< Luka 8 >

1 Baada ya haya Yesu alikwenda, akawa anazunguka katika miji na vijiji akihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walikuwa pamoja naye,
And it happened afterwards that he was making a journey through the cities and towns, preaching and evangelizing the kingdom of God. And the twelve were with him,
2 pia baadhi ya wanawake waliokuwa wametolewa pepo wachafu na kuponywa magonjwa. Miongoni mwao alikuwepo Maria Magdalene, aliyetolewa pepo wachafu saba;
along with certain women who had been healed of evil spirits and infirmities: Mary, who is called Magdalene, from whom seven demons had departed,
3 Yoana mkewe Kuza, msimamizi wa nyumba ya watu wa nyumbani mwa Herode; Susana; na wengine wengi waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
and Joanna, the wife of Chuza, Herod’s steward, and Susanna, and many other women, who were ministering to him from their resources.
4 Umati mkubwa wa watu ulipokuwa ukija kwa Yesu kutoka kila mji, akawaambia mfano huu:
Then, when a very numerous crowd was gathering together and hurrying from the cities to him, he spoke using a comparison:
5 “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia; zikakanyagwa, nao ndege wa angani wakazila.
“The sower went out to sow his seed. And as he sowed, some fell beside the way; and it was trampled and the birds of the air devoured it.
6 Mbegu nyingine zilianguka penye miamba, nazo zilipoota, hiyo mimea ikakauka kwa kukosa unyevu.
And some fell upon rock; and having sprung up, it withered away, because it had no moisture.
7 Nazo mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo ile miiba ikakua pamoja nazo, na kuisonga hiyo mimea.
And some fell among thorns; and the thorns, rising up with it, suffocated it.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri. Zikaota na kuzaa mara mia moja zaidi ya mbegu alizopanda.” Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti, akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
And some fell upon good soil; and having sprung up, it produced fruit one hundredfold.” As he said these things, he cried out, “Whoever has ears to hear, let him hear.”
9 Wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo.
Then his disciples questioned him as to what this parable might mean.
10 Naye akasema, “Ninyi mmepewa kufahamu siri za Ufalme wa Mungu, lakini kwa wengine nazungumza kwa mifano, ili, “‘ingawa wanatazama, wasione; ingawa wanasikiliza, wasielewe.’
And he said to them: “To you it has been given to know the mystery of the kingdom of God. But to the rest, it is in parables, so that: seeing, they may not perceive, and hearing, they may not understand.
11 “Maana ya mfano huu ni hii: Mbegu ni neno la Mungu.
Now the parable is this: The seed is the word of God.
12 Zile zilizoanguka kando ya njia ni wale ambao husikia neno, naye ibilisi anakuja na kuliondoa neno kutoka mioyoni mwao, ili wasije wakaamini na kuokoka.
And those beside the way are those who hear it, but then the devil comes and takes the word from their heart, lest by believing it they may be saved.
13 Zile mbegu zilizoanguka kwenye mwamba ni wale ambao hulipokea neno kwa furaha wanapolisikia, lakini hawana mizizi. Wanaamini kwa muda mfupi, lakini wakati wa kujaribiwa huiacha imani.
Now those upon rock are those who, when they hear it, accept the word with joy, but these have no roots. So they believe for a time, but in a time of testing, they fall away.
14 Zile mbegu zilizoanguka kwenye miiba ni mfano wa wale wanaosikia, lakini wanapoendelea husongwa na masumbufu ya maisha haya, utajiri na anasa, nao hawakui.
And those which fell among thorns are those who have heard it, but as they go along, they are suffocated by the concerns and riches and pleasures of this life, and so they do not yield fruit.
15 Lakini zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo mzuri ni mfano wa wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mnyofu wa utiifu, nao kwa kuvumilia kwingi huzaa matunda.
But those which were on good soil are those who, upon hearing the word with a good and noble heart, retain it, and they bring forth fruit in patience.
16 “Hakuna mtu awashaye taa na kuificha ndani ya gudulia au kuiweka mvunguni mwa kitanda. Badala yake, huiweka juu ya kinara, ili wale waingiao ndani waone mwanga.
Now no one, lighting a candle, covers it with a container, or sets it under a bed. Instead, he places it on a lampstand, so that those who enter may see the light.
17 Kwa maana hakuna jambo lolote lililofichika ambalo halitafichuliwa, wala lolote lililositirika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi.
For there is nothing secret, which will not be made clear, nor is there anything hidden, which will not be known and be brought into plain sight.
18 Kwa hiyo, kuweni waangalifu mnavyosikia. Kwa maana yeyote aliye na kitu atapewa zaidi. Lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani anacho atanyangʼanywa.”
Therefore, take care how you listen. For whoever has, it will be given to him; and whoever does not have, even what he thinks he has will be taken away from him.”
19 Wakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kumwona, lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu.
Then his mother and brothers came to him; but they were not able to go to him because of the crowd.
20 Mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.”
And it was reported to him, “Your mother and your brothers are standing outside, wanting to see you.”
21 Yesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulifanya.”
And in response, he said to them, “My mother and my brothers are those who hear the word of God and do it.”
22 Siku moja Yesu alipanda ndani ya mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo ya ziwa.” Nao wakaondoka.
Now it happened, on a certain day, that he climbed into a little boat with his disciples. And he said to them, “Let us make a crossing over the lake.” And they embarked.
23 Hivyo walipokuwa wakienda, akalala usingizi. Dhoruba kali ikatokea mle ziwani, hata mashua ikawa inajaa maji, nao walikuwa katika hatari kubwa.
And as they were sailing, he slept. And a windstorm descended over the lake. And they were taking on water and were in danger.
24 Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, Bwana, tunaangamia!” Yeye akaamka, akaukemea ule upepo na yale mawimbi; dhoruba ikakoma, nako kukawa shwari.
Then, drawing near, they awakened him, saying, “Teacher, we are perishing.” But as he rose up, he rebuked the wind and the raging water, and they ceased. And a tranquility occurred.
25 Akawauliza wanafunzi wake, “Imani yenu iko wapi?” Kwa woga na mshangao wakaulizana, “Huyu ni nani, ambaye anaamuru hata upepo na maji, navyo vikamtii?”
Then he said to them, “Where is your faith?” And they, being afraid, were amazed, saying to one another, “Who do you think this is, so that he commands both wind and sea, and they obey him?”
26 Basi wakafika katika nchi ya Wagerasi, ambayo iko upande wa pili wa ziwa kutoka Galilaya.
And they sailed to the region of the Gerasenes, which is opposite Galilee.
27 Yesu aliposhuka kutoka mashua na kukanyaga ufuoni, alikutana na mtu mmoja wa mji ule aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, naye kwa muda mrefu alikuwa havai nguo wala kuishi nyumbani, bali aliishi makaburini.
And when he had gone out to the land, a certain man met him, who had now had a demon for a long time. And he did not wear clothes, nor did he stay in a house, but among the sepulchers.
28 Alipomwona Yesu, alipiga kelele, akajitupa chini mbele yake na kusema kwa sauti kuu, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Nakuomba, usinitese!”
And when he saw Jesus, he fell down before him. And crying out in a loud voice, he said: “What is there between me and you, Jesus, Son of the Most High God? I beg you not to torture me.”
29 Wakati huo Yesu alikuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke huyo mtu. Mara nyingi huyo pepo mchafu alimpagaa, na hata alipofungwa kwa minyororo mikono na miguu na kuwekwa chini ya ulinzi, alikata hiyo minyororo na kupelekwa na huyo pepo mchafu kwenda nyikani.
For he was ordering the unclean spirit to depart from the man. For on many occasions, it would seize him, and he was bound with chains and held by fetters. But breaking the chains, he was driven by the demon into deserted places.
30 Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Legioni,” kwa kuwa alikuwa ameingiwa na pepo wachafu wengi mno.
Then Jesus questioned him, saying, “What is your name?” And he said, “Legion,” because many demons had entered into him.
31 Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo. (Abyssos g12)
And they petitioned him not to order them to go into the abyss. (Abyssos g12)
32 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe hapo likilisha kando ya kilima. Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu awaruhusu wawaingie hao nguruwe, naye akawaruhusu.
And in that place, there was a herd of many swine, pasturing on the mountain. And they petitioned him to permit them to enter into them. And he permitted them.
33 Wale pepo wachafu walipomtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremkia gengeni kwa kasi, likatumbukia ziwani na kuzama.
Therefore, the demons departed from the man, and they entered into the swine. And the herd rushed violently down a precipice into the lake, and they were drowned.
34 Wale watu waliokuwa wakichunga lile kundi la nguruwe walipoona yaliyotukia, wakakimbia, wakaeneza habari hizi mjini na mashambani.
And when those who were pasturing them had seen this, they fled and reported it in the city and the villages.
35 Nao watu wakatoka kwenda kujionea wenyewe yaliyotukia. Walipofika hapo alipokuwa Yesu, wakamkuta yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu amekaa karibu na Yesu, akiwa amevaa nguo na mwenye akili timamu! Wakaogopa.
Then they went out to see what was happening, and they came to Jesus. And they found the man, from whom the demons had departed, sitting at his feet, clothed as well as in a sane mind, and they were afraid.
36 Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine jinsi yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu alivyoponywa.
Then those who had seen this also reported to them how he had been healed from the legion.
37 Ndipo watu wote wa nchi ile ya Wagerasi wakamwomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu walikuwa wamejawa na hofu. Basi akaingia katika mashua, akaondoka zake.
And the entire multitude from the region of the Gerasenes pleaded with him to depart from them. For they were seized by a great fear. Then, climbing into the boat, he went back again.
38 Yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu akamsihi Yesu afuatane naye, lakini Yesu akamuaga, akamwambia:
And the man from whom the demons had departed pleaded with him, so that he might be with him. But Jesus sent him away, saying,
39 “Rudi nyumbani ukawaeleze mambo makuu Mungu aliyokutendea.” Kwa hiyo yule mtu akaenda, akatangaza katika mji wote mambo makuu ambayo Yesu alimtendea.
“Return to your house and explain to them what great things God has done for you.” And he traveled through the entire city, preaching about the great things that Jesus had done for him.
40 Basi Yesu aliporudi, umati mkubwa wa watu ukampokea kwa furaha, kwani walikuwa wakimngojea.
Now it happened that, when Jesus had returned, the crowd received him. For they were all waiting for him.
41 Kisha mtu mmoja, jina lake Yairo, aliyekuwa kiongozi wa sinagogi, akaja na kuanguka miguuni mwa Yesu, akimwomba afike nyumbani kwake,
And behold, a man came, whose name was Jairus, and he was a leader of the synagogue. And he fell down at the feet of Jesus, asking him to enter into his house.
42 kwa kuwa binti yake wa pekee, mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa anakufa. Yesu alipokuwa akienda, umati wa watu ukamsonga sana.
For he had an only daughter, nearly twelve years old, and she was dying. And it happened that, as he was going there, he was hemmed in by the crowd.
43 Katika umati huo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa na tatizo la kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Tena alikuwa amegharimia yote aliyokuwa nayo kwa ajili ya matibabu, wala hakuna yeyote aliyeweza kumponya.
And there was a certain woman, with a flow of blood for twelve years, who had paid out all her substance on physicians, and she was unable to be cured by any of them.
44 Huyo mwanamke akaja kwa nyuma ya Yesu na kugusa upindo wa vazi lake. Mara kutokwa damu kwake kukakoma.
She approached him from behind, and she touched the hem of his garment. And at once the flow of her blood stopped.
45 Yesu akauliza, “Ni nani aliyenigusa?” Watu wote walipokana, Petro akasema, “Bwana, huu umati wa watu unakusonga na kukusukuma kila upande.”
And Jesus said, “Who is it that touched me?” But as everyone was denying it, Peter, and those who were with him, said: “Teacher, the crowd hems you in and presses upon you, and yet you say, ‘Who touched me?’”
46 Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, kwa maana nimetambua kuwa nguvu zimenitoka.”
And Jesus said: “Someone has touched me. For I know that power has gone out from me.”
47 Yule mwanamke alipofahamu ya kuwa hawezi kuendelea kujificha, alikuja akitetemeka, akaanguka miguuni mwa Yesu. Akaeleza mbele ya watu wote kwa nini alimgusa na jinsi alivyoponywa mara.
Then the woman, upon seeing that she was not hidden, came forward, trembling, and she fell down before his feet. And she declared before all the people the reason that she had touched him, and how she had been immediately healed.
48 Basi Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
But he said to her: “Daughter, your faith has saved you. Go in peace.”
49 Yesu alipokuwa bado anasema, akaja mtumishi kutoka nyumbani kwa Yairo, yule kiongozi wa sinagogi, kumwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Usiendelee kumsumbua Mwalimu.”
While he was still speaking, someone came to the ruler of the synagogue, saying to him: “Your daughter is dead. Do not trouble him.”
50 Yesu aliposikia jambo hili, akamwambia Yairo, “Usiogope. Amini tu, naye binti yako atapona.”
Then Jesus, upon hearing this word, replied to the father of the girl: “Do not be afraid. Only believe, and she will be saved.”
51 Walipofika nyumbani kwa Yairo, hakumruhusu mtu yeyote aingie ndani naye isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, pamoja na baba na mama wa yule binti.
And when he had arrived at the house, he would not permit anyone to enter with him, except Peter and James and John, and the father and mother of the girl.
52 Wakati ule ule watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili ya huyo binti. Yesu akawaambia, “Acheni kulia. Huyu binti hajafa, ila amelala.”
Now all were weeping and mourning for her. But he said: “Do not weep. The girl is not dead, but only sleeping.”
53 Wao wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekwisha kufa.
And they derided him, knowing that she had died.
54 Yesu akamshika yule binti mkono na kuita, “Binti, amka!”
But he, taking her by the hand, cried out, saying, “Little girl, arise.”
55 Roho yake ikamrudia, naye akainuka mara moja. Akaamuru apewe kitu cha kula.
And her spirit returned, and she immediately rose up. And he ordered them to give her something to eat.
56 Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote juu ya yale yaliyotukia.
And her parents were stupefied. And he instructed them not to tell anyone what had happened.

< Luka 8 >