< Malaki 3 >
1 “Angalieni, nitamtuma mjumbe wangu, atakayeiandaa njia mbele yangu. Ndipo ghafula Bwana mnayemtafuta atakuja hekaluni mwake. Mjumbe wa Agano, ambaye mnamwonea shauku, atakuja,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Behold, I will send my messenger, And he shall prepare the way before me; And the Lord, whom ye seek, shall suddenly come to his temple; And the messenger of the covenant, whom ye desire, Behold, he shall come, saith Jehovah of hosts.
2 Lakini ni nani atakayeweza kustahimili hiyo siku ya kuja kwake? Ni nani awezaye kusimama atakapotokea? Kwa kuwa atakuwa kama moto wa mfua fedha au kama sabuni ya afuaye nguo.
But who shall abide the day of his coming? And who shall stand when he appeareth? For he shall be like the fire of the refiner, And like the soap of the fuller.
3 Ataketi kama mfuaji na asafishaye fedha. Atawatakasa Walawi, naye atawasafisha kama dhahabu na fedha. Kisha Bwana atakuwa na watu watakaoleta sadaka katika haki,
And he shall sit as a refiner and purifier of silver, And he shall purify the sons of Levi, And shall refine them as gold and silver, That, being holy to Jehovah, they may bring an offering in righteousness.
4 nazo sadaka za Yuda na Yerusalemu zitakubalika kwa Bwana, kama katika siku zilizopita, kama katika miaka ya zamani.
Then shall the offering of Judah and Jerusalem be pleasing to Jehovah, As in the days of old, And as in former years.
5 “Basi nitakuja karibu nanyi ili kuhukumu. Nami nitakuwa mwepesi kushuhudia dhidi ya wachawi, wazinzi, waapao kwa uongo, wanaopunja vibarua malipo yao, wanaowaonea wajane na yatima, na wanaowanyima wageni haki, lakini hawaniogopi mimi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And I will come near to you to judgment; And I will be a swift witness Against sorcerers, and against adulterers, and against false swearers, And against those who defraud the hireling of his hire, And oppress the widow and the fatherless, And turn aside the stranger from his right, And fear not me, saith Jehovah of hosts.
6 “Mimi Bwana sibadiliki. Kwa hiyo ninyi, enyi uzao wa Yakobo, hamjaangamizwa.
For I am Jehovah; I change not; Therefore, ye sons of Jacob, are ye not consumed.
7 Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Lakini mnauliza, ‘Tutarudi kwa namna gani?’
From the days of your fathers have ye turned aside from my statutes, And have not kept them; Return to me, and I will return to you, Saith Jehovah of hosts. But ye say, “Wherein shall we return?”
8 “Je, mwanadamu atamwibia Mungu? Hata hivyo mnaniibia mimi. “Lakini mnauliza, ‘Tunakuibia kwa namna gani?’ “Mnaniibia zaka na dhabihu.
Shall a man rob God, That ye have robbed me? But ye say, “Wherein have we robbed thee?” In tithes and offerings.
9 Mko chini ya laana, ninyi taifa lote, kwa sababu mnaniibia mimi.
Ye are cursed with a curse, For ye have robbed me, even this whole nation.
10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kuwe na chakula katika nyumba yangu. Nijaribuni katika hili,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nanyi mwone kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose nafasi ya kutosha.
Bring ye all the tithes into the storehouse, That there be food in my house; And try me now in this, Saith Jehovah of hosts, Whether I will not open to you the windows of heaven, And pour out upon you a blessing, until there is none left.
11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And I will rebuke for you the devourer, And he shall not destroy the fruits of your ground, Nor shall your vine be barren in the field, Saith Jehovah of hosts.
12 “Ndipo mataifa yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And all nations shall call you blessed; For ye shall be a delightful land, Saith Jehovah of hosts.
13 “Mmesema vitu vigumu dhidi yangu,” asema Bwana. “Hata hivyo mnauliza, ‘Tumesema nini dhidi yako?’
Your words have been bold against me, saith Jehovah; Yet ye say, “What have we spoken against thee?”
14 “Mmesema, ‘Ni bure kumtumikia Mungu. Tumepata faida gani kwa kushika maagizo yake na kwenda kama waombolezaji mbele za Bwana Mwenye Nguvu Zote?
Ye have said, “It is a vain thing to serve God”; And, “What profit is it that we have kept his ordinances, And that we have walked mournfully before Jehovah of hosts?
15 Lakini sasa wenye kiburi wanabarikiwa. Hakika watenda mabaya wanastawi, pia hata wale wanaoshindana na Mungu ndio wanaosalimika.’”
Therefore we call the proud happy; Yea, they that do wickedness are built up; Yea, they tempt God, and are delivered.”
16 Ndipo wale waliomcha Bwana wakasemezana wao kwa wao, naye Bwana akasikiliza na akasikia. Kitabu cha kumbukumbu kikaandikwa mbele yake kuhusu wale ambao walimcha Bwana na kuliheshimu jina lake.
Then they that feared Jehovah spake to one another, And Jehovah gave ear and heard; And a book of remembrance was written before him, For them that feared Jehovah, And that thought upon his name.
17 “Nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “katika siku ile nitakapowafanya watu kuwa hazina yangu. Nitawahurumia, kama vile kwa huruma mtu amhurumiavyo mwanawe anayemtumikia.
And they shall be to me, saith Jehovah of hosts, In the day which I appoint, as my own possession; And I will spare them, As a father spareth his own son that serveth him.
18 Kwa mara nyingine tena utaona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia.
Then shall ye return and see What is the difference between the righteous and the wicked, Between him who serveth God And him who serveth him not.