< Luka 1 >
1 Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
Since, indeed, many have attempted to set in order a narrative of the things that have been completed among us,
2 kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
just as they have been handed on to those of us who from the beginning saw the same and were ministers of the word,
3 mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
so it seemed good to me also, having diligently followed everything from the beginning, to write to you, in an orderly manner, most excellent Theophilus,
4 ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
so that you might know the truthfulness of those words by which you have been instructed.
5 Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
There was, in the days of Herod, king of Judea, a certain priest named Zechariah, of the section of Abijah, and his wife was of the daughters of Aaron, and her name was Elizabeth.
6 Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
Now they were both just before God, progressing in all of the commandments and the justifications of the Lord without blame.
7 Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
And they had no child, because Elizabeth was barren, and they both had become advanced in years.
8 Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
Then it happened that, when he was exercising the priesthood before God, in the order of his section,
9 alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
according to the custom of the priesthood, the lot fell so that he would offer incense, entering into the temple of the Lord.
10 Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
And the entire multitude of the people was praying outside, at the hour of incense.
11 Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
Then there appeared to him an Angel of the Lord, standing at the right of the altar of incense.
12 Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
And upon seeing him, Zechariah was disturbed, and fear fell over him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
But the Angel said to him: “Do not be afraid, Zechariah, for your prayer has been heard, and your wife Elizabeth shall bear a son to you. And you shall call his name John.
14 Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
And there will be joy and exultation for you, and many will rejoice in his nativity.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
For he will be great in the sight of the Lord, and he will not drink wine or strong drink, and he will be filled with the Holy Spirit, even from his mother’s womb.
16 Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
And he will convert many of the sons of Israel to the Lord their God.
17 Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
And he will go before him with the spirit and power of Elijah, so that he may turn the hearts of the fathers to the sons, and the incredulous to the prudence of the just, so as to prepare for the Lord a completed people.”
18 Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
And Zechariah said to the Angel: “How may I know this? For I am elderly, and my wife is advanced in years.”
19 Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
And in response, the Angel said to him: “I am Gabriel, who stands before God, and I have been sent to speak to you, and to proclaim these things to you.
20 Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
And behold, you will be silent and unable to speak, until the day on which these things shall be, because you have not believed my words, which will be fulfilled in their time.”
21 Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
And the people were waiting for Zechariah. And they wondered why he was being delayed in the temple.
22 Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
Then, when he came out, he was unable to speak to them. And they realized that he had seen a vision in the temple. And he was making signs to them, but he remained mute.
23 Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
And it happened that, after the days of his office were completed, he went away to his house.
24 Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
Then, after those days, his wife Elizabeth conceived, and she hid herself for five months, saying:
25 Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
“For the Lord did this for me, at the time when he decided to take away my reproach among men.”
26 Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
Then, in the sixth month, the Angel Gabriel was sent by God, to a city of Galilee named Nazareth,
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
to a virgin betrothed to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the name of the virgin was Mary.
28 Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
And upon entering, the Angel said to her: “Hail, full of grace. The Lord is with you. Blessed are you among women.”
29 Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
And when she had heard this, she was disturbed by his words, and she considered what kind of greeting this might be.
30 Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
And the Angel said to her: “Do not be afraid, Mary, for you have found grace with God.
31 Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
Behold, you shall conceive in your womb, and you shall bear a son, and you shall call his name: JESUS.
32 Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
He will be great, and he will be called the Son of the Most High, and the Lord God will give him the throne of David his father.
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
And he will reign in the house of Jacob for eternity. And his kingdom shall have no end.” (aiōn )
34 Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
Then Mary said to the Angel, “How shall this be done, since I do not know man?”
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
And in response, the Angel said to her: “The Holy Spirit will pass over you, and the power of the Most High will overshadow you. And because of this also, the Holy One who will be born of you shall be called the Son of God.
36 Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
And behold, your cousin Elizabeth has herself also conceived a son, in her old age. And this is the sixth month for her who is called barren.
37 Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
For no word will be impossible with God.”
38 Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
Then Mary said: “Behold, I am the handmaid of the Lord. Let it be done to me according to your word.” And the Angel departed from her.
39 Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
And in those days, Mary, rising up, traveled quickly into the hill country, to a city of Judah.
40 Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
And she entered into the house of Zechariah, and she greeted Elizabeth.
41 Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
And it happened that, as Elizabeth heard the greeting of Mary, the infant leaped in her womb, and Elizabeth was filled with the Holy Spirit.
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
And she cried out with a loud voice and said: “Blessed are you among women, and blessed is the fruit of your womb.
43 Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
And how does this concern me, so that the mother of my Lord would come to me?
44 Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
For behold, as the voice of your greeting came to my ears, the infant in my womb leaped for joy.
45 Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
And blessed are you who believed, for the things that were spoken to you by the Lord shall be accomplished.”
46 Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
And Mary said: “My soul magnifies the Lord.
47 nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
And my spirit leaps for joy in God my Savior.
48 kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
For he has looked with favor on the humility of his handmaid. For behold, from this time, all generations shall call me blessed.
49 kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
For he who is great has done great things for me, and holy is his name.
50 Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
And his mercy is from generation to generations for those who fear him.
51 Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
He has accomplished powerful deeds with his arm. He has scattered the arrogant in the intentions of their heart.
52 Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
He has deposed the powerful from their seat, and he has exalted the humble.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
He has filled the hungry with good things, and the rich he has sent away empty.
54 Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
He has taken up his servant Israel, mindful of his mercy,
55 Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
just as he spoke to our fathers: to Abraham and to his offspring forever.” (aiōn )
56 Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
Then Mary stayed with her for about three months. And she returned to her own house.
57 Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
Now the time for Elizabeth to give birth arrived, and she brought forth a son.
58 Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
And her neighbors and relatives heard that the Lord had magnified his mercy with her, and so they congratulated her.
59 Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
And it happened that, on the eighth day, they arrived to circumcise the boy, and they called him by his father’s name, Zechariah.
60 Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
And in response, his mother said: “Not so. Instead, he shall be called John.”
61 Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
And they said to her, “But there is no one among your relatives who is called by that name.”
62 Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
Then they made signs to his father, as to what he wanted him to be called.
63 Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
And requesting a writing tablet, he wrote, saying: “His name is John.” And they all wondered.
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
Then, at once, his mouth was opened, and his tongue loosened, and he spoke, blessing God.
65 Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
And fear fell upon all of their neighbors. And all these words were made known throughout all the hill country of Judea.
66 Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
And all those who heard it stored it up in their heart, saying: “What do you think this boy will be?” And indeed, the hand of the Lord was with him.
67 Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
And his father Zechariah was filled with the Holy Spirit. And he prophesied, saying:
68 “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
“Blessed is the Lord God of Israel. For he has visited and has wrought the redemption of his people.
69 Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
And he has raised up a horn of salvation for us, in the house of David his servant,
70 kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
just as he spoke by the mouth of his holy Prophets, who are from ages past: (aiōn )
71 kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
salvation from our enemies, and from the hand of all those who hate us,
72 ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
to accomplish mercy with our fathers, and to call to mind his holy testament,
73 kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
the oath, which he swore to Abraham, our father, that he would grant to us,
74 kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
so that, having been freed from the hand of our enemies, we may serve him without fear,
75 katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
in holiness and in justice before him, throughout all our days.
76 “Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
And you, child, shall be called the prophet of the Most High. For you will go before the face of the Lord: to prepare his ways,
77 kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
to give knowledge of salvation to his people for the remission of their sins,
78 kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
through the heart of the mercy of our God, by which, descending from on high, he has visited us,
79 ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
to illuminate those who sit in darkness and in the shadow of death, and to direct our feet in the way of peace.”
80 Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.
And the child grew, and he was strengthened in spirit. And he was in the wilderness, until the day of his manifestation to Israel.