< Malaki 3 >

1 “Angalieni, nitamtuma mjumbe wangu, atakayeiandaa njia mbele yangu. Ndipo ghafula Bwana mnayemtafuta atakuja hekaluni mwake. Mjumbe wa Agano, ambaye mnamwonea shauku, atakuja,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Behold, I send my agent, and he shall prepare the way before me. And the Lord, whom ye seek, will suddenly come to his temple. And the messenger of the covenant, whom ye desire, behold, he comes, says Jehovah of hosts.
2 Lakini ni nani atakayeweza kustahimili hiyo siku ya kuja kwake? Ni nani awezaye kusimama atakapotokea? Kwa kuwa atakuwa kama moto wa mfua fedha au kama sabuni ya afuaye nguo.
But who can abide the day of his coming? And who shall stand when he appears? For he is like a refiner's fire, and like fuller's soap.
3 Ataketi kama mfuaji na asafishaye fedha. Atawatakasa Walawi, naye atawasafisha kama dhahabu na fedha. Kisha Bwana atakuwa na watu watakaoleta sadaka katika haki,
And he will sit as a refiner and purifier of silver. And he will purify the sons of Levi, and refine them as gold and silver. And they shall offer to Jehovah offerings in righteousness.
4 nazo sadaka za Yuda na Yerusalemu zitakubalika kwa Bwana, kama katika siku zilizopita, kama katika miaka ya zamani.
Then the offering of Judah and Jerusalem shall be pleasant to Jehovah, as in the days of old, and as in ancient years.
5 “Basi nitakuja karibu nanyi ili kuhukumu. Nami nitakuwa mwepesi kushuhudia dhidi ya wachawi, wazinzi, waapao kwa uongo, wanaopunja vibarua malipo yao, wanaowaonea wajane na yatima, na wanaowanyima wageni haki, lakini hawaniogopi mimi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And I will come near to you to judgment, and I will be a swift witness against the sorcerers, and against the adulterers, and against the false swearers, and against those who oppress the hireling in his wages, the widow, and the fatherless, and who turn aside the sojourner, and do not fear me, says Jehovah of hosts.
6 “Mimi Bwana sibadiliki. Kwa hiyo ninyi, enyi uzao wa Yakobo, hamjaangamizwa.
For I, Jehovah, do not change. Therefore ye, O sons of Jacob, are not consumed.
7 Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Lakini mnauliza, ‘Tutarudi kwa namna gani?’
From the days of your fathers ye have turned aside from my ordinances, and have not kept them. Return to me, and I will return to you, says Jehovah of hosts. But ye say, How shall we return?
8 “Je, mwanadamu atamwibia Mungu? Hata hivyo mnaniibia mimi. “Lakini mnauliza, ‘Tunakuibia kwa namna gani?’ “Mnaniibia zaka na dhabihu.
Will a man rob God? Yet ye rob me. But ye say, How have we robbed thee? In tithes and offerings.
9 Mko chini ya laana, ninyi taifa lote, kwa sababu mnaniibia mimi.
Ye are cursed with the curse, for ye rob me, even this whole nation.
10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kuwe na chakula katika nyumba yangu. Nijaribuni katika hili,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nanyi mwone kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose nafasi ya kutosha.
Bring ye the whole tithe into the storehouse, that there may be food in my house, and prove me now with this, says Jehovah of hosts, if I will not open to you the windows of heaven, and pour you out a blessing, that there shall not be room enough for it.
11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And I will rebuke the devourer for your sakes, and he shall not destroy the fruits of your ground, nor shall your vine cast its fruit before the time in the field, says Jehovah of hosts.
12 “Ndipo mataifa yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And all nations shall call you blessed, for ye shall be a delightful land, says Jehovah of hosts.
13 “Mmesema vitu vigumu dhidi yangu,” asema Bwana. “Hata hivyo mnauliza, ‘Tumesema nini dhidi yako?’
Your words have been stout against me, says Jehovah. Yet ye say, What have we spoken against thee?
14 “Mmesema, ‘Ni bure kumtumikia Mungu. Tumepata faida gani kwa kushika maagizo yake na kwenda kama waombolezaji mbele za Bwana Mwenye Nguvu Zote?
Ye have said, It is vain to serve God, and what profit is it that we have kept his charge, and that we have walked mournfully before Jehovah of hosts?
15 Lakini sasa wenye kiburi wanabarikiwa. Hakika watenda mabaya wanastawi, pia hata wale wanaoshindana na Mungu ndio wanaosalimika.’”
And now we call the proud happy. Yea, those who work wickedness are built up. Yea, they challenge God, and escape.
16 Ndipo wale waliomcha Bwana wakasemezana wao kwa wao, naye Bwana akasikiliza na akasikia. Kitabu cha kumbukumbu kikaandikwa mbele yake kuhusu wale ambao walimcha Bwana na kuliheshimu jina lake.
Then those who feared Jehovah spoke one with another, and Jehovah hearkened, and heard, and a book of remembrance was written before him, for those who feared Jehovah, and who thought upon his name.
17 “Nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “katika siku ile nitakapowafanya watu kuwa hazina yangu. Nitawahurumia, kama vile kwa huruma mtu amhurumiavyo mwanawe anayemtumikia.
And they shall be mine, says Jehovah of hosts, my own possession, in the day that I make. And I will spare them, as a man spares his own son who serves him.
18 Kwa mara nyingine tena utaona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia.
Then ye shall return and discern between the righteous man and the wicked man, between him who serves God and him who does not serve him.

< Malaki 3 >