< Malaki 4 >

1 “Hakika siku inakuja, itawaka kama tanuru. Wote wenye kiburi na kila mtenda mabaya watakuwa mabua makavu, na siku ile inayokuja itawawasha moto,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Hakuna mzizi wala tawi litakalosalia kwao.
“The day is coming that will burn like a furnace, and all the proud and all evildoers will be stubble, and the day that is coming will burn them up,” says the Lord of hosts, “leaving neither root nor branch.
2 Bali kwenu ninyi mnaoliheshimu Jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mabawa yake. Nanyi mtatoka nje na kurukaruka kama ndama aliyeachiwa kutoka zizini.
But to you who revere my name there will arise the sun of righteousness with healing in its wings, and you will run free like calves let out from their stall.
3 Kisha ninyi mtawakanyaga waovu, nao watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu siku ile nitakayofanya mambo haya,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
In the day when I act you will tread down the wicked, they will be as ashes under the soles of your feet,” says the Lord of hosts.
4 “Kumbukeni sheria ya mtumishi wangu Mose, amri na sheria nilizompa huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote.
“Remember the law of Moses my servant, statutes and judgments which I gave him at Horeb for all Israel.
5 “Tazama, nitawapelekea nabii Eliya kabla ya kuja siku ile iliyo kuu na ya kutisha ya Bwana.
I am about to send to you Elijah the prophet, before the great and terrible day of the Lord comes.
6 Ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, la sivyo nitakuja na kuipiga nchi kwa laana.”
He will turn fathers’ hearts to their sons and sons’ hearts to their fathers, so that I will not come and strike the earth with judgement.”

< Malaki 4 >