< Malaki 2 >

1 “Sasa onyo hili ni kwa ajili yenu, enyi makuhani.
« Maintenant, vous, prêtres, ce commandement est pour vous.
2 Kama hamtasikiliza, na kama hamtaki kuielekeza mioyo yenu kuheshimu Jina langu, nitatuma laana juu yenu, nami nitalaani baraka zenu. Naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamkuielekeza mioyo yenu kuniheshimu mimi,” Asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Si vous n'écoutez pas, si vous ne prenez pas à cœur de glorifier mon nom, dit Yahvé des Armées, alors j'enverrai la malédiction sur vous, et je maudirai vos bénédictions. Je les ai déjà maudits, parce que vous ne prenez pas cela à cœur.
3 “Kwa sababu yenu nitawakatilia mbali wazao wenu. Nitazipaka nyuso zenu mavi, mavi ya dhabihu zenu. Nanyi mtafukuzwa pamoja nazo mtoke mbele zangu.
Voici, je réprimanderai vos descendants, je répandrai sur vos visages du fumier, le fumier de vos fêtes, et vous en serez emportés.
4 Nanyi mtajua kuwa nimewapelekea onyo hili ili kwamba Agano langu na Lawi lipate kuendelea,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Vous saurez que je vous ai envoyé ce commandement, afin que mon alliance soit avec Lévi, dit l'Éternel des armées.
5 “Agano langu lilikuwa pamoja naye, agano la uhai na amani, nami nilimpa yote, ili aniche na kuniheshimu, naye akaniheshimu na kusimama akilicha Jina langu.
« Mon alliance avec lui était la vie et la paix; je les lui ai données pour qu'il me respecte; et il m'a respecté et a craint mon nom.
6 Fundisho la kweli lilikuwa kinywani mwake, wala hakuna uongo wowote uliopatikana katika midomo yake. Alitembea nami katika amani na unyofu, naye akawageuza wengi kutoka dhambini.
La loi de la vérité était dans sa bouche, et l'iniquité ne se trouvait pas sur ses lèvres. Il a marché avec moi dans la paix et la droiture, et il a détourné beaucoup de gens de l'iniquité.
7 “Kwa maana yapasa midomo ya kuhani kuhifadhi maarifa. Tena kutoka kinywani mwake watu wangepaswa kutafuta mafundisho, kwa sababu yeye ni mjumbe wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Car les lèvres du prêtre doivent garder la connaissance, et on doit chercher la loi à sa bouche, car il est le messager de l'Éternel des armées.
8 Lakini mmegeuka mkaiacha njia, na kwa mafundisho yenu mmesababisha wengi kujikwaa. Mmevunja agano na Lawi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Mais vous vous êtes détournés du chemin. Tu as fait trébucher beaucoup de gens dans la loi. Tu as corrompu l'alliance de Lévi, dit l'Éternel des armées.
9 “Kwa hiyo nimewasababisha ninyi kudharauliwa na kufedheheshwa mbele ya watu wote, kwa sababu hamkufuata njia zangu, bali mmeonyesha upendeleo katika mambo ya sheria.”
« C'est pourquoi je t'ai aussi rendu méprisable et méchant devant tout le peuple, selon que tu n'as pas gardé mes voies, mais que tu as respecté des personnes dans la loi.
10 Je, sote hatuna Baba mmoja? Hatukuumbwa na Mungu mmoja? Kwa nini basi tunalinajisi Agano la baba zetu kwa kukosa uaminifu kila mmoja kwa mwenzake?
N'avons-nous pas tous un seul père? N'avons-nous pas été créés par un seul Dieu? Pourquoi sommes-nous perfides, chacun contre son frère, et profanons-nous l'alliance de nos pères?
11 Yuda amevunja uaminifu. Jambo la kuchukiza limetendeka katika Israeli na katika Yerusalemu: Yuda amepanajisi mahali patakatifu apendapo Bwana, kwa kuoa binti wa mungu mgeni.
Juda a agi en traître, et une abomination a été commise en Israël et à Jérusalem; car Juda a profané la sainteté de l'Éternel qu'il aime, et il a épousé la fille d'un dieu étranger.
12 Kwa maana kwa mtu yeyote atendaye jambo hili, Bwana na amkatilie mbali kutoka hema za Yakobo, hata kama huwa anamletea Bwana Mwenye Nguvu Zote sadaka.
Yahvé retranchera l'homme qui fait cela, celui qui se réveille et celui qui répond, des tentes de Jacob et de celui qui présente une offrande à Yahvé des armées.
13 Kitu kingine mnachokifanya: Mnaifurikisha madhabahu ya Bwana kwa machozi. Mnalia na kuugua kwa sababu yeye haziangalii tena sadaka zenu wala hazikubali kwa furaha kutoka mikononi mwenu.
« Voici ce que vous faites encore: vous couvrez l'autel de Yahvé de larmes, de pleurs et de soupirs, parce qu'il n'a plus égard à l'offrande et qu'il ne la reçoit pas de votre main avec bienveillance.
14 Mnauliza, “Kwa nini?” Ni kwa sababu Bwana ni shahidi kati yako na mke wa ujana wako, kwa sababu umevunja uaminifu naye, ingawa yeye ni mwenzako, mke wa agano lako la ndoa.
Et tu dis: « Pourquoi? » Parce que l'Éternel a été témoin entre toi et la femme de ta jeunesse, contre laquelle tu as été infidèle, alors qu'elle était ta compagne et la femme de ton alliance.
15 Je, Bwana hakuwafanya wao kuwa mmoja? Katika mwili na katika roho wao ni wa Mungu. Kwa nini wawe mmoja? Kwa sababu Mungu alikuwa akitafuta mzao mwenye kumcha Mungu. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, mtu asivunje uaminifu kwa mke wa ujana wake.
N'a-t-il pas fait de vous un seul être, alors qu'il avait le résidu de l'Esprit? Pourquoi un seul? Il cherchait une descendance pieuse. Prends donc garde à ton esprit, et que personne ne soit infidèle à la femme de sa jeunesse.
16 “Ninachukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli, “pia nachukia mtu anayejivika jeuri kama vazi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, wala msije mkavunja uaminifu.
Celui qui hait et répudie, dit Yahvé, le Dieu d'Israël, couvre son vêtement de violence, dit Yahvé des armées. « Fais donc attention à ton esprit, afin de ne pas être infidèle.
17 Mmemchosha Bwana kwa maneno yenu. Nanyi mnauliza, “Tumemchosha kwa namna gani?” Mmemchosha kwa kusema, “Wote watendao mabaya ni wema machoni pa Bwana, naye anapendezwa nao” au “Mungu wa haki yuko wapi?”
Vous avez fatigué l'Éternel par vos paroles. Et vous dites: Comment l'avons-nous fatigué? Vous dites: « Tous ceux qui font le mal sont bons aux yeux de l'Éternel, et il s'en réjouit », ou bien: « Où est le Dieu de la justice? ».

< Malaki 2 >