< Malaki 4 >

1 “Hakika siku inakuja, itawaka kama tanuru. Wote wenye kiburi na kila mtenda mabaya watakuwa mabua makavu, na siku ile inayokuja itawawasha moto,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Hakuna mzizi wala tawi litakalosalia kwao.
For, behold, the day cometh, which shall burn as an oven; Then shall all the proud, And all that do wickedness, be stubble; And the day that cometh shall burn them up, Saith Jehovah of hosts; It shall leave them neither root nor branch.
2 Bali kwenu ninyi mnaoliheshimu Jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mabawa yake. Nanyi mtatoka nje na kurukaruka kama ndama aliyeachiwa kutoka zizini.
But for you that fear my name Shall the sun of salvation arise With healing under his wings. And ye shall go forth and leap for joy, Like calves of the stall.
3 Kisha ninyi mtawakanyaga waovu, nao watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu siku ile nitakayofanya mambo haya,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And ye shall tread down the wicked; For they shall be as dust under the soles of your feet In the day which I appoint, saith Jehovah of hosts.
4 “Kumbukeni sheria ya mtumishi wangu Mose, amri na sheria nilizompa huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote.
Remember ye the law of Moses, my servant, Which I commanded him in Horeb for all Israel, My statutes and precepts!
5 “Tazama, nitawapelekea nabii Eliya kabla ya kuja siku ile iliyo kuu na ya kutisha ya Bwana.
Behold, I will send you Elijah, the prophet, Before the day of Jehovah come, The great and terrible day.
6 Ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, la sivyo nitakuja na kuipiga nchi kwa laana.”
He shall turn the heart of the fathers to the children, And the heart of the children to their fathers, That I may not come And smite the land with a curse.

< Malaki 4 >