< Malaki 3 >
1 “Angalieni, nitamtuma mjumbe wangu, atakayeiandaa njia mbele yangu. Ndipo ghafula Bwana mnayemtafuta atakuja hekaluni mwake. Mjumbe wa Agano, ambaye mnamwonea shauku, atakuja,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Lo! Y sende myn aungel, and he schal make redi weie bifor my face; and anoon the lordshipere, whom ye seken, schal come to his hooli temple, and the aungel of testament, whom ye wolen. Lo! he cometh, seith the Lord of oostis;
2 Lakini ni nani atakayeweza kustahimili hiyo siku ya kuja kwake? Ni nani awezaye kusimama atakapotokea? Kwa kuwa atakuwa kama moto wa mfua fedha au kama sabuni ya afuaye nguo.
and who schal mowe thenke the dai of his comyng? and who schal stonde for to se hym? For he schal be as fier wellynge togidere, and as erbe of fulleris;
3 Ataketi kama mfuaji na asafishaye fedha. Atawatakasa Walawi, naye atawasafisha kama dhahabu na fedha. Kisha Bwana atakuwa na watu watakaoleta sadaka katika haki,
and he schal sitte wellynge togidere and clensynge siluer, and he schal purge the sones of Leuy; and he schal purge hem as gold and as siluer, and thei schulen be offrynge to the Lord sacrifices in riytfulnesse.
4 nazo sadaka za Yuda na Yerusalemu zitakubalika kwa Bwana, kama katika siku zilizopita, kama katika miaka ya zamani.
And the sacrifice of Juda and of Jerusalem schal plese to the Lord, as the daies of the world, and as olde yeeris.
5 “Basi nitakuja karibu nanyi ili kuhukumu. Nami nitakuwa mwepesi kushuhudia dhidi ya wachawi, wazinzi, waapao kwa uongo, wanaopunja vibarua malipo yao, wanaowaonea wajane na yatima, na wanaowanyima wageni haki, lakini hawaniogopi mimi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And Y schal come to you in doom, and Y schal be a swift witnesse to mysdoeris, `ether enchaunteris of deuelis craft, and to auouteris, and forsworn men, and that falsli calengen the hire of the hirid man, and widewis, and fadirles, `ether modirles, children, and oppressen a pilgrym, `nether dredden me, seith the Lord of oostis.
6 “Mimi Bwana sibadiliki. Kwa hiyo ninyi, enyi uzao wa Yakobo, hamjaangamizwa.
Forsothe Y am the Lord, and am not chaungid; and ye sones of Jacob ben not wastid.
7 Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Lakini mnauliza, ‘Tutarudi kwa namna gani?’
Forsothe fro daies of youre fadris ye wenten awei fro my lawful thingis, and kepten not; turne ye ayen to me, and Y schal ayen turne to you, seith the Lord of oostis. And ye seiden, In what thing schulen we turne ayen?
8 “Je, mwanadamu atamwibia Mungu? Hata hivyo mnaniibia mimi. “Lakini mnauliza, ‘Tunakuibia kwa namna gani?’ “Mnaniibia zaka na dhabihu.
If a man schal turmente God, for ye `togidere fitchen me. And ye seiden, In what thing `togidere fitchen we thee? In tithis and in `firste fruitis;
9 Mko chini ya laana, ninyi taifa lote, kwa sababu mnaniibia mimi.
and ye ben cursid in nedynesse, and alle ye folc disseyuen me, and `togidere fitchen.
10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kuwe na chakula katika nyumba yangu. Nijaribuni katika hili,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nanyi mwone kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose nafasi ya kutosha.
Brynge ye yn ech tithe in to my berne, that mete be in myn hous, and preue ye me on this thing, seith the Lord, if Y schal not opene to you the goteris of heuene, and schal schede out to you blessyng, til to aboundaunce.
11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And Y schal blame for you that that deuourith, and he schal not distrie the fruit of youre lond; nether bareyn vyneyerd schal be in the feeld,
12 “Ndipo mataifa yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
seith the Lord of oostis, and alle folkis schulen seie you blessid; for ye schulen be a desirable lond, seith the Lord of oostis.
13 “Mmesema vitu vigumu dhidi yangu,” asema Bwana. “Hata hivyo mnauliza, ‘Tumesema nini dhidi yako?’
Youre wordis wexiden strong on me, seith the Lord; and ye seiden, What han we spokun ayens thee?
14 “Mmesema, ‘Ni bure kumtumikia Mungu. Tumepata faida gani kwa kushika maagizo yake na kwenda kama waombolezaji mbele za Bwana Mwenye Nguvu Zote?
And ye seiden, He is veyn, that serueth God; and what wynnyng for we kepten hise heestis, and for we wenten sorewful bifore the Lord of oostis?
15 Lakini sasa wenye kiburi wanabarikiwa. Hakika watenda mabaya wanastawi, pia hata wale wanaoshindana na Mungu ndio wanaosalimika.’”
Therfor now we seien proude men blessid; for thei ben bildid doynge vnpitee, and thei temptiden God, and ben maad saaf.
16 Ndipo wale waliomcha Bwana wakasemezana wao kwa wao, naye Bwana akasikiliza na akasikia. Kitabu cha kumbukumbu kikaandikwa mbele yake kuhusu wale ambao walimcha Bwana na kuliheshimu jina lake.
Thanne men dredynge God spaken, ech with his neiybore; and the Lord perseyuede, and herde, and a book of mynde is writun bifor hym to `men dredynge God, and thenkynge his name.
17 “Nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “katika siku ile nitakapowafanya watu kuwa hazina yangu. Nitawahurumia, kama vile kwa huruma mtu amhurumiavyo mwanawe anayemtumikia.
And thei schulen be to me, seith the Lord of oostis, in the dai in which Y schal make, in to a special tresour; and Y schal spare hem, as a man sparith his sone seruynge to hym.
18 Kwa mara nyingine tena utaona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia.
And ye schulen be conuertid, and ye schulen se, what is bitwixe the iust man and vnpitouse, bitwixe `the seruynge to the Lord and `not seruynge to hym.