< Luka 8 >

1 Baada ya haya Yesu alikwenda, akawa anazunguka katika miji na vijiji akihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walikuwa pamoja naye,
Majdată d aja Isusu pljika p trgurj š p saturj s rubjaskă Bună vorbă d cara alu Dimizov. Afost ku Isusu duavăsprjače apostolurj
2 pia baadhi ya wanawake waliokuwa wametolewa pepo wachafu na kuponywa magonjwa. Miongoni mwao alikuwepo Maria Magdalene, aliyetolewa pepo wachafu saba;
š njeke mujerj karje Isusu lja likujit dăla sufljeti alji rovj š dăla buală. Alja mujerj afost Marija karje afost d trg Magdala, dăn karje Isusu aputirit šaptje sufljeti alji rovj,
3 Yoana mkewe Kuza, msimamizi wa nyumba ya watu wa nyumbani mwa Herode; Susana; na wengine wengi waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
Ivana, karje afost mujarja alu Kuza karje irja upravitelju ăn palače alu Herod, Suzana š multje altje mujerj. Jalje ku banji alor ažutat alu Isusuluj š alu apostolilor.
4 Umati mkubwa wa watu ulipokuwa ukija kwa Yesu kutoka kila mji, akawaambia mfano huu:
Kănd pănglă Isusu sa străns mulc lumje dăn tot trgu, atunča Isusu lji rubja asta vorbă:
5 “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia; zikakanyagwa, nao ndege wa angani wakazila.
“Una zuvă aišăt omu s posijaskă sămănca ăn polje. Kănd aposijit, njeka sămănca akăzut p drum š lumja umbla p aja š puji lja amănkat.
6 Mbegu nyingine zilianguka penye miamba, nazo zilipoota, hiyo mimea ikakauka kwa kukosa unyevu.
Njeka sămănca akăzut p pămănt undje jaštje buluvan š tek ča kriskut sa uskat daja če narje apă.
7 Nazo mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo ile miiba ikakua pamoja nazo, na kuisonga hiyo mimea.
Njeka sămănca akăzut ăntră mărčinj š mărčinjilje akriskut una ku jej š ja sa ugušăt.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri. Zikaota na kuzaa mara mia moja zaidi ya mbegu alizopanda.” Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti, akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
A njeka sămănca akăzut p bun pămănt š krjaštje š rudjaštje d usută d vorj.” Isusu azăs aja, š astrigat: “Toc činje arje urjekj s audă, trjebje s puje urjajke š s razumjaskă!”
9 Wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo.
Učenikurlje alu Isusuluj la antribat če značaštje asta vorbă.
10 Naye akasema, “Ninyi mmepewa kufahamu siri za Ufalme wa Mungu, lakini kwa wengine nazungumza kwa mifano, ili, “‘ingawa wanatazama, wasione; ingawa wanasikiliza, wasielewe.’
Isusu azăs: “Dopustit vuavă s razumic tajnilje d cara alu Dimizov. Ali koristjesk aša vorbje kănd jo ănvăc p alcă s ispunjaskă Svănta pismă: ‘S ujtă a nu prepoznajaštje, š s audă, a nu razumjaštje’.
11 “Maana ya mfano huu ni hii: Mbegu ni neno la Mungu.
Jakă če značaštje asta vorbă: sămănca je vorba alu Dimizov.
12 Zile zilizoanguka kando ya njia ni wale ambao husikia neno, naye ibilisi anakuja na kuliondoa neno kutoka mioyoni mwao, ili wasije wakaamini na kuokoka.
A sămănca karje akăzut p drum prestavjaštje p ălja karje audje, ali vinje nikuratu š adus vorba alu Dimizov d inima alor aša s nu krjadje š nu s spasaskă.
13 Zile mbegu zilizoanguka kwenye mwamba ni wale ambao hulipokea neno kwa furaha wanapolisikia, lakini hawana mizizi. Wanaamini kwa muda mfupi, lakini wakati wa kujaribiwa huiacha imani.
A sămănca karje akăzut p buluvan prestavjaštje p ălja karje audje, ku radost primjaštje vorba alu Dimizov, ali narje korjen. Ălja njeka vrijamje krjadje, a kănd vinje iskušjala prestanjaštje s krjadje.
14 Zile mbegu zilizoanguka kwenye miiba ni mfano wa wale wanaosikia, lakini wanapoendelea husongwa na masumbufu ya maisha haya, utajiri na anasa, nao hawakui.
A sămănca karje akăzut ăn mărčinj prestavjaštje p ăštja karje punje urjajke la vorba alu Dimizov, ali kum vrijamja trjače, p jej lji ugušaštje brigilje, bugucija š tuatje užitkulje alu životuluj, daja jej nu duče plodu kopt.
15 Lakini zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo mzuri ni mfano wa wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mnyofu wa utiifu, nao kwa kuvumilia kwingi huzaa matunda.
A sămănca karje akăzut p bun pămănt prestavjaštje p lumja karje ku bună š ku poštena inimă păzaštje vorba alu Dimizov karje audje, jej pljakă maj dăpartje kănd je grjev, daja jej aduče bun plod.”
16 “Hakuna mtu awashaye taa na kuificha ndani ya gudulia au kuiweka mvunguni mwa kitanda. Badala yake, huiweka juu ya kinara, ili wale waingiao ndani waone mwanga.
“Nimilja nu prindje lampa s viljaskă ku posuda ili s uaskundje dusu pat, njego s upuje p postolje aša toc ălja karje untră s puată s vjadă binje.
17 Kwa maana hakuna jambo lolote lililofichika ambalo halitafichuliwa, wala lolote lililositirika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi.
K tot čije ăviljit osă fije dăzvăljit š tot čije skuns osă s štije š osă vije p lumină.
18 Kwa hiyo, kuweni waangalifu mnavyosikia. Kwa maana yeyote aliye na kitu atapewa zaidi. Lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani anacho atanyangʼanywa.”
Daja punjec binje urjajke k ăla karje păzaštje vorba amja osă razumjaskă mult, a p ălja karje nu păzaštje vorba amja osă s ja š aja če găndjaštje k razumjaštje.”
19 Wakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kumwona, lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu.
Atunča muma š fracă alu Isusuluj avinjit s l vjadă, ali na putut s vije la jel k afost mulc lumje.
20 Mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.”
Ajavit alu Isusuluj: “Mumuta š fracă alji tej stă afar š vrja s t vjadă.”
21 Yesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulifanya.”
Kănd Isusu auzăt aja, azăs alu lumjej: “Ălja karje punje urjajke š askultă vorba alu Dimizov mije je ka muma š ka frac.”
22 Siku moja Yesu alipanda ndani ya mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo ya ziwa.” Nao wakaondoka.
Ăn una zuvă azăs Isusu alu učenikurlje aluj: “Tričem p alta partje la apă.” Jej auntrat ăn čamac š aotplovit.
23 Hivyo walipokuwa wakienda, akalala usingizi. Dhoruba kali ikatokea mle ziwani, hata mashua ikawa inajaa maji, nao walikuwa katika hatari kubwa.
Pănd plovja, Isusu ančiput s kulčje. Š ančiput s suflje marje vănt. Văntu ančiput s fakă marj valurj karje ančiput s napunjaskă čamacu d apă š jej sa găsăt ăn rov.
24 Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, Bwana, tunaangamia!” Yeye akaamka, akaukemea ule upepo na yale mawimbi; dhoruba ikakoma, nako kukawa shwari.
Jej avinjit la Isusu š la skulat š ja zăs: “Gospodarulje, Gospodarulje, tonim!” A Isusu sa skulat, azapovidit alu văntuluj š alu valulor alji marj s stja š jej sa smirit š afost tišina.
25 Akawauliza wanafunzi wake, “Imani yenu iko wapi?” Kwa woga na mshangao wakaulizana, “Huyu ni nani, ambaye anaamuru hata upepo na maji, navyo vikamtii?”
Atunča Isusu azăs alu učenikurlje aluj: “Dăče nas krizut ăn minje?” A učenikurlje sa spirjat š sa mirat. Azăs unji alu alc: “Činje ăsta s zapovidjaskă čak š alu văntuluj š alu apăj, š punje urjajke la jel?”
26 Basi wakafika katika nchi ya Wagerasi, ambayo iko upande wa pili wa ziwa kutoka Galilaya.
Avinjit ăn regija Gerasa, karje je p alta partje d apă d regija Galileja.
27 Yesu aliposhuka kutoka mashua na kukanyaga ufuoni, alikutana na mtu mmoja wa mji ule aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, naye kwa muda mrefu alikuwa havai nguo wala kuishi nyumbani, bali aliishi makaburini.
Čim Isusu aišăt d čamac p obală, avinjit la intja alu Isusuluj njeki om dăn trg karje avut sufljeti alji rovj ăn jel. Već d mult kum nu sa brkat nič atrijit ăn kasă njego irja la mărmănc.
28 Alipomwona Yesu, alipiga kelele, akajitupa chini mbele yake na kusema kwa sauti kuu, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Nakuomba, usinitese!”
Multă vrijamje sufljeti alji rovj l cănja š akă lumja la ljigat p lanacurj š okove š l păza, jel rupja lanacu š sufljeti alji rovj l natirja s pljače ăn lok undje nuje nimika. Kănd omula avizut p Isusu, acăpat. Isusu azapovidit alu sufljeti alji rovj s jašă d omula. Akăzut la intja alu Isusuluj š astrigat: “Če vrjaj dăla minje, Isusulje, Bijatu alu Maj marje Dimizov? Mărog d tinje, nu m mučja!”
29 Wakati huo Yesu alikuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke huyo mtu. Mara nyingi huyo pepo mchafu alimpagaa, na hata alipofungwa kwa minyororo mikono na miguu na kuwekwa chini ya ulinzi, alikata hiyo minyororo na kupelekwa na huyo pepo mchafu kwenda nyikani.
30 Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Legioni,” kwa kuwa alikuwa ameingiwa na pepo wachafu wengi mno.
Isusu la tribat: “Kum t kjem?” Jel zăče: “Mulc”, k afost ăn jel mulc sufljeti alji rovj.
31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo. (Abyssos g12)
Š sufljeti alji rovj ančiput mult s s ruađje d Isusu s nu naridjaskă s pljače ăn jamă frzdă kraj undje osă fije kaznic. (Abyssos g12)
32 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe hapo likilisha kando ya kilima. Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu awaruhusu wawaingie hao nguruwe, naye akawaruhusu.
A ănklo p djal mult porč s ranja. Sufljeti alji rovj sa rugat d Isusu s dopustjaskă s untră ăn porč š Isusu adopustit.
33 Wale pepo wachafu walipomtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremkia gengeni kwa kasi, likatumbukia ziwani na kuzama.
Atunča sufljeti alji rovj aišăt d om š auntrat ăn porč. Toc porči adat fuga ăn zos dăpă djal ăn apă š sa nikat.
34 Wale watu waliokuwa wakichunga lile kundi la nguruwe walipoona yaliyotukia, wakakimbia, wakaeneza habari hizi mjini na mashambani.
Kănd lumja karje păza p porči avizut ča fost, afuđit š arazglasăt p trg š p saturj.
35 Nao watu wakatoka kwenda kujionea wenyewe yaliyotukia. Walipofika hapo alipokuwa Yesu, wakamkuta yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu amekaa karibu na Yesu, akiwa amevaa nguo na mwenye akili timamu! Wakaogopa.
A lumja avinjit s vjadje ča fost. Kănd jej ažuns, avizut p Isusu ku omu dăn karje aišăt sufljeti alji rovj. Avizut p omu karje šadje š punja urjajke la Isusu, ănbrkat š bun ăn kap. Š lumja sa spirjat.
36 Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine jinsi yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu alivyoponywa.
Jej karje avizut ča fost, arubit alu lumjaja kum Isusu likujit p omu ăn karje afost sufljeti alji rovj.
37 Ndipo watu wote wa nchi ile ya Wagerasi wakamwomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu walikuwa wamejawa na hofu. Basi akaingia katika mashua, akaondoka zake.
Tuată lumja d regija Gerasa lja pukat marje frikă, š arugat p Isusu s pljače dăla jej. Isusu auntrat ăn čamac s pljače pisti apă ăndrăt.
38 Yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu akamsihi Yesu afuatane naye, lakini Yesu akamuaga, akamwambia:
Majdată njego če Isusu š učenikurlje aluj aotplovit ăn čamac, omu d karje sufljeti alji rovj aišăt sa rugat mult d Isusu s puată s rămăje ku jel. Ali Isusu ja zăs:
39 “Rudi nyumbani ukawaeleze mambo makuu Mungu aliyokutendea.” Kwa hiyo yule mtu akaenda, akatangaza katika mji wote mambo makuu ambayo Yesu alimtendea.
“Ăntuarčitje akas š zi alu toc če Dimizov afukut d tinje.” Atunča jel apljikat š razglasăt p tot trgu če ja fukut Isusu.
40 Basi Yesu aliporudi, umati mkubwa wa watu ukampokea kwa furaha, kwani walikuwa wakimngojea.
Multă lumje aštipta p Isusu s s ăntuarkă dăpă alta partje d apă. Kănd Isusu ažuns, toc ku radostu la štiptat.
41 Kisha mtu mmoja, jina lake Yairo, aliyekuwa kiongozi wa sinagogi, akaja na kuanguka miguuni mwa Yesu, akimwomba afike nyumbani kwake,
D dăturdată avinjit omu karje sa kima Jair, karje irja vođa alu lumje karje s sastaja ăn sinagogă. Akăzut la intja alu Isusuluj š mult sa rugat s vije ăn kasa aluj.
42 kwa kuwa binti yake wa pekee, mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa anakufa. Yesu alipokuwa akienda, umati wa watu ukamsonga sana.
Jel avut jedinică fată karje avut duavăsprjače d aj karje irja p muartje. Pănd Isusu pljika la Jair, mulc lumja l pinđja dăpă pistot.
43 Katika umati huo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa na tatizo la kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Tena alikuwa amegharimia yote aliyokuwa nayo kwa ajili ya matibabu, wala hakuna yeyote aliyeweza kumponya.
Ăntră lumje irja mujerj karje duavăsprjače d aj krvarja, š potrošăt tot ča vut p doktorjamje, ali nimilja na putut s ju likujaskă.
44 Huyo mwanamke akaja kwa nyuma ya Yesu na kugusa upindo wa vazi lake. Mara kutokwa damu kwake kukakoma.
Avinjit d drăt š apus măna p rubu alu cuala alu Isusuluj š odma aprestanit s krvarjaskă.
45 Yesu akauliza, “Ni nani aliyenigusa?” Watu wote walipokana, Petro akasema, “Bwana, huu umati wa watu unakusonga na kukusukuma kila upande.”
Antribat Isusu: “Činje apus măna p minje?” Š pănd toc azăs: “Nu jo”, Petar azăs: “Gospodarulje, multă lumje t pinđje š t strănđe!”
46 Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, kwa maana nimetambua kuwa nguvu zimenitoka.”
A Isusu azăs: “Njeko namjerno apus măna p minje. Amositit k săla aišăt d minje.”
47 Yule mwanamke alipofahamu ya kuwa hawezi kuendelea kujificha, alikuja akitetemeka, akaanguka miguuni mwa Yesu. Akaeleza mbele ya watu wote kwa nini alimgusa na jinsi alivyoponywa mara.
Kănd mujaraja saznajit k nu puatje s askundă k ja apus măna p Isusu, atrimurat d frikă š akăzut la intja alu Isusuluj š la intja alu tot narodu š lja zăs dăče apus măna p Isusu š kum odma sa likujit.
48 Basi Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
A Isusu alu je azăs: “Fata amja, tu ta likujit daja ča krizut. S c dja Dimizov mir pănd plječ!”
49 Yesu alipokuwa bado anasema, akaja mtumishi kutoka nyumbani kwa Yairo, yule kiongozi wa sinagogi, kumwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Usiendelee kumsumbua Mwalimu.”
Kănd Isusu još arubit alu mujaraja, avinjit njeko d kasă alu Jair ku poruka: “Camurit fata. Nu maj muča učitelju više.”
50 Yesu aliposikia jambo hili, akamwambia Yairo, “Usiogope. Amini tu, naye binti yako atapona.”
Auzăt Isusu š azăs alu Jair: “Na vja frikă! Samo krjadje š ja osă fije binje!”
51 Walipofika nyumbani kwa Yairo, hakumruhusu mtu yeyote aingie ndani naye isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, pamoja na baba na mama wa yule binti.
Kănd Isusu avinjit ăn kasă alu Jair, Isusu adopustit samo alu Petar, alu Ivan, š alu Jakov, š alu tatăj š alu mamăj alu fataja s utrje ku jel.
52 Wakati ule ule watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili ya huyo binti. Yesu akawaambia, “Acheni kulia. Huyu binti hajafa, ila amelala.”
Š toc karje već irja ăn kasă plănđja š tuguja dăpă ja. Isusu lja zăs: “Nu plănđec! Nuje muartă, njego s kulkă!”
53 Wao wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekwisha kufa.
Atunča toc ančiput s s ljađe d jel daja ča štijut k je muartă.
54 Yesu akamshika yule binti mkono na kuita, “Binti, amka!”
Isusu alato d mănă š astrigat: “Kupilulje, skual!”
55 Roho yake ikamrudia, naye akainuka mara moja. Akaamuru apewe kitu cha kula.
Š sufljetu sa tors š odma sa skulat. Isusu azăs s ji dja s mălănče.
56 Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote juu ya yale yaliyotukia.
Roditelji alu je irja začudic, a Isusu ja naredit s nu zăkă alu nimilja če sa dogodit.

< Luka 8 >