< Luka 1 >
1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
Bonchcho Tewofiloosa, nu giddon polettidabas daroti, banttaw dandda7ettida mela xaafidosona.
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
He taarikiya entti xaafiday koyroppe doomidi ayfe markkatinne qaala haggaazeyssati nuus odidayssa.
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
Takka ta baggara koyroppe akeeka xeellidaappe guye, he taarikiya hanotaa maarayada new xaafoy taw lo77o gidi benttis.
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
Hessika, ne tamaaridabay tuma gideyssa erisanaassa.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
Yihuda kawuwa Heroodisa wode Abbaya yaraappe gidida Zakkariyaasa giya Ayhude kahiney de7ees. Iya machchiyaka Aarona sheeshaappe. I sunthaykka Elsabeexo.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
Nam77ayka Godaa woganne kiita ubbaa naagidi borey baynna Xoossaa sinthan xillotethan de7idosona.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
Hanoppe attin Elsabeexa maynthi gidida gisho enttaw na7i baawa. Nam77ayka qassi cimidosona.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
Issi gallas Zakkariyaasi ba gishuwa maaran Xoossaa sinthan kahinetethan haggaazees.
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
Kahinetetha wogan Xoossa Keethi gelidi ixaane cuyisanaw iya saami gakkis.
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
Ixaaney cuya wode asay karen woossees.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
Godaa kiitanchchoy yarshshuwa yarshshiya bessaafe ushachcha baggara eqqidi benttis.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
Zakkariyaasi iya be7ida wode dagammidi daro yayyis.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
Shin kiitanchchoy iyaakko, “Zakkariyaasa yayyofa; ne woosay si7ettis. Ne machchiya Elsabeexa adde na7a yelana, iya Yohaannisa gada ne sunthana.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
I new injjenne ufayssi gidana; daroti iya yeletethan ufayttana.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
Godaa sinthan I gita gidana woyne ushshaa gidin hara mathoya ushshaa uyenna. Ba aaye ulon de7ishe Geeshsha Ayyaanan kumana.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
Isra7eele asatappe darota bantta Godaa, Xoossaakko zaarana.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
Aawata wozana naytakko zaarana, kiitettonayssata xillota cinccatethaako zaarana mela, Godaas bessiya dere giigisanaw Eliyaasa ayyaananinne wolqqan Godaa sinthan baana” yaagis.
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
Zakkariyaasi kiitanchchuwako, “Ta hessa aybin eranee? Taaranne ta machcheera cimida” yaagis.
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
Kiitanchchoy zaaridi, “Taani Xoossaa sinthan eqqiya Gabreele. Ha mishirachchuwa new odanaw Xoossaafe kiitetas.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
Hekko, wodiya naagidi polettiya ta qaala ne ammanonna ixxida gisho, hayssi polettana gakkanaw neeni muume gidana, odettanawukka dandda7akka” yaagis.
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
He wode Zakkariyaasi Xoossa Keethi gelidi gam77ida gisho, aybi hanide gidi asay karen naagishe gam77is.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
I kare keyidi enttana odisanaw dandda7ibeenna. Malli besoppe attin odettanaw dandda7onayssa be7ida wode qonccethi be7idayssa eridosona.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
Zakkariyaasi ba haggazuwa polidi soo simmis.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
Hessafe guye, iya machchiya Elsabeexa qanthatasu. Ichchashu ageena kumethi bana geenthada gam77asu.
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
Iya, “Goday ba maarotan ta boriya asaa giddofe digganaw be7idi ha wodiyan hayssa oothis” yaagasu.
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
Elsabeexa qanthatin usuppuntha ageenan, Xoossay kiitanchchuwa Gabreele Galiila biittan de7iya Naazirete katamaa kiittis.
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
Kawuwa Dawite sheeshaappe gidida Yoosefa giya uraas oyshettida geela7eekko kiittis. He geela7iya Mayraamo geetettawusu.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
Kiitanchchoy iikko bidi, “Daro dosettidare, saroy new gido, Xoossay neera de7ees” yaagis.
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
Mayraama iya odan daro dagammada, “Hayssi aybi sarotho” gada heetasu.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
Kiitanchchoy zaaridi, “Mayraame babbofa; neeni Xoossaa sinthan saba demmadasa.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
Hekko neeni qanthatana adde na7a yelana, iya sunthaaka Yesuusa gada sunthana.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
I gita gidana, Ubbaafe Bolla Xoossaa na7aa geetetti xeegettana. Godaa Xoossay iya aawa Dawite araata iyaw immana.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
I Yayqooba sheeshaa bolla merinaw kawotana; iya kawotethaas zawi baawa” yaagis. (aiōn )
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Mayraama kiitanchchuwako, “Hessi waanidi hananee? Ta adde erikke” yaagasu.
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
Kiitanchchoy zaaridi, “Geeshsha Ayyaanay ne bolla wodhdhana, Ubbaafe Bolla Xoossaa wolqqay ne bolla kuyattana. Hessa gisho, yelettiya geeshsha na7ay Xoossaa Na7aa geetettana.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
Hekko, ne dabbiya Elsabeexa ba cimatetha laythan adde na7a qanthatasu. Iya maynthi geetettidaaro, shin ha77i usuppuntha ageena oykkasu.
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
Xoossaa xooniyabay baawa” yaagis.
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
Mayraama, “Hekko, taani Godaa aylliw, ne qaalada taw hano” yaagasu. Hessafe guye, kiitanchchoy iippe shaakettis.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
Mayraama he saaminttan denddada Yihuda biittan de7iya issi geze katama basu.
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
Zakkariyaasa soo gelada Elsabeexo sarothasu.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
Elsabeexa Mayraami sarothuwa si7ida wode I uluwan de7iya na7ay ufayssan guppis. Elsabeexa Geeshsha Ayyaanan kumada,
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
ba qaala dhoqqu oothada, “Neeni maccasaa giddofe anjjettidaaro, ne qanthatida na7aykka anjjettidayssa.
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
Hanoshin, ta Godaa aaye, neeni taakko yaana mela taani oonee?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
Hekko ne sarothuwa ta si7ida wode ta uluwan de7iya na7ay ufayssan guppis.
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
Goday polana gidi immida qaala ammanidaara, iya anjjettidaaro” yaagasu.
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
Mayraama hayssada yaagasu: “Ta shemppiya Godaa bonchchawusu,
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
ta Ayyaanay dhaliya Xoossan ufayttees.
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
I ba aylle kawushshatethaa be7is. Hachchife doomidi yeletethi ubbay tana anjjettidaaro gaana.
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
Ays giikko, wolqqaama gidida I, taw gitabaa oothis. Iya sunthay Geeshshaa.
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
Iya bonchcheyssata bolla, iya maarotethay merinaappe merinaa gakkanaassa.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
Ba qesiyan minobaa oothis, bantta wozanan otortteyssata laallis.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
Wolqqaama kawota araataappe kawushshis; banttana kawushshidayssata kabboys.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
Koshattidayssata lo77oban kalssis, shin dureta mela kushe yeddis.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
Ba maarota qoppidi, Ba aylliya Isra7eele maaddis.
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
Hessika nu aawatas odida qaalaa, Abrahamesinne iya sheeshas gidayssa merinaw polanaassa” yaagasu. (aiōn )
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
Mayraama Elsabeexi matan heedzu ageena mela gam77ada ba soo simmasu.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Elsabeexis yelo qammay gakkin adde na7a yelasu.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
I shoorotinne I dabboti Goday gita maarota oothidayssa si7idi, iira issife ufayttidosona.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
Hosppuntha gallasan yooga na7a qaxxaranaw yidosona. Iya aawa sunthan Zakkariyaasa gidi sunthanaw koyidosona.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
Shin aayiya, “Akkay, Yohaannisa geetettanaw bessees” yaagasu.
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
Enttika, “Ne dabbotappe ha sunthan xeegettiday oonikka baawa” yaagidosona.
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
Iya aaway oona gidi sunthaneekko eranaw koyidi iya malla oychchidosona.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
I xaafiyabaa oychchi ekkidi, “Iya sunthay Yohaannisa” gidi xaafis. Ubbay I xaafidayssa be7idi malaalettidosona.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
Iira Zakkariyaasa inxarssay bilettis, Xoossaa galatishe odetethi oykkis.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
Shooroti ubbay yashshan kumidosona. Ha hanidabay geze Yihuda biittan odettis.
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
Hessa si7ida ubbay, “Ha na7ay ay hananddeshsha” gidi bantta giddon odettidosona. Godaa kushey iyara de7ees.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
Yohaannisa aaway Zakkariyaasi Geeshsha Ayyaanan kumidi hayssada yaagidi tinbbite odis.
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
“Isra7eeliya Goday galatetto, yidi ba asaa wozis.
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
Ba aylliya Dawite keethan atotethaa kaciya denthis.
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
Hessika beni wode geeshsha nabeta doonan odettidayssa mela, (aiōn )
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
Iya ashoy nu morkketappenne nuura eqettiya ubbaa kushiyappe.
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
Hessa I oothiday nu aawatas ba maarota bessanaasinne, ba geeshsha caaquwa naaganaassa.
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
Nu aawa Abrahames caaqqida caaquwa qoppanasinne
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
nu morkketa kusheppe kessidi yashshi baynna iya haggaazana melassa.
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
Nu laytha ubban geeshshatethaninne xillotethan ba sinthan nuna essanaassa.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
Qassi laa na7aw, neeni Ubbaafe Bolla Xoossaa nabe geetettana. Godaa ogiya loythanaw ne iya sinthan baana.
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
Entta nagaray qushettin, entti atotethi demmanayssa ne Godaa deriyas odana.
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
Nu Xoossaa lo77o maarotethaafe denddoyssan wontta xalqey nuus saluwappe keyis.
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
Hessika dhumaninne, hayqo kuya garssan de7eyssatas poo7isanaassa, nu tohuwakka saro ogiyakko zaaranaassa” yaagis.
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
Na7ay diccis, Ayyaanan minnis, Isra7eele asaas qonccana gakkanaw bazzo biittan de7is.