuha hnu läki xawi.
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
Jesuh la axüisaw he Kapenawm mlüha law u se, angawi Sabbath mhmüp üng Jesuh naw Sinakok k’uma lut lü, a jah mthei.
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
Thum jah mtheiki hea kba am kya lü, ana takia kba jah mthei se khyang he aktäa cäiki he.
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
Acunüng, ami Sinakoka k’uma khyang mat, ngmüimkhyaksea awmnak naw,
24 naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
“Nazaret Jesuh aw, i mi nglak ve se ja? Na jah kpyeh khaia na lawki aw? Nang u ti ka ksingki. Nang cun Mhnama ngsä ngcim ni!” ti lü, ngpyangki.
25 Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
Jesuh naw, “Ä khihkhe lü, a k’um üngka naw, angxita lut lawa,” ti lü, ngmüimkhya kse a ksät.
26 Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
Khawyai naw acuna khyang cun ksün lü, angsanga ngpyang lü, lut lawki.
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
Khyang he ami van cäi law u lü, “Hin hin ia ngkhaw ni? Ahina mtheimthangnak hin akthai am niki aw? Ana takia kba khawyai he pi jah ksät se, a pyen ngaiki he hin,” tia mat la mat ngthähki he.
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
Acun la angxita, Kalile khaw avan üng Jesuha mawng ngthang hüki.
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
Jesuh la axüisaw he Sinakok üngka naw lut law u lü, Jakuk la Johan am, Sihmon la Andrua ima cit ktäiki he.
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
Sihmona pi, mhnatei se ngjänki, Jesuh a pha law la ami mtheh.
31 Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
Jesuh naw a veia cit lü, a kut üng kaih lü, a mthawh la mhnat naw khya se, acun la a jah khinak.
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
Mü lam khawkyak käna, am phetki he avan la khawyai he naw a jah awmnak avan he cun Jesuha veia ami jah lawpüi.
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
Mlüh üngka khyang avan mkawt maa ngcun lawki he.
34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
Jesuh naw natnak ahmäi hmäia phäha am phetki he jah m’yai be lü khawyai he a jah ksät. Khawyai he naw ani cun ami ksinga phäha ani naw ä a jah ngthuheisak.
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
Ngawi lam khaw am a thaih phat üng, Jesuh tho law lü im ceh ta lü, anghinaka hmüna cit lü, va ktaiyüki.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
Cunsepi Sihmon la a püi he cun Jesuh sui khai hea citki he.
37 nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
Acunüng, ami hmuh law üng, “Khyang avan naw ning suihüki he ni,” ami ti.
38 Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
Cunsepi, Jesuh naw, “Ahina pipei ngnam hea pi, ngthu ka pyen khaia mi cit khai, acun vaia ni kei ka law,” a ti.
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
Acukba, Jesuh cun Kalile khaw avan üng cit hü lü, Sinakok hea ngthu pyen hü lü, khawyai he pi jah ksätki.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
Mnehkse mnehki khyang mat Jesuha veia law lü, a mkhuk ngdäng lü, “Na hlüei üng ta, na na ngcimcaihsak theiki ni,” ti lü, a nghuinak.
41 Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
Jesuh naw m'yeneinak am a kut sängki naw hnet lü, “Ä, hlüei veng, ngcima,” a ti.
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
Acukba a pyen la angxita mnehkse cun khyük se, ani cun ngcimcai law beki.
43 Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
Acunüng Jesuh naw ksükki naw a tüih be.
44 akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
Acukba a pyen käna, “U am icapi ä na mtheh vai, cit lü, ktaiyü am na va ngtengei kyusak vai, acunüng Mosi naw a jah mtheha kba, na ngcimcainak ami msingnak vaia ngkengnak va pawha,” ti lü a tüih be.
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
Cunsepi, acuna khyang naw cit lü acuna mawng cun avan üng va sang hü se, Jesuh angdanga mlüh k’uma am lut thei lü anghinaka awmki. Acuia, khyang pung akce kce üngka he naw ami ceh si.