< Luka 1 >
1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
kulyuve mwoghopua Tiofilo avaanhu vinga valembile imhola isa Yesu Kilisite ndavule silyavombike kulyusue.
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
valembile imhola isi ndavule tulyapangilue na vano valyalolile na maaso ghave, navano valyasipulisie kuhuma vuvutengulilo vwake.
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
ulwakuva nilondile vunono uvwakyang'haani vwa mhola sa Yesu vuhuma vuvutengulilo lino najune nivwene lunono kukulembela isi sooni muvutavike.
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
neke ulukagule ulwakyang'haani lwa mbombo sino ukavulanisivue.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
mu fighono fya Helode untwa ghwa Yudea, pwealyale untekesi jumonga juno alyale ikemelua Sakalia ughwa lukolo lwa Abia un'dala ghwake alyahumile muvaliive va Haluni, ni litavua lyake alyale ikemelua Elisabeti.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
voni van valyale vagholofu pa maaso gha Nguluve amaghendele ghale ghasita kukuvapika mundaghilo sooni munjovele ja Mutwa.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
neke navalyale nu mwana ulwakuva uElisabeti alyale mughumba na kukavalilo akuo voni vale vaghogholofijo.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
lino lulyahumile kuuti uSakalia alyale nu Mhepo umwimike kuvutavike vwa Nguluve. akalutile nuvutavike vwa vutekesi kuhumila mu vutavike vwa ludimo lwake.
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
kwevulyale uvutavike uvwa kuvomba mu nyumba ja Nguluve veni umuunhu untekesi, veni idalikila akasalulua ikipugha akingila mu nhumba ja Mutwa akanyanya uvufumba.
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
ilipugha lyoni lya vaanhu vakava vikufunya kunji ye vinyanya uvusumba.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
unyaMhola ghwa Mutwa akamwumila na kukwiima ulubale lwa luvoko lwa ndia kufitekelelo kuno vinyanyila uvusumba.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
uSakalia akoghopa ye alwaghile ulutetemo lulyamughwila.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
neke unyaMhola akam'bula kuuti, ulekaghe pikwoghopa Sakalia ulwakuva ulufunyo lwako lupulikike. undala ghwako uElisabeti ikukuholela umwana ilitavua lyake ghukun'kemela Yohani.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
ghuliva nu lukelo na kuhovoka, na vinga vikuhovokela kuholua kwa mwene.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
ulwakuva iliva nu vuvaha kuhuma kwa Mutwa ujuo nanganyisaghe nambe kimonga kino kighasia. looli ingufu sa Mhepo umwimike siiva nu mwene kuhuma pano ali mulileme lwa ng'iina.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
na vaanhu vinga ava Silaeli ilikuvagomosiagha kwa Nguluve uMutwa ghwave.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
ujuo ilikumulongolela uMutwa mu ngufu nu mwojo ndavule alyale uEliya kusambania mu ngufu sa Mhepo uMwimike neve vano navikumwoghopa vighendagha muluhala lwa vano valweli. ikuvavombela ndiki kukuvavika kwa Mutwa avaanhu vano vaghelanisivue vwimila jake.
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
uSakalia akam'bula unyaMhola, “niwesia ndani kukagula ili? ulwakuva une nili nsehe nu n'dala ghwango na maka ghake ghali minga kyongo”.
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
unyaMhola akamwamula na kumb'ula, une nene Gabilieli, nejuno nikwima pavulongolo pa Nguluve. nisung'ilue kukuvuula, kukuletela iMhola inofu iji.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
kange lolagha, nungajove kinu ghuva kimie nungawesie kujova kuhanga ikighono kila pano isi siva sihumile. ulu lwe ulwakuva ukakunilue kukwitika amasio ghango ghano mu nsiki ghiva ghavombike.
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
lino avaanhu valyale vikumughula uSakalia. valyadeghile kuuti alyale itumila unsiki mwinga ku nyumba inyimike ja kufunyila.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
neke ye ahumile kunji, akakunilue kujova navo. pe aveene vakakagula kuuti, luvonike lumonga mu nyuma inyimike neke umwene akava ihufia lumonga na mavoko. akajigha kinunu.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
ye fisilile ifighono fyakuvomba imbombo jakilekesi ayavukile kugomoka kunyumba jake.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
pambele uSakalia akavuja kukaja kuhuma ku mbombo sake sakitekesi un'dala ghwake akava n'kunue, akifisa amesi ghahaano akajova.
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
“ulwakuva lwe luno uMutwa ambombile une ye andolile kulughano lwoni kukumbusikisia isoni pa maaso gha vaanhu”
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
ye ghufikile umwesi ghwa n'tanda pavukunue vwa Elisabeti uNguluve akatuma unyaMhola uGabilieli kuluta mu iisi ja Galilaya ilitavua ilinge Nasaleti,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
kwa mhinja juno akatambulwagha Maliya. kwa mhinja juno alyatunilue nu mughosi ilitavua lyake ghwe Yosefu. umuholua mukikolo kya Davidi nilitavua lya mhinja akakemeluagha ghwe Maliya.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
unyaMhola ye afikile akati, “nikukuhungila uve ghwe juno usungukilue nu Mutwa, uMutwa alinuve;
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
amasio ghanyaMhola ghaka mangajisia kyongo mu mwojo ghwake na alyaghamanyile kiki unyaMhola ihungila hungila iji kidegho.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
unyaMhola akam'bula “nungoghopaghe Maliya ulwakuva uNguluve akusungukile.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
lolagha ghuva nu vukunue, ghupapagha umwana neke ghukun'kemelagha ilitavua ghwe Yesu.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
iliva m'baha ikemeluagha mwana ghwa juno alikukyanya kyongo, uMutwa uNguluve neke ikumpelagha ikitengo kya vutwa kya Davidi uvuse.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
itemagha uvutwa mu lukolo lwa Yakovo uvusila nakusila lusiku. (aiōn )
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
uMaliya akam'bula unyaMhola ili, iva ndani ulwakuva une nanighelile kuvwafuka nu mughosi ghwoghwoni?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
unyamhola akamwamula akam'bula “uMhepo uMwimike ikwisa kulyuve. ni ngufu sa juno alikukyanya kyongo sikwisa kulyuve. pe lino umwimike juno iholua ikemeluagha mwana ghwa Nguluve.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
lolagha ulukololuo uElisabeti alinuukunue vwa mwana mufighono fyake fya vughogholo, ughu ghwe mwesi ghwa n'tanda juno valyatile mughumba.
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
ulwakuva kwa Nguluve nakwekili kino kimuulemile”
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
uMaliya akajova akati, une nilim'baanda ghwa Mutwa neke luuleke luve luve kulyune ndavule ujovile” pe pano unyaMhola akavuka iluta.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
ye fikikile ifighono nde filingi uMaliya avuka ng'haning'habi na kuluta ku iisi jimonga jino jale nyafidunda, ija Yudea.
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
ukuo akingila mu nyumba ija Sakalia na kumwungila uElisabeti,
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
lino pe lulyahumile kuuti,” uElisabeti ye apulike uluhungilo lwa Maliya. umwana mu lileme akaomoka tomoka, neke uElisabeti ingufu isa Mhepo uMwimike sikamwisila.
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
pe akatengula pijova kungufu akati, “ufunyilue uve mukighavo kya vakijuuva najumwana juno alimulileme lyako afunyilue.
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
neke lulindani kulyune ungiina ghwa Mutwa lunoghile pikwisa kulyune?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
ulwakuva lolagha ye lupulikike mu mbughulutu sango ilisio lya kuhungila kulyuve umwana mulileme lyango atomwike nu lukelo.
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
neke afunyilue umukijuva jula juno alyitike kuuti vulyahumila uvya kyang'haani vwa sino alyavulilue kuhuma kwa Mutwa”.
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
uMaliya akati, inimbula jango jikunfunya uMutwa,
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
naghumwojo ghwango ghuvovwike mwa Nguluve umpoki ghwango.
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
ulwakuva avulolile uvukotofu vwa m'banda ghwake umhinja. lolagha kuhuma mu fisina fyoni vikughonelagha nilifunyua.
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
ulwakuva umwene unya sooni avombile sino mbaha kylyune. ni litavua lyake ilyimike.
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
uvukola vwake kuhuma ikisina ni kisina ku vano vikumwopa umwene.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
avonisie ingufu mu luvoko lyake avapalanisie vala vano vakighiniagha mu masaghe gha mooja ghave.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
avisisie paasi avana va vatwa kuhuma mufitengo fyave ifya vutwa na kukuvatosia kukyanya vano vakotofu.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
alyavapelile avanya njala ifinu ifi nono looli avamofu avadagile na mavoko gheene.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
ahumisie uvutangilisi kwa Isilaeli um'bombi ghake, neke akumuke kuvonesia uvuhugu.
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
(ndavule alyajovile kuvanhaata vitu) kwa Abulahamu ni fisina fyake kuvusila na kusila” (aiōn )
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
uMalia alikalile nu Elisabeti hwene mesi ghatatu pepano akagomoka ku nyumba ja mwene.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
lino unsiki ghulyafikile ughwa Elisabeti kupaapa umwana un'dimi.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
avabading'ani vake na vanyalukolo vake valyapulike ndavule uMutwa atupelanisie mu vuhugu vwake, kange vakahovoka palikimo nu mwene.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
lino kilyahumile ikighono kya lekela kwoni valisile kukivungo najumwana lulyanoghile vampele ilitavua lyake ghwe Sakalia kulwiho lwa vise.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
looli ung'ina akamula akati, “ndali” ikemelua ghwe Yohani”
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
vakam'bula napwale nambe jumo mulukolo juno itambulua ku litavua ili”
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
pe vakam'bombela ikimanyilo uvise kuuti, umwene iti ilitavua akemelue veni.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
uvise akalonda ikisegho akalemba “ilitavua ghwe Yohani” voni vakadegha ku ili
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
ku kenyemukila umulomo ghake ghukadinduka nu lumili lwake lukava vuleka akajova na kukumughinia uNguluve
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
uludwesi lukavisila voni vano valikalile pipi navoimbombo isio sikakwilana mu iisi jooni ja fidunda fya Yudea,
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
na voni vano valyaghapulike vakaghagadilila mu mwoojo ghave, vakati umwana uju ghwa ndani ndani?” ulwakuva uluvoko lwa Mutwa lulyale palikimo naghwo.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
ivise ghwa Sakalia akapeluula ingufu nu Mhepo uMwimike akatengula kuhumia uvuvili akatisagha,
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
aghinwaghe uMutwa, uNguluve ghwa Isilaeli, ulwakuva atangile kange na kukuvavanga avaanhu vake.
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
atupelile uvupoki kuhuma mu nyumba ja nyambombo ghwake u Davidi, kuhuma mukikolo kya m'bombi ghwake uDavidi.
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
ndavule alyajovile mumulomo ghwa vavili vake vano kwevalyale kuhuma kuvukuulu. (aiōn )
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
alatupoka kuhuma kuvalugu viitu na kuhuma mumavoko ghavaanhu vooni vano vikutukalalila.
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
alavomba ndiki kuvonesia ulusungu kuvanhaata vitu na kukumbuka ululaghilo lwake ulwimike.
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
ulujigho luno alayjovile kwa Abulahamu unhaata ghwitu.
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
alyajighile na kunkangasia kuuti lunoghile pikum'bombela umwene kisila vwoghofi pano tupokilue pihuma mumavoko ghavalugu viitu.
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
muvwimike na muvagholofu uvwakyang'haani pa maaso ghake ni fighono fyake fyoni.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
Ena, najuve mwana ghukemeluagha uli mb'ili ghw ajuno ali kukyanya fiijo ulwakuva alyaghendelelagha ku maaso ghwa Mutwa kuuti ikuvavonesia isila. neke kukunosekesia isila avaanhu pano ikwisagha umwene.
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
kukuvavula avaanhu vake kuuti valapyanilwagha valavuvunagha uvupoki kusila kusila ja vupoki vwa nyfi saave.
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
ili lilyahumile ulwakuva ja lusungu lwa Nguluve ghwitu ulwakuva ilijuva kuhuma kukyanya likutwisila.
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
kukutumulikila ku vano vikalile mu ng'isi nu lumwighighi ghwa vafue alavomba ndiki kulongosia amaghulu ghitu kusila ja lutengano.”
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
lino umwana jula akakula na kuva nyangufu mwa Mhepo uMwimike. alikalile kulihaka kuhanga unsiki ghuno akavonekagha ku vaSilaeli.