< Luka 9 >
1 Yesu kisha akawaita wale kumi na wawili pamoja, akawapa mamlaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,
tataH paraM sa dvAdashashiShyAnAhUya bhUtAn tyAjayituM rogAn pratikarttu ncha tebhyaH shaktimAdhipatya ncha dadau|
2 kisha akawatuma waende wakahubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
apara ncha IshvarIyarAjyasya susaMvAdaM prakAshayitum rogiNAmArogyaM karttu ncha preraNakAle tAn jagAda|
3 Akawaagiza akisema, “Msichukue chochote safarini: sio fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, hata msichukue kanzu ya ziada.
yAtrArthaM yaShTi rvastrapuTakaM bhakShyaM mudrA dvitIyavastram, eShAM kimapi mA gR^ihlIta|
4 Katika nyumba yoyote mwingiayo, kaeni humo hadi mtakapoondoka katika mji huo.
yUya ncha yanniveshanaM pravishatha nagaratyAgaparyyanataM tanniveshane tiShThata|
5 Kama watu wasipowakaribisha, mnapoondoka katika mji wao, kungʼuteni mavumbi kutoka kwenye miguu yenu ili kuwa ushuhuda dhidi yao.”
tatra yadi kasyachit purasya lokA yuShmAkamAtithyaM na kurvvanti tarhi tasmAnnagarAd gamanakAle teShAM viruddhaM sAkShyArthaM yuShmAkaM padadhUlIH sampAtayata|
6 Hivyo wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji, wakihubiri habari njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
atha te prasthAya sarvvatra susaMvAdaM prachArayituM pIDitAn svasthAn karttu ncha grAmeShu bhramituM prArebhire|
7 Basi Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za yote yaliyotendeka. Naye akafadhaika, kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema Yohana Mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu.
etarhi herod rAjA yIshoH sarvvakarmmaNAM vArttAM shrutvA bhR^ishamudvivije
8 Wengine wakasema Eliya amewatokea, na wengine wakasema kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuka.
yataH kechidUchuryohan shmashAnAdudatiShThat| kechidUchuH, eliyo darshanaM dattavAn; evamanyalokA UchuH pUrvvIyaH kashchid bhaviShyadvAdI samutthitaH|
9 Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa. Lakini ni nani huyu ambaye ninasikia mambo kama haya kumhusu?” Akatamani sana kumwona.
kintu heroduvAcha yohanaH shiro. ahamaChinadam idAnIM yasyedR^ikkarmmaNAM vArttAM prApnomi sa kaH? atha sa taM draShTum aichChat|
10 Mitume wake waliporudi, wakamweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua, akaenda nao faraghani mpaka mji uitwao Bethsaida.
anantaraM preritAH pratyAgatya yAni yAni karmmANi chakrustAni yIshave kathayAmAsuH tataH sa tAn baitsaidAnAmakanagarasya vijanaM sthAnaM nItvA guptaM jagAma|
11 Lakini umati wa watu ukafahamu alikokwenda, ukamfuata. Akawakaribisha na kunena nao kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwaponya wale wote waliokuwa wanahitaji uponyaji.
pashchAl lokAstad viditvA tasya pashchAd yayuH; tataH sa tAn nayan IshvarIyarAjyasya prasa NgamuktavAn, yeShAM chikitsayA prayojanam AsIt tAn svasthAn chakAra cha|
12 Ilipokaribia jioni, wale mitume kumi na wawili wakaenda kwa Yesu na kumwambia, “Waage makutano ili waende vijijini jirani na mashambani, ili wapate chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tuko nyikani.”
apara ncha divAvasanne sati dvAdashashiShyA yIshorantikam etya kathayAmAsuH, vayamatra prAntarasthAne tiShThAmaH, tato nagarANi grAmANi gatvA vAsasthAnAni prApya bhakShyadravyANi kretuM jananivahaM bhavAn visR^ijatu|
13 Yesu akawajibu, “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakajibu, “Hatuna zaidi ya mikate mitano na samaki wawili. Labda twende tukanunue chakula cha kuwatosha watu hawa wote.”
tadA sa uvAcha, yUyameva tAn bhejayadhvaM; tataste prochurasmAkaM nikaTe kevalaM pa ncha pUpA dvau matsyau cha vidyante, ataeva sthAnAntaram itvA nimittameteShAM bhakShyadravyeShu na krIteShu na bhavati|
14 Walikuwako wanaume wapatao 5,000. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini hamsini.”
tatra prAyeNa pa nchasahasrANi puruShA Asan|
15 Wanafunzi wakafanya hivyo, wakawaketisha wote.
tadA sa shiShyAn jagAda pa nchAshat pa nchAshajjanaiH paMktIkR^itya tAnupaveshayata, tasmAt te tadanusAreNa sarvvalokAnupaveshayApAsuH|
16 Yesu akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavibariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi ili wawagawie watu.
tataH sa tAn pa ncha pUpAn mInadvaya ncha gR^ihItvA svargaM vilokyeshvaraguNAn kIrttayA nchakre bha NktA cha lokebhyaH pariveShaNArthaM shiShyeShu samarpayAmbabhUva|
17 Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
tataH sarvve bhuktvA tR^iptiM gatA avashiShTAnA ncha dvAdasha DallakAn saMjagR^ihuH|
18 Wakati mmoja, Yesu alipokuwa akiomba faraghani, nao wanafunzi wake wakiwa pamoja naye, akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
athaikadA nirjane shiShyaiH saha prArthanAkAle tAn paprachCha, lokA mAM kaM vadanti?
19 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema kwamba ni mmoja wa manabii wa kale amefufuka kutoka kwa wafu.”
tataste prAchuH, tvAM yohanmajjakaM vadanti; kechit tvAm eliyaM vadanti, pUrvvakAlikaH kashchid bhaviShyadvAdI shmashAnAd udatiShThad ityapi kechid vadanti|
20 Kisha akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo wa Mungu.”
tadA sa uvAcha, yUyaM mAM kaM vadatha? tataH pitara uktavAn tvam IshvarAbhiShiktaH puruShaH|
21 Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo.
tadA sa tAn dR^iDhamAdidesha, kathAmetAM kasmaichidapi mA kathayata|
22 Yesu akasema, “Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na itampasa auawe, lakini siku ya tatu kufufuliwa kutoka mauti.”
sa punaruvAcha, manuShyaputreNa vahuyAtanA bhoktavyAH prAchInalokaiH pradhAnayAjakairadhyApakaishcha sovaj nAya hantavyaH kintu tR^itIyadivase shmashAnAt tenotthAtavyam|
23 Kisha akawaambia wote, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
aparaM sa sarvvAnuvAcha, kashchid yadi mama pashchAd gantuM vA nChati tarhi sa svaM dAmyatu, dine dine krushaM gR^ihItvA cha mama pashchAdAgachChatu|
24 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
yato yaH kashchit svaprANAn rirakShiShati sa tAn hArayiShyati, yaH kashchin madarthaM prANAn hArayiShyati sa tAn rakShiShyati|
25 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akapoteza au kuangamiza nafsi yake?
kashchid yadi sarvvaM jagat prApnoti kintu svaprANAn hArayati svayaM vinashyati cha tarhi tasya ko lAbhaH?
26 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu atakapokuja katika utukufu wake na katika utukufu wa Baba, pamoja na malaika watakatifu.
puna ryaH kashchin mAM mama vAkyaM vA lajjAspadaM jAnAti manuShyaputro yadA svasya pitushcha pavitrANAM dUtAnA ncha tejobhiH pariveShTita AgamiShyati tadA sopi taM lajjAspadaM j nAsyati|
27 Amin, nawaambia, wako baadhi ya watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu.”
kintu yuShmAnahaM yathArthaM vadAmi, IshvarIyarAjatvaM na dR^iShTavA mR^ityuM nAsvAdiShyante, etAdR^ishAH kiyanto lokA atra sthane. api daNDAyamAnAH santi|
28 Yapata siku nane baada ya Yesu kusema hayo, aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana, akaenda nao mlimani kuomba.
etadAkhyAnakathanAt paraM prAyeNAShTasu dineShu gateShu sa pitaraM yohanaM yAkUba ncha gR^ihItvA prArthayituM parvvatamekaM samAruroha|
29 Alipokuwa akiomba, sura ya uso wake ikabadilika, nayo mavazi yake yakametameta kama mwanga wa umeme wa radi.
atha tasya prArthanakAle tasya mukhAkR^itiranyarUpA jAtA, tadIyaM vastramujjvalashuklaM jAtaM|
30 Ghafula wakawaona watu wawili, ndio Mose na Eliya, wakizungumza naye.
apara ncha mUsA eliyashchobhau tejasvinau dR^iShTau
31 Walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea huko Yerusalemu.
tau tena yirUshAlampure yo mR^ityuH sAdhiShyate tadIyAM kathAM tena sArddhaM kathayitum ArebhAte|
32 Petro na wenzake walikuwa wamelala usingizi mzito. Walipoamka, wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
tadA pitarAdayaH svasya sa Ngino nidrayAkR^iShTA Asan kintu jAgaritvA tasya tejastena sArddham uttiShThantau janau cha dadR^ishuH|
33 Mose na Eliya walipokuwa wanaondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri tukae hapa! Tutajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.” Lakini Petro alikuwa hajui asemacho.
atha tayorubhayo rgamanakAle pitaro yIshuM babhAShe, he guro. asmAkaM sthAne. asmin sthitiH shubhA, tata ekA tvadarthA, ekA mUsArthA, ekA eliyArthA, iti tisraH kuTyosmAbhi rnirmmIyantAM, imAM kathAM sa na vivichya kathayAmAsa|
34 Alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu, likawafunika, nao wakaogopa walipoingia mle kwenye wingu.
apara ncha tadvAkyavadanakAle payoda eka Agatya teShAmupari ChAyAM chakAra, tatastanmadhye tayoH praveshAt te shasha Nkire|
35 Sauti ikatoka kwenye lile wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, niliyemchagua. Msikieni yeye.”
tadA tasmAt payodAd iyamAkAshIyA vANI nirjagAma, mamAyaM priyaH putra etasya kathAyAM mano nidhatta|
36 Baada ya sauti hiyo kusema, walimkuta Yesu akiwa peke yake. Wale wanafunzi wakalihifadhi jambo hili, wala kwa wakati huo hawakumwambia mtu yeyote yale waliyokuwa wameyaona.
iti shabde jAte te yIshumekAkinaM dadR^ishuH kintu te tadAnIM tasya darshanasya vAchamekAmapi noktvA manaHsu sthApayAmAsuH|
37 Kesho yake waliposhuka kutoka mlimani, alikutana na umati mkubwa wa watu.
pare. ahani teShu tasmAchChailAd avarUDheShu taM sAkShAt karttuM bahavo lokA AjagmuH|
38 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akapaza sauti, akasema, “Mwalimu, naomba umwangalie mwanangu, kwani ndiye mtoto wangu wa pekee.
teShAM madhyAd eko jana uchchairuvAcha, he guro ahaM vinayaM karomi mama putraM prati kR^ipAdR^iShTiM karotu, mama sa evaikaH putraH|
39 Mara kwa mara pepo mchafu humpagaa na kumfanya apige kelele, kisha humwangusha na kumtia kifafa hata akatokwa na povu kinywani. Huyo pepo mchafu anamtesa sana, na hamwachi ila mara chache.
bhUtena dhR^itaH san saM prasabhaM chIchChabdaM karoti tanmukhAt pheNA nirgachChanti cha, bhUta itthaM vidAryya kliShTvA prAyashastaM na tyajati|
40 Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
tasmAt taM bhUtaM tyAjayituM tava shiShyasamIpe nyavedayaM kintu te na shekuH|
41 Yesu akawajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”
tadA yIshuravAdIt, re AvishvAsin vipathagAmin vaMsha katikAlAn yuShmAbhiH saha sthAsyAmyahaM yuShmAkam AcharaNAni cha sahiShye? tava putramihAnaya|
42 Hata yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo mchafu akamwangusha, akamtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu amtoke, akamponya yule mtoto, na akamrudisha kwa baba yake.
tatastasminnAgatamAtre bhUtastaM bhUmau pAtayitvA vidadAra; tadA yIshustamamedhyaM bhUtaM tarjayitvA bAlakaM svasthaM kR^itvA tasya pitari samarpayAmAsa|
43 Watu wote wakastaajabia uweza mkuu wa Mungu. Wakati bado watu walikuwa wanastaajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye akawaambia wanafunzi wake:
Ishvarasya mahAshaktim imAM vilokya sarvve chamachchakruH; itthaM yIshoH sarvvAbhiH kriyAbhiH sarvvairlokairAshcharyye manyamAne sati sa shiShyAn babhAShe,
44 “Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.”
katheyaM yuShmAkaM karNeShu pravishatu, manuShyaputro manuShyANAM kareShu samarpayiShyate|
45 Lakini wao hawakuelewa alimaanisha nini. Maana ya maneno hayo ilifichika kwao, hivyo hawakuyaelewa, nao wakaogopa kumuuliza maana yake.
kintu te tAM kathAM na bubudhire, spaShTatvAbhAvAt tasyA abhiprAyasteShAM bodhagamyo na babhUva; tasyA AshayaH ka ityapi te bhayAt praShTuM na shekuH|
46 Kukazuka mabishano miongoni mwa wanafunzi kuhusu ni nani miongoni mwao atakayekuwa mkuu kuliko wote.
tadanantaraM teShAM madhye kaH shreShThaH kathAmetAM gR^ihItvA te mitho vivAdaM chakruH|
47 Lakini Yesu akayatambua mawazo yao, naye akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kando yake.
tato yIshusteShAM manobhiprAyaM viditvA bAlakamekaM gR^ihItvA svasya nikaTe sthApayitvA tAn jagAda,
48 Kisha akawaambia, “Yeyote amkaribishaye mtoto huyu mdogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi, na yeyote atakayenikaribisha mimi, atakuwa amemkaribisha yeye aliyenituma. Kwa maana yeye aliye mdogo miongoni mwenu, ndiye aliye mkuu kuliko wote.”
yo jano mama nAmnAsya bAlAsyAtithyaM vidadhAti sa mamAtithyaM vidadhAti, yashcha mamAtithyaM vidadhAti sa mama prerakasyAtithyaM vidadhAti, yuShmAkaM madhyeyaH svaM sarvvasmAt kShudraM jAnIte sa eva shreShTho bhaviShyati|
49 Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamzuia, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
apara ncha yohan vyAjahAra he prabhe tava nAmnA bhUtAn tyAjayantaM mAnuSham ekaM dR^iShTavanto vayaM, kintvasmAkam apashchAd gAmitvAt taM nyaShedhAm| tadAnIM yIshuruvAcha,
50 Yesu akasema, “Msimzuie, kwa sababu yeyote ambaye si kinyume nanyi, yu upande wenu.”
taM mA niShedhata, yato yo janosmAkaM na vipakShaH sa evAsmAkaM sapakSho bhavati|
51 Wakati ulipokaribia wa yeye kuchukuliwa mbinguni, alikaza uso wake kwenda Yerusalemu.
anantaraM tasyArohaNasamaya upasthite sa sthirachetA yirUshAlamaM prati yAtrAM karttuM nishchityAgre dUtAn preShayAmAsa|
52 Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu;
tasmAt te gatvA tasya prayojanIyadravyANi saMgrahItuM shomiroNIyAnAM grAmaM pravivishuH|
53 lakini watu wa kijiji kile hawakumkaribisha kwa sababu alikuwa anakwenda zake Yerusalemu.
kintu sa yirUshAlamaM nagaraM yAti tato heto rlokAstasyAtithyaM na chakruH|
54 Wanafunzi wake, yaani Yakobo na Yohana, walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuagize moto kutoka mbinguni ili uwaangamize?”
ataeva yAkUbyohanau tasya shiShyau tad dR^iShTvA jagadatuH, he prabho eliyo yathA chakAra tathA vayamapi kiM gagaNAd Agantum etAn bhasmIkarttu ncha vahnimAj nApayAmaH? bhavAn kimichChati?
55 Yesu akageuka na kuwakemea,
kintu sa mukhaM parAvartya tAn tarjayitvA gaditavAn yuShmAkaM manobhAvaH kaH, iti yUyaM na jAnItha|
56 nao wakaenda kijiji kingine.
manujasuto manujAnAM prANAn nAshayituM nAgachChat, kintu rakShitum AgachChat| pashchAd itaragrAmaM te yayuH|
57 Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”
tadanantaraM pathi gamanakAle jana ekastaM babhAShe, he prabho bhavAn yatra yAti bhavatA sahAhamapi tatra yAsyAmi|
58 Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
tadAnIM yIshustamuvAcha, gomAyUnAM garttA Asate, vihAyasIyavihagAnAM nIDAni cha santi, kintu mAnavatanayasya shiraH sthApayituM sthAnaM nAsti|
59 Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
tataH paraM sa itarajanaM jagAda, tvaM mama pashchAd ehi; tataH sa uvAcha, he prabho pUrvvaM pitaraM shmashAne sthApayituM mAmAdishatu|
60 Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”
tadA yIshuruvAcha, mR^itA mR^itAn shmashAne sthApayantu kintu tvaM gatveshvarIyarAjyasya kathAM prachAraya|
61 Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”
tatonyaH kathayAmAsa, he prabho mayApi bhavataH pashchAd gaMsyate, kintu pUrvvaM mama niveshanasya parijanAnAm anumatiM grahItum ahamAdishyai bhavatA|
62 Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”
tadAnIM yIshustaM proktavAn, yo jano lA Ngale karamarpayitvA pashchAt pashyati sa IshvarIyarAjyaM nArhati|