< Malaki 1 >

1 Ujumbe: Neno la Bwana kwa Israeli kupitia kwa Malaki.
The prophecy of the word of Jehovah, concerning Israel, by Malachi.
2 Bwana asema, “Nimewapenda ninyi.” “Lakini ninyi mnauliza, ‘Wewe umetupendaje?’” Bwana asema, “Je, Esau hakuwa ndugu yake Yakobo? Hata hivyo nimempenda Yakobo,
I have loved you, saith Jehovah. But ye say, “Wherein hast thou loved us?” Was not Esau Jacob's brother, saith Jehovah? Yet I loved Jacob,
3 lakini nikamchukia Esau, nami nimeifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa jangwani.”
And Esau I hated; And I made his mountains a desolation, And his inheritance to be habitations of the desert.
4 Edomu anaweza kusema, “Ingawa tumepondapondwa, tutajenga upya magofu.” Lakini hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Wanaweza kujenga, lakini nitabomoa. Wataitwa Nchi Ovu, watu ambao siku zote wapo chini ya ghadhabu ya Bwana.
Although Edom say, “We are ruined, Yet will we build again the desolate places.” Thus saith Jehovah of hosts: They may build, but I will throw down; And men shall call them “The impious land, The people against whom Jehovah hath indignation forever.”
5 Mtayaona kwa macho yenu wenyewe na kusema, ‘Bwana ni mkuu, hata nje ya mipaka ya Israeli!’
And your eyes shall see it, and ye shall say, “Great is Jehovah beyond the borders of Israel!”
6 “Mwana humheshimu baba yake, naye mtumishi humheshimu bwana wake. Kama mimi ni baba, iko wapi heshima ninayostahili? Kama mimi ni bwana, iko wapi heshima ninayostahili?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau Jina langu. “Lakini mnauliza, ‘Tumelidharau Jina lako kwa namna gani?’
A son honoreth his father, And a servant his master; If I, then, be a father, where is mine honor? And if I be a master, where is my fear? Saith Jehovah of hosts to you, ye priests that despise my name. Ye say, “Wherein do we despise thy name?”
7 “Mnatoa sadaka chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu. “Lakini ninyi mnauliza, ‘Tumekutia unajisi kwa namna gani?’ “Kwa kusema kuwa meza ya Bwana ni ya kudharauliwa.
Ye bring polluted food to mine altar. And ye say, “Wherein do we pollute thee?” In that ye say, “The table of Jehovah is contemptible.”
8 Wakati mletapo dhabihu za wanyama walio vipofu, je, hilo si kosa? Mnapoleta dhabihu zilizo vilema au wanyama wagonjwa, je, hilo si kosa? Jaribuni kuvitoa kwa mtawala wenu! Je, angefurahishwa nanyi? Je, atawakubalia?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
For when ye bring the blind for sacrifice, [[ye say, ]] “It is not evil.” And when ye offer the lame and the sick, [[Ye say, ]] “It is not evil.” Offer it, then, to thy governor; Will he be pleased with thee, Or have regard to thee? Saith Jehovah of hosts.
9 “Basi mwombeni Mungu awe na neema kwetu. Je, kwa sadaka kama hizo kutoka mikononi mwenu, atawapokea?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And now, I pray you, beseech God to be gracious unto us! Since such things are done by you, Will he have regard to you, Saith Jehovah of hosts?
10 “Laiti mmoja wenu angalifunga milango ya Hekalu, ili msije mkawasha moto usiokuwa na faida juu ya madhabahu yangu! Sina furaha nanyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nami sitaikubali sadaka toka mikononi mwenu.
O that some one of you would close the doors, That ye might not kindle the fire upon mine altar in vain! I have no pleasure in you, saith Jehovah of hosts, Neither will I accept an offering at your hand.
11 Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa, kuanzia mawio ya jua hata machweo yake. Kila mahali uvumba na sadaka safi zitaletwa kwa Jina langu, kwa sababu Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
For from the rising of the sun even to the going down of the same My name shall be great among the nations. And in every place shall incense be offered to my name, And a pure offering; For my name shall be great among the nations, Saith Jehovah of hosts.
12 “Lakini mnalinajisi Jina langu kwa kusema kuhusu meza ya Bwana, ‘Imetiwa unajisi pamoja na chakula chake. Ni ya kudharauliwa.’
But ye profane it, In that ye say, “The table of Jehovah is polluted, And what is offered thereon, even its food, is contemptible.”
13 Nanyi mnasema, ‘Mzigo gani huu!’ Nanyi mnaidharau kwa kiburi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Wakati mnapowaleta wanyama mliopokonya kwa nguvu, walio vilema au walio wagonjwa na kuwatoa kama dhabihu, je, niwakubali kutoka mikononi mwenu?” asema Bwana.
Ye say also, “Behold, what weariness!” And ye snuff at it, Saith Jehovah of hosts; And ye bring that which is plundered, and lame, and sick, And present it for an offering; Shall I accept it at your hand? Saith Jehovah.
14 “Amelaaniwa yeye adanganyaye, aliye na mnyama wa kiume anayekubalika katika kundi lake na kuweka nadhiri ya kumtoa, lakini akatoa dhabihu ya mnyama aliye na dosari kwa Bwana. Kwa kuwa mimi ni Mfalme Mkuu, nalo Jina langu linapaswa kuogopwa miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Cursed be the deceiver, Who hath in his flock a male, And yet voweth and sacrificeth to Jehovah that which is marred; For I am a great king, saith Jehovah of hosts; And my name is terrible among the nations.

< Malaki 1 >