< Luka 8 >
1 Baada ya haya Yesu alikwenda, akawa anazunguka katika miji na vijiji akihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walikuwa pamoja naye,
And it came to pass, in due course, that he was passing through, city by city and village by village, proclaiming, and delivering the glad-message of the kingdom of God, —and, the twelve, were with him;
2 pia baadhi ya wanawake waliokuwa wametolewa pepo wachafu na kuponywa magonjwa. Miongoni mwao alikuwepo Maria Magdalene, aliyetolewa pepo wachafu saba;
and certain women, who had been cured from evil spirits and infirmities, —Mary, the one called Magdalene, from whom seven demons had gone forth,
3 Yoana mkewe Kuza, msimamizi wa nyumba ya watu wa nyumbani mwa Herode; Susana; na wengine wengi waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
and Joana, wife of Chuza steward of Herod, and Susanna, and many others, —who indeed were ministering unto them out of their possessions.
4 Umati mkubwa wa watu ulipokuwa ukija kwa Yesu kutoka kila mji, akawaambia mfano huu:
And, seeing that a great multitude were coming together, and they who from every city were journeying forth unto him, he spake through means of a parable: —
5 “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia; zikakanyagwa, nao ndege wa angani wakazila.
The sower went forth to sow his seed, —and, as he sowed, some, indeed, fell beside the pathway, and was trodden down; and, the birds of heaven, devoured it.
6 Mbegu nyingine zilianguka penye miamba, nazo zilipoota, hiyo mimea ikakauka kwa kukosa unyevu.
And, other, fell down upon the rock; and, growing, was withered, because it had not moisture.
7 Nazo mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo ile miiba ikakua pamoja nazo, na kuisonga hiyo mimea.
And, other, fell and thorns; and, growing together, the thorns, choked it.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri. Zikaota na kuzaa mara mia moja zaidi ya mbegu alizopanda.” Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti, akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
And, other, fell into good ground; and, growing, brought forth fruit, a hundredfold. These things, saying, he went on to cry aloud—He that hath ears to hear, let him hear.
9 Wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo.
But his disciples began to question him—What might, this very, parable be?
10 Naye akasema, “Ninyi mmepewa kufahamu siri za Ufalme wa Mungu, lakini kwa wengine nazungumza kwa mifano, ili, “‘ingawa wanatazama, wasione; ingawa wanasikiliza, wasielewe.’
And, he, said—Unto you, hath it been given, to get to know the sacred secrets of the kingdom of God; but, unto the rest, in parables, —in order that, seeing, they may not see, and, hearing, they may not understand.
11 “Maana ya mfano huu ni hii: Mbegu ni neno la Mungu.
Now the parable, is this—The seed, is, the word of God.
12 Zile zilizoanguka kando ya njia ni wale ambao husikia neno, naye ibilisi anakuja na kuliondoa neno kutoka mioyoni mwao, ili wasije wakaamini na kuokoka.
And, those beside the pathway, are they who have heard; afterwards, cometh the adversary, and catcheth away the word from their heart, lest, believing, they should, be saved.
13 Zile mbegu zilizoanguka kwenye mwamba ni wale ambao hulipokea neno kwa furaha wanapolisikia, lakini hawana mizizi. Wanaamini kwa muda mfupi, lakini wakati wa kujaribiwa huiacha imani.
And, those upon the rock, are they who, as soon as they hear, with joy, welcome the word; and, these, not having, root, are they who, for a season, believe, —and, in a season of testing, draw back.
14 Zile mbegu zilizoanguka kwenye miiba ni mfano wa wale wanaosikia, lakini wanapoendelea husongwa na masumbufu ya maisha haya, utajiri na anasa, nao hawakui.
And, that which in among the thorns fell, these, are they who have heard; and, by anxieties and wealth and pleasures of life being borne along, are choked up, and bear not to perfection.
15 Lakini zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo mzuri ni mfano wa wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mnyofu wa utiifu, nao kwa kuvumilia kwingi huzaa matunda.
But, that in the good ground, these, are they who, indeed, in a noble and good heart having heard the word, hold fast, and bear fruit with endurance.
16 “Hakuna mtu awashaye taa na kuificha ndani ya gudulia au kuiweka mvunguni mwa kitanda. Badala yake, huiweka juu ya kinara, ili wale waingiao ndani waone mwanga.
And, no one having lit a lamp, covereth it up with a vessel, or, beneath a couch, putteth it; but, upon a lamp-stand, putteth it, that, they who come in, may see the light.
17 Kwa maana hakuna jambo lolote lililofichika ambalo halitafichuliwa, wala lolote lililositirika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi.
For there is no secret, which shall not be made, manifest; neither a hidden thing, which shall in anywise not be made known, or not come, where it can be seen.
18 Kwa hiyo, kuweni waangalifu mnavyosikia. Kwa maana yeyote aliye na kitu atapewa zaidi. Lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani anacho atanyangʼanywa.”
Be taking heed therefore how ye hear; for, whosoever shall have, it shall be given unto him; and, whosoever shall not have, even what he seemeth to have, shall be taken from him.
19 Wakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kumwona, lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu.
And his mother and brethren came near unto him, and were unable to reach him, because of the multitude.
20 Mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.”
And it was reported to him—Thy mother and thy brethren, are standing outside, desiring, to see, thee.
21 Yesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulifanya.”
But, he, answering, said unto them—My mother and my brethren, are, these—they who, the word of God, are hearing and doing.
22 Siku moja Yesu alipanda ndani ya mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo ya ziwa.” Nao wakaondoka.
And it came to pass, on one of the days, that, he, entered into a boat, and his disciples; and he said unto them—Let us pass over unto the other side of the lake. And they set sail.
23 Hivyo walipokuwa wakienda, akalala usingizi. Dhoruba kali ikatokea mle ziwani, hata mashua ikawa inajaa maji, nao walikuwa katika hatari kubwa.
Now, as they were sailing, he fell asleep. And there came down a hurricane of wind upon the lake, and they began to be filled, and to be in peril.
24 Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, Bwana, tunaangamia!” Yeye akaamka, akaukemea ule upepo na yale mawimbi; dhoruba ikakoma, nako kukawa shwari.
And, coming near, they roused him up, saying—Master! Master! we perish! And, he, roused up, rebuked the wind, and the surging of the water; and they ceased, and it became a calm.
25 Akawauliza wanafunzi wake, “Imani yenu iko wapi?” Kwa woga na mshangao wakaulizana, “Huyu ni nani, ambaye anaamuru hata upepo na maji, navyo vikamtii?”
And he said unto them—Where was your faith? But, struck with fear, they marvelled, saying one to another—Who then is, this, —that, even unto the winds, he giveth orders, and unto the water, and they hearken unto him.
26 Basi wakafika katika nchi ya Wagerasi, ambayo iko upande wa pili wa ziwa kutoka Galilaya.
And they sailed down into the country of the Gerasenes, the which is over against Galilee.
27 Yesu aliposhuka kutoka mashua na kukanyaga ufuoni, alikutana na mtu mmoja wa mji ule aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, naye kwa muda mrefu alikuwa havai nguo wala kuishi nyumbani, bali aliishi makaburini.
And, when he went forth upon the land, there met him a certain man, out of the city, having demons; and, for a considerable time, he had put on no garment, and, in a house, would not abide, but among the tombs.
28 Alipomwona Yesu, alipiga kelele, akajitupa chini mbele yake na kusema kwa sauti kuu, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Nakuomba, usinitese!”
But, seeing Jesus, he cried out aloud, and fell down before him, and, with a loud voice, said—What have I in common with thee, O Jesus, Son of [God] the Most High? I beg of thee—Do not torment me!—
29 Wakati huo Yesu alikuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke huyo mtu. Mara nyingi huyo pepo mchafu alimpagaa, na hata alipofungwa kwa minyororo mikono na miguu na kuwekwa chini ya ulinzi, alikata hiyo minyororo na kupelekwa na huyo pepo mchafu kwenda nyikani.
for he was about to charge the impure spirit to come out from the man. For, many times, had it snatched him away; and he used to be bound with chains and fetters, for a safe-guard, and was wont to break in pieces the bonds, and to be driven by the demon into the deserts.
30 Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Legioni,” kwa kuwa alikuwa ameingiwa na pepo wachafu wengi mno.
And Jesus questioned him—What name hast thou? And, he, said—Legion! because many demons had entered into him.
31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo. (Abyssos )
And they were beseeching him that he would not order them, into the abyss, to depart. (Abyssos )
32 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe hapo likilisha kando ya kilima. Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu awaruhusu wawaingie hao nguruwe, naye akawaruhusu.
Now there was there, a herd of a good many swine, feeding in the mountain; and they besought him, that he would suffer them, into those, to enter; and he suffered them.
33 Wale pepo wachafu walipomtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremkia gengeni kwa kasi, likatumbukia ziwani na kuzama.
And the demons, going forth from the man entered into the swine; and the herd rushed down the cliff, into the lake, and were choked.
34 Wale watu waliokuwa wakichunga lile kundi la nguruwe walipoona yaliyotukia, wakakimbia, wakaeneza habari hizi mjini na mashambani.
And they who had been feeding them, seeing what had happened, fled, and carried tidings into the city, and into the country-places.
35 Nao watu wakatoka kwenda kujionea wenyewe yaliyotukia. Walipofika hapo alipokuwa Yesu, wakamkuta yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu amekaa karibu na Yesu, akiwa amevaa nguo na mwenye akili timamu! Wakaogopa.
And they went forth to see what had happened; and came unto Jesus, and found the man from whom the demons had gone forth, sitting, clothed, and of sound mind, near the feet of Jesus, —and they were struck with fear.
36 Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine jinsi yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu alivyoponywa.
And they who had seen it, reported unto them, how the demonized man was saved.
37 Ndipo watu wote wa nchi ile ya Wagerasi wakamwomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu walikuwa wamejawa na hofu. Basi akaingia katika mashua, akaondoka zake.
And one and all of the throng of the surrounding country of the Gerasenes, requested him, to depart from them; because, with a great fear, were they oppressed. And, he, entering into a boat, returned.
38 Yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu akamsihi Yesu afuatane naye, lakini Yesu akamuaga, akamwambia:
And the man from whom the demons had gone forth, began to beg of him, that he might be with him; but he dismissed him, saying—
39 “Rudi nyumbani ukawaeleze mambo makuu Mungu aliyokutendea.” Kwa hiyo yule mtu akaenda, akatangaza katika mji wote mambo makuu ambayo Yesu alimtendea.
Be returning unto thy house, and telling forth what great things, God, for thee, hath done. And he departed, through all the city, proclaiming what great things, Jesus, had done for him.
40 Basi Yesu aliporudi, umati mkubwa wa watu ukampokea kwa furaha, kwani walikuwa wakimngojea.
Now, when Jesus returned, the multitude welcomed him back, for they were all expecting him.
41 Kisha mtu mmoja, jina lake Yairo, aliyekuwa kiongozi wa sinagogi, akaja na kuanguka miguuni mwa Yesu, akimwomba afike nyumbani kwake,
And lo! there came a man, whose name was Jairus, and, the same, was, a ruler of the synagogue, —and, falling down near the feet of Jesus, he began beseeching him to enter into his house;
42 kwa kuwa binti yake wa pekee, mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa anakufa. Yesu alipokuwa akienda, umati wa watu ukamsonga sana.
because he had, an only-begotten daughter, about twelve years old, and, she, was dying. Now, as he withdrew, the multitudes, were hemming him in.
43 Katika umati huo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa na tatizo la kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Tena alikuwa amegharimia yote aliyokuwa nayo kwa ajili ya matibabu, wala hakuna yeyote aliyeweza kumponya.
And, a woman, with a flow of blood of twelve years standing, who indeed could, from no one, be cured,
44 Huyo mwanamke akaja kwa nyuma ya Yesu na kugusa upindo wa vazi lake. Mara kutokwa damu kwake kukakoma.
coming near behind, touched the fringe of his mantle; and, instantly, was stayed the flow of her blood.
45 Yesu akauliza, “Ni nani aliyenigusa?” Watu wote walipokana, Petro akasema, “Bwana, huu umati wa watu unakusonga na kukusukuma kila upande.”
And Jesus said—Who, is it that touched me? And, when all were denying, Peter said—Master! the multitudes, are hemming thee in, and pressing along.
46 Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, kwa maana nimetambua kuwa nguvu zimenitoka.”
But, Jesus, said—Some one touched me, for, I, took note of power, gone out from me.
47 Yule mwanamke alipofahamu ya kuwa hawezi kuendelea kujificha, alikuja akitetemeka, akaanguka miguuni mwa Yesu. Akaeleza mbele ya watu wote kwa nini alimgusa na jinsi alivyoponywa mara.
And, the woman seeing that she had not escaped notice, trembling, came, and, falling down before him, reported before all the people, for what cause she had touched him, and how she was healed instantly!
48 Basi Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
And, he, said to her—Daughter! thy faith, hath saved thee: Go thy way into peace.
49 Yesu alipokuwa bado anasema, akaja mtumishi kutoka nyumbani kwa Yairo, yule kiongozi wa sinagogi, kumwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Usiendelee kumsumbua Mwalimu.”
While yet he is speaking, there cometh one from the synagogue ruler’s, saying—Thy daughter, is dead: No further, be troubling the teacher.
50 Yesu aliposikia jambo hili, akamwambia Yairo, “Usiogope. Amini tu, naye binti yako atapona.”
But, Jesus, hearing, answered him—Do not fear! Only believe, and she shall be saved.
51 Walipofika nyumbani kwa Yairo, hakumruhusu mtu yeyote aingie ndani naye isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, pamoja na baba na mama wa yule binti.
And, when he came into the house, he suffered no one to enter with him, save Peter and John and James, and the father of the girl, and the mother.
52 Wakati ule ule watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili ya huyo binti. Yesu akawaambia, “Acheni kulia. Huyu binti hajafa, ila amelala.”
And they were all weeping, and beating themselves, for her. And he said—Be not weeping; for she died not, but is sleeping.
53 Wao wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekwisha kufa.
And they were deriding him, knowing that she died.
54 Yesu akamshika yule binti mkono na kuita, “Binti, amka!”
But, he, grasping her hand, called aloud, saying—O girl! arise!
55 Roho yake ikamrudia, naye akainuka mara moja. Akaamuru apewe kitu cha kula.
And her spirit returned, and she rose up instantly, and he ordered that something should be given her to eat.
56 Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote juu ya yale yaliyotukia.
And her parents were beside themselves. But, he, charged them to tell, no one, what had happened.