< Malaki 4 >

1 “Hakika siku inakuja, itawaka kama tanuru. Wote wenye kiburi na kila mtenda mabaya watakuwa mabua makavu, na siku ile inayokuja itawawasha moto,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Hakuna mzizi wala tawi litakalosalia kwao.
Denn siehe, es kommt der Tag, der wie der Ofen brennt; und alle Vermessenen und die, so Ungerechtigkeit taten, sind Stoppel, und der Tag, der kommt, entflammt sie, spricht Jehovah der Heerscharen, und weder Wurzel, noch Ast wird er denselben hinterlassen.
2 Bali kwenu ninyi mnaoliheshimu Jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mabawa yake. Nanyi mtatoka nje na kurukaruka kama ndama aliyeachiwa kutoka zizini.
Euch aber, die ihr Meinen Namen fürchtet, wird aufgehen die Sonne der Gerechtigkeit, und Heilung unter ihren Flügeln, und ihr geht aus und wachset heran wie die Mastkälber.
3 Kisha ninyi mtawakanyaga waovu, nao watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu siku ile nitakayofanya mambo haya,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Und die Gottlosen werdet ihr daniedertreten; denn Asche sollen sie unter den Sohlen eurer Füße sein an dem Tage, den Ich mache, spricht Jehovah der Heerscharen.
4 “Kumbukeni sheria ya mtumishi wangu Mose, amri na sheria nilizompa huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote.
Gedenkt an das Gesetz des Moses, Meines Knechtes, das Ich ihm gebot auf Choreb an ganz Israel, an die Satzungen und Rechte.
5 “Tazama, nitawapelekea nabii Eliya kabla ya kuja siku ile iliyo kuu na ya kutisha ya Bwana.
Siehe, Ich sende euch Elijah, den Propheten, bevor da kommt der Tag Jehovahs, der große und furchtbare.
6 Ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, la sivyo nitakuja na kuipiga nchi kwa laana.”
Und er wird das Herz der Väter zu den Söhnen zurückwenden, und das Herz der Söhne zu ihren Vätern, auf daß Ich nicht komme und schlage mit dem Banne das Land.

< Malaki 4 >