< Malaki 1 >
1 Ujumbe: Neno la Bwana kwa Israeli kupitia kwa Malaki.
RAB'bin Malaki aracılığıyla İsrail halkına bildirisi.
2 Bwana asema, “Nimewapenda ninyi.” “Lakini ninyi mnauliza, ‘Wewe umetupendaje?’” Bwana asema, “Je, Esau hakuwa ndugu yake Yakobo? Hata hivyo nimempenda Yakobo,
RAB, “Sizi sevdim” diyor. “Oysa siz, ‘Bizi nasıl sevdin?’ diye soruyorsunuz.” RAB, “Esav Yakup'un ağabeyi değil mi?” diye karşılık veriyor, “Ben Yakup'u sevdim,
3 lakini nikamchukia Esau, nami nimeifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa jangwani.”
Esav'dan ise nefret ettim. Dağlarını viraneye çevirdim, yurdunu kırın çakallarına verdim.”
4 Edomu anaweza kusema, “Ingawa tumepondapondwa, tutajenga upya magofu.” Lakini hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Wanaweza kujenga, lakini nitabomoa. Wataitwa Nchi Ovu, watu ambao siku zote wapo chini ya ghadhabu ya Bwana.
Edomlular, “Biz ezildik, ama yıkıntıları yeniden kuracağız” deseler de, Her Şeye Egemen RAB şu karşılığı verecek: “Onlar kurabilirler, ama ben yıkacağım. Ülkeleri kötülük ülkesi, kendileri de RAB'bin her zaman lanetlediği halk olarak tanınacak.
5 Mtayaona kwa macho yenu wenyewe na kusema, ‘Bwana ni mkuu, hata nje ya mipaka ya Israeli!’
Bunu gözlerinizle görünce, ‘RAB İsrail sınırının ötesinde de büyüktür!’ diyeceksiniz.”
6 “Mwana humheshimu baba yake, naye mtumishi humheshimu bwana wake. Kama mimi ni baba, iko wapi heshima ninayostahili? Kama mimi ni bwana, iko wapi heshima ninayostahili?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau Jina langu. “Lakini mnauliza, ‘Tumelidharau Jina lako kwa namna gani?’
Her Şeye Egemen RAB, adını küçümseyen siz kâhinlere, “Oğul babasına, kul efendisine saygı gösterir” diyor, “Eğer ben babaysam, hani bana saygınız? Eğer efendiysem, hani benden korkunuz? “Oysa siz, ‘Adını nasıl küçümsedik?’ diye soruyorsunuz.
7 “Mnatoa sadaka chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu. “Lakini ninyi mnauliza, ‘Tumekutia unajisi kwa namna gani?’ “Kwa kusema kuwa meza ya Bwana ni ya kudharauliwa.
“Hem sunağıma murdar yiyecek getiriyor, hem de, ‘Yiyeceği nasıl murdar ettik?’ diye soruyorsunuz. “‘RAB'bin sofrası küçümsenir’ demenizle.
8 Wakati mletapo dhabihu za wanyama walio vipofu, je, hilo si kosa? Mnapoleta dhabihu zilizo vilema au wanyama wagonjwa, je, hilo si kosa? Jaribuni kuvitoa kwa mtawala wenu! Je, angefurahishwa nanyi? Je, atawakubalia?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Kör hayvan kurban etmek kötü değil mi? Topal ya da hasta hayvan kurban etmek kötü değil mi? Böyle bir hayvanı kendi valine sun bakalım! Senden hoşnut kalır mı, ya da seni kabul eder mi?” Böyle diyor Her Şeye Egemen RAB.
9 “Basi mwombeni Mungu awe na neema kwetu. Je, kwa sadaka kama hizo kutoka mikononi mwenu, atawapokea?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
“Şimdi bize lütfetmesi için Tanrı'ya yalvarın. Siz böyle sunular sunarken hiç sizi kabul eder mi?” Böyle diyor Her Şeye Egemen RAB.
10 “Laiti mmoja wenu angalifunga milango ya Hekalu, ili msije mkawasha moto usiokuwa na faida juu ya madhabahu yangu! Sina furaha nanyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nami sitaikubali sadaka toka mikononi mwenu.
“Ne olurdu, sunağımda boşuna ateş yakmayasınız diye aranızda tapınağın kapılarını kapatan biri olsaydı! Ben sizden hoşnut değilim” diyor Her Şeye Egemen RAB, “Getireceğiniz sunuları da kabul etmeyeceğim.
11 Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa, kuanzia mawio ya jua hata machweo yake. Kila mahali uvumba na sadaka safi zitaletwa kwa Jina langu, kwa sababu Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Doğudan batıya kadar uluslar arasında adım büyük olacak! Her yerde adıma buhur yakılacak, temiz sunular sunulacak. Çünkü uluslar arasında adım büyük olacak!” diyor Her Şeye Egemen RAB.
12 “Lakini mnalinajisi Jina langu kwa kusema kuhusu meza ya Bwana, ‘Imetiwa unajisi pamoja na chakula chake. Ni ya kudharauliwa.’
“‘Rab'bin sofrası murdardır, yemeği de küçümsenir’ diyerek adımı bayağılaştırıyorsunuz.
13 Nanyi mnasema, ‘Mzigo gani huu!’ Nanyi mnaidharau kwa kiburi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Wakati mnapowaleta wanyama mliopokonya kwa nguvu, walio vilema au walio wagonjwa na kuwatoa kama dhabihu, je, niwakubali kutoka mikononi mwenu?” asema Bwana.
Üstelik, ‘Ne yorucu!’ diyerek bana burun kıvırıyorsunuz.” Böyle diyor Her Şeye Egemen RAB. “Kurban olarak çalıntıyı, topalı, hastayı getirdiğinizde, elinizden kabul mu edeyim?” diye soruyor RAB.
14 “Amelaaniwa yeye adanganyaye, aliye na mnyama wa kiume anayekubalika katika kundi lake na kuweka nadhiri ya kumtoa, lakini akatoa dhabihu ya mnyama aliye na dosari kwa Bwana. Kwa kuwa mimi ni Mfalme Mkuu, nalo Jina langu linapaswa kuogopwa miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
“Sürüsünden adadığı erkek hayvan yerine Rab'be kusurlu hayvan kurban eden aldatıcıya lanet olsun! Çünkü ben büyük bir kralım” diyor Her Şeye Egemen RAB, “Ve uluslar adımdan korku duyacak.”