< Luka 9 >
1 Yesu kisha akawaita wale kumi na wawili pamoja, akawapa mamlaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,
Puis [Jésus] ayant assemblé ses douze Disciples, leur donna puissance et autorité sur tous les démons, et [le pouvoir] de guérir les malades.
2 kisha akawatuma waende wakahubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
Et il les envoya prêcher le Royaume de Dieu, et guérir les malades,
3 Akawaagiza akisema, “Msichukue chochote safarini: sio fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, hata msichukue kanzu ya ziada.
Et leur dit: ne portez rien pour le voyage, ni bâtons, ni sac, ni pain, ni argent; et n'ayez point chacun deux robes.
4 Katika nyumba yoyote mwingiayo, kaeni humo hadi mtakapoondoka katika mji huo.
Et en quelque maison que vous entriez, demeurez-y jusqu'à ce que vous partiez de là.
5 Kama watu wasipowakaribisha, mnapoondoka katika mji wao, kungʼuteni mavumbi kutoka kwenye miguu yenu ili kuwa ushuhuda dhidi yao.”
Et partout où l'on ne vous recevra point, en partant de cette ville-là secouez la poudre de vos pieds, en témoignage contre eux.
6 Hivyo wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji, wakihubiri habari njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
Eux donc étant partis allaient de bourgade en bourgade, évangélisant, et guérissant partout.
7 Basi Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za yote yaliyotendeka. Naye akafadhaika, kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema Yohana Mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu.
Or Hérode le Tétrarque ouït parler de toutes les choses que Jésus faisait; et il ne savait que croire de ce que quelques-uns disaient que Jean était ressuscité des morts;
8 Wengine wakasema Eliya amewatokea, na wengine wakasema kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuka.
Et quelques-uns, qu'Elie était apparu; et d'autres, que quelqu'un des anciens Prophètes était ressuscité.
9 Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa. Lakini ni nani huyu ambaye ninasikia mambo kama haya kumhusu?” Akatamani sana kumwona.
Et Hérode dit: j'ai [fait] décapiter Jean; qui est donc celui-ci de qui j'entends dire de telles choses? Et il cherchait à le voir.
10 Mitume wake waliporudi, wakamweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua, akaenda nao faraghani mpaka mji uitwao Bethsaida.
Puis les Apôtres étant de retour, lui racontèrent toutes les choses qu'ils avaient faites. Et Jésus les emmena avec lui, et se retira dans un lieu désert, près de la ville appelée Bethsaïda.
11 Lakini umati wa watu ukafahamu alikokwenda, ukamfuata. Akawakaribisha na kunena nao kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwaponya wale wote waliokuwa wanahitaji uponyaji.
Ce que les troupes ayant su, elles le suivirent, et il les reçut, et leur parlait du Royaume de Dieu, et guérissait ceux qui avaient besoin d'être guéris.
12 Ilipokaribia jioni, wale mitume kumi na wawili wakaenda kwa Yesu na kumwambia, “Waage makutano ili waende vijijini jirani na mashambani, ili wapate chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tuko nyikani.”
Or le jour ayant commencé à baisser, les douze [Disciples] vinrent à [lui], et lui dirent: donne congé à cette multitude, afin qu'ils s'en aillent aux bourgades et aux villages des environs, pour s'y retirer, et trouver à manger; car nous sommes ici dans un pays désert.
13 Yesu akawajibu, “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakajibu, “Hatuna zaidi ya mikate mitano na samaki wawili. Labda twende tukanunue chakula cha kuwatosha watu hawa wote.”
Mais il leur dit: donnez-leur vous-mêmes à manger. Et ils dirent: nous n'avons pas plus de cinq pains et de deux poissons; à moins que nous n'allions acheter des vivres pour tout ce peuple;
14 Walikuwako wanaume wapatao 5,000. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini hamsini.”
Car ils étaient environ cinq mille hommes. Et il dit à ses Disciples: faites-les arranger par troupes, de cinquante chacune.
15 Wanafunzi wakafanya hivyo, wakawaketisha wote.
Ils le firent ainsi, et les firent tous arranger.
16 Yesu akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavibariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi ili wawagawie watu.
Puis il prit les cinq pains et les deux poissons, et regardant vers le ciel, il les bénit, et les rompit, et il les distribua à ses Disciples, afin qu'ils les missent devant cette multitude.
17 Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
Et ils en mangèrent tous, et furent rassasiés, et on remporta douze corbeilles pleines des pièces de pain qu'il y avait eu de reste.
18 Wakati mmoja, Yesu alipokuwa akiomba faraghani, nao wanafunzi wake wakiwa pamoja naye, akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
Or il arriva que comme il était dans un lieu retiré pour prier, et que les Disciples étaient avec lui, il les interrogea, disant: qui disent les troupes que je suis?
19 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema kwamba ni mmoja wa manabii wa kale amefufuka kutoka kwa wafu.”
Ils lui répondirent: [Les uns disent que tu es] Jean Baptiste; et les autres, Elie; et les autres, que quelqu'un des anciens Prophètes est ressuscité.
20 Kisha akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo wa Mungu.”
Il leur dit alors: et vous, qui dites-vous que je suis? Et Pierre répondant lui dit: tu es le Christ de Dieu.
21 Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo.
Mais usant de menaces il leur commanda de ne le dire à personne.
22 Yesu akasema, “Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na itampasa auawe, lakini siku ya tatu kufufuliwa kutoka mauti.”
Et il leur dit: il faut que le Fils de l'homme souffre beaucoup, et qu'il soit rejeté des Anciens, et des principaux Sacrificateurs, et des Scribes, et qu'il soit mis à mort, et qu'il ressuscite le troisième jour.
23 Kisha akawaambia wote, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
Puis il disait à tous: si quelqu'un veut venir après moi, qu'il renonce à soi-même, et qu'il charge de jour en jour sa croix, et me suive.
24 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
Car quiconque voudra sauver sa vie, la perdra; mais quiconque perdra sa vie pour l'amour de moi, la sauvera.
25 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akapoteza au kuangamiza nafsi yake?
Et que sert-il à un homme de gagner tout le monde, s'il se détruit lui-même, et se perd lui-même?
26 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu atakapokuja katika utukufu wake na katika utukufu wa Baba, pamoja na malaika watakatifu.
Car quiconque aura eu honte de moi et de mes paroles; le Fils de l'homme aura honte de lui, quand il viendra en sa gloire, et [dans celle] du Père, et des saints Anges.
27 Amin, nawaambia, wako baadhi ya watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu.”
Et je vous dis, en vérité, qu'entre ceux qui sont ici présents, il y en a qui ne mourront point jusqu'à ce qu'ils aient vu le règne de Dieu.
28 Yapata siku nane baada ya Yesu kusema hayo, aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana, akaenda nao mlimani kuomba.
Or il arriva environ huit jours après ces paroles, qu'il prit avec lui Pierre, et Jean, et Jacques, et qu'il monta sur une montagne pour prier.
29 Alipokuwa akiomba, sura ya uso wake ikabadilika, nayo mavazi yake yakametameta kama mwanga wa umeme wa radi.
Et comme il priait, la forme de son visage devint tout autre, et son vêtement devint blanc en sorte qu'il était resplendissant comme un éclair.
30 Ghafula wakawaona watu wawili, ndio Mose na Eliya, wakizungumza naye.
Et voici, deux personnages, savoir Moïse et Elie, parlaient avec lui.
31 Walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea huko Yerusalemu.
Et ils apparurent environnés de gloire, et ils parlaient de sa mort qu'il devait souffrir à Jérusalem.
32 Petro na wenzake walikuwa wamelala usingizi mzito. Walipoamka, wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
Or Pierre et ceux qui étaient avec lui étaient accablés de sommeil; et quand ils furent réveillés, ils virent sa gloire, et les deux personnages qui étaient avec lui.
33 Mose na Eliya walipokuwa wanaondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri tukae hapa! Tutajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.” Lakini Petro alikuwa hajui asemacho.
Et il arriva comme ces personnages se séparaient de lui, que Pierre dit à Jésus: Maître, il est bon que nous soyons ici, faisons-y donc trois tentes, une pour toi, une pour Moïse, et une pour Elie; ne sachant ce qu'il disait.
34 Alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu, likawafunika, nao wakaogopa walipoingia mle kwenye wingu.
Et comme il disait ces choses, une nuée vint qui les couvrit de son ombre; et comme ils entraient dans la nuée, ils eurent peur.
35 Sauti ikatoka kwenye lile wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, niliyemchagua. Msikieni yeye.”
Et une voix vint de la nuée, disant: celui-ci est mon Fils bien-aimé; écoutez-le.
36 Baada ya sauti hiyo kusema, walimkuta Yesu akiwa peke yake. Wale wanafunzi wakalihifadhi jambo hili, wala kwa wakati huo hawakumwambia mtu yeyote yale waliyokuwa wameyaona.
Et comme la voix se prononçait, Jésus se trouva seul. Et ils se turent tous, et ils ne rapportèrent en ces jours-là à personne rien de ce qu'ils avaient vu.
37 Kesho yake waliposhuka kutoka mlimani, alikutana na umati mkubwa wa watu.
Or il arriva le jour suivant, qu'eux étant descendus de la montagne, une grande troupe vint à sa rencontre.
38 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akapaza sauti, akasema, “Mwalimu, naomba umwangalie mwanangu, kwani ndiye mtoto wangu wa pekee.
Et voici, un homme de la troupe s'écria, disant: Maître, Je te prie, jette les yeux sur mon fils, car je n'ai que celui-là.
39 Mara kwa mara pepo mchafu humpagaa na kumfanya apige kelele, kisha humwangusha na kumtia kifafa hata akatokwa na povu kinywani. Huyo pepo mchafu anamtesa sana, na hamwachi ila mara chache.
Et voici, un esprit le saisit, qui aussitôt le fait crier, et l'agite avec violence en le faisant écumer, et à peine il se retire de lui, après l'avoir [comme] brisé.
40 Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
Or j'ai prié tes Disciples de le chasser dehors, mais ils n'ont pu.
41 Yesu akawajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”
Et Jésus répondant dit: ô génération incrédule et perverse, jusques à quand serai-je avec vous, et vous supporterai-je? Amène ici ton fils.
42 Hata yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo mchafu akamwangusha, akamtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu amtoke, akamponya yule mtoto, na akamrudisha kwa baba yake.
Et comme il approchait seulement, le démon l'agita violemment comme s'il l'eût voulu déchirer; mais Jésus censura fortement l'esprit immonde, et guérit l'enfant, et le rendit à son père.
43 Watu wote wakastaajabia uweza mkuu wa Mungu. Wakati bado watu walikuwa wanastaajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye akawaambia wanafunzi wake:
Et tous furent étonnés de la magnifique vertu de Dieu. Et comme tous s'étonnaient de tout ce qu'il faisait, il dit à ses Disciples:
44 “Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.”
Vous, écoutez bien ces discours: car il arrivera que le Fils de l'homme sera livré entre les mains des hommes.
45 Lakini wao hawakuelewa alimaanisha nini. Maana ya maneno hayo ilifichika kwao, hivyo hawakuyaelewa, nao wakaogopa kumuuliza maana yake.
Mais ils ne comprirent point cette parole, et elle leur était tellement obscure, qu'ils ne la comprenaient pas; et ils craignaient de l'interroger touchant cette parole.
46 Kukazuka mabishano miongoni mwa wanafunzi kuhusu ni nani miongoni mwao atakayekuwa mkuu kuliko wote.
Puis ils entrèrent en dispute, pour savoir lequel d'entre eux était le plus grand.
47 Lakini Yesu akayatambua mawazo yao, naye akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kando yake.
Mais Jésus voyant la pensée de leur cœur, prit un petit enfant, et le mit auprès de lui;
48 Kisha akawaambia, “Yeyote amkaribishaye mtoto huyu mdogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi, na yeyote atakayenikaribisha mimi, atakuwa amemkaribisha yeye aliyenituma. Kwa maana yeye aliye mdogo miongoni mwenu, ndiye aliye mkuu kuliko wote.”
Puis il leur dit: quiconque recevra ce petit enfant en mon Nom, il me reçoit; et quiconque me recevra, il reçoit celui qui m'a envoyé. Car celui qui est le plus petit d'entre vous tous, c'est celui qui sera grand.
49 Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamzuia, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
Et Jean prenant la parole, dit: Maître, nous avons vu quelqu'un qui chassait les démons en ton Nom, et nous l'en avons empêché parce qu'il ne [te] suit point avec nous.
50 Yesu akasema, “Msimzuie, kwa sababu yeyote ambaye si kinyume nanyi, yu upande wenu.”
Mais Jésus lui dit: ne l'en empêchez point; car celui qui n'est pas contre nous, est pour nous.
51 Wakati ulipokaribia wa yeye kuchukuliwa mbinguni, alikaza uso wake kwenda Yerusalemu.
Or il arriva quand les jours de son élévation s'accomplissaient, qu'il dressa sa face, [tout résolu] d'aller à Jérusalem.
52 Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu;
Et il envoya devant lui des messagers, qui étant partis entrèrent dans une bourgade des Samaritains, pour lui préparer un logis.
53 lakini watu wa kijiji kile hawakumkaribisha kwa sababu alikuwa anakwenda zake Yerusalemu.
Mais [les Samaritains] ne le reçurent point, parce qu'il paraissait qu'il allait à Jérusalem.
54 Wanafunzi wake, yaani Yakobo na Yohana, walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuagize moto kutoka mbinguni ili uwaangamize?”
Et quand Jacques et Jean, ses Disciples, virent cela, ils dirent: Seigneur! veux-tu que nous disions, comme fit Elie, que le feu descende du ciel, et les consume.
55 Yesu akageuka na kuwakemea,
Mais Jésus se tournant les censura fortement, en leur disant: Vous ne savez de quel esprit vous êtes [animés].
56 nao wakaenda kijiji kingine.
Car le Fils de l'homme n'est pas venu pour faire périr les âmes des hommes, mais pour les sauver. Ainsi ils s'en allèrent à une autre bourgade.
57 Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”
Et il arriva comme ils allaient par le chemin, qu'un certain homme lui dit: je te suivrai, Seigneur, partout où tu iras.
58 Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
Mais Jésus lui répondit: les renards ont des tanières, et les oiseaux du ciel ont des nids, mais le Fils de l'homme n'a pas où reposer sa tête.
59 Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
Puis il dit à un autre: suis-moi; et celui-ci [lui] répondit: permets-moi premièrement d'aller ensevelir mon père.
60 Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”
Et Jésus lui dit: laisse les morts ensevelir leurs morts; mais toi, va, et annonce le Royaume de Dieu.
61 Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”
Un autre aussi lui dit: Seigneur, je te suivrai; mais permets-moi de prendre premièrement congé de ceux qui sont dans ma maison.
62 Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”
Mais Jésus lui répondit: nul qui met la main à la charrue, et qui regarde en arrière, n'est bien disposé pour le Royaume de Dieu.