< Luka 7 >

1 Baada ya Yesu kumaliza kusema haya yote watu wakiwa wanamsikiliza, akaingia Kapernaumu.
Ko je torej končal vse svoje govore pred občinstvom ljudi, je vstopil v Kafarnáum.
2 Mtumishi wa jemadari mmoja wa Kirumi, ambaye bwana wake alimthamini sana, alikuwa mgonjwa sana karibu kufa.
Neki služabnik stotnika, ki mu je bil dragocen, je bil bolan in pripravljen na smrt.
3 Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee wa Kiyahudi kwake, wakamwomba aje kumponya mtumishi wa huyo jemadari.
Ko je slišal o Jezusu, je k njemu poslal judovske starešine in ga rotil, da bi prišel in ozdravil njegovega služabnika.
4 Wale wazee walipofika kwa Yesu, wakamsihi sana amsaidie yule jemadari wakisema, “Mtu huyu anastahili wewe umfanyie jambo hili,
Ko so prišli k Jezusu, so ga takoj iskreno rotili, rekoč: »Vreden je bil, da bi to storil zanj,
5 kwa sababu analipenda taifa letu tena ametujengea sinagogi.”
kajti rad ima naš narod in sinagogo nam je zgradil.«
6 Hivyo Yesu akaongozana nao, lakini alipokuwa hayuko mbali na nyumbani, yule jemadari akatuma rafiki zake kumwambia Yesu, “Bwana, usijisumbue, kwani mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu.
Potem je Jezus odšel z njimi. In ko je bil torej nedaleč od hiše, je stotnik k njemu poslal prijatelje, rekoč mu: »Gospod, ne delaj si sitnosti, kajti nisem vreden, da bi stopil pod mojo streho,
7 Ndiyo maana sikujiona hata ninastahili kuja kwako wewe. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
zato se tudi nisem imel za vrednega, da bi prišel k tebi, toda reci besedo in moj služabnik bo ozdravljen.
8 Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
Kajti tudi sam sem človek, postavljen pod oblast. Pod seboj imam vojake in nekomu rečem: ›Pojdi, ‹ in gre, in drugemu: ›Pridi‹ in pride, in svojemu služabniku: ›Naredi to, ‹ in to stori.«
9 Yesu aliposikia maneno haya, alishangazwa naye sana. Akaugeukia ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akawaambia, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
Ko je Jezus slišal te besede, se je začudil nad njim in se obrnil ter rekel množici, ki mu je sledila: »Povem vam: ›Nisem našel tako velike vere, ne, niti v Izraelu ne.‹«
10 Nao wale watu waliokuwa wametumwa kwa Yesu waliporudi nyumbani walimkuta yule mtumishi amepona.
In tisti, ki so bili poslani, so se vrnili k hiši in našli služabnika, ki je bil bolan, zdravega.
11 Baadaye kidogo, Yesu alikwenda katika mji mmoja ulioitwa Naini. Nao wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu walikwenda pamoja naye.
Pripetilo se je dan kasneje, da je odšel v mesto, imenovano Nain in z njim so odšli mnogi izmed njegovih učencev ter veliko ljudi.
12 Alipokaribia lango la mji, alikutana na watu waliokuwa wamebeba maiti wakitoka nje ya mji. Huyu aliyekufa alikuwa mwana pekee wa mwanamke mjane. Umati mkubwa wa watu wa mji ule ulikuwa pamoja na huyo mwanamke.
Ko je torej prišel blizu k mestnim velikim vratom, glej, je bil ven odnesen mrtev človek, edini sin njegove matere in ta je bila vdova; in z njo je bilo veliko ljudi iz mesta.
13 Bwana Yesu alipomwona yule mjane, moyo wake ulimhurumia, akamwambia, “Usilie.”
Ko jo je Gospod zagledal, je imel sočutje do nje in ji je rekel: »Ne jokaj.«
14 Kisha akasogea mbele akaligusa lile jeneza na wale waliokuwa wamelibeba wakasimama kimya. Akasema, “Kijana, nakuambia inuka.”
Prišel je in se dotaknil mrtvaškega odra, in tisti, ki so ga nosili, so mirno stali. In rekel je: »Mladenič, rečem ti: ›Vstani.‹«
15 Yule aliyekuwa amekufa akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
In ta, ki je bil mrtev, se je usedel in začel govoriti. In izročil ga je njegovi materi.
16 Watu wote wakajawa na hofu ya Mungu, nao wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea miongoni mwetu, Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
Strah je prišel na vse in slavili so Boga, rekoč, da je med nami vstal velik prerok in da je Bog obiskal svoje ljudi.
17 Habari hizi za mambo aliyoyafanya Yesu zikaenea Uyahudi wote na sehemu zote za jirani.
In ta govorica o njem je šla naprej po vsej celotni Judeji in naokoli po vsem celotnem področju.
18 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakamweleza Yohana mambo haya yote. Hivyo Yohana akawaita wanafunzi wake wawili
In Janezovi učenci so mu povedali o vseh teh stvareh.
19 na kuwatuma kwa Bwana ili kumuuliza, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
In Janez je k sebi poklical dva izmed svojih učencev in ju poslal k Jezusu, rekoč: »Ali si ti tisti, ki naj bi prišel? Ali [naj] pričakujemo drugega?«
20 Wale watu walipofika kwa Yesu wakamwambia, “Yohana Mbatizaji ametutuma tukuulize, ‘Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?’”
Ko sta moža prišla k njemu, sta rekla: »Janez Krstnik naju je poslal k tebi, rekoč: ›Ali si ti tisti, ki naj bi prišel? Ali [naj] pričakujemo drugega?‹«
21 Wakati huo huo, Yesu aliwaponya wengi waliokuwa na magonjwa, maradhi na pepo wachafu, na pia akawafungua vipofu wengi macho wakapata kuona.
In v tej isti uri je mnoge ozdravil njihovih slabotnosti in nadlog ter od zlih duhov, in mnogim, ki so bili slepi, je dal vid.
22 Hivyo akawajibu wale wajumbe, “Rudini mkamwambie Yohana yote mnayoyaona na kuyasikia: Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa habari njema.
Potem jima Jezus odgovori in reče: »Pojdita svojo pot in povejta Janezu, kakšne stvari sta videla in slišala: kako slepi vidijo, hromi hodijo, gobavi so očiščeni, gluhi slišijo, mrtvi so obujeni, revnim je oznanjen evangelij.
23 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
In blagoslovljen je, kdorkoli se ne bo spotaknil ob mene.«
24 Wajumbe wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
In ko sta Janezova poslanca odšla, je množici začel govoriti glede Janeza: »Kaj ste odšli ven v divjino, da vidite? Trst, ki se maje z vetrom?
25 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari na kuishi maisha ya anasa wako katika majumba ya kifalme.
Toda kaj ste odšli ven, da vidite? Človeka, oblečenega v mehka oblačila? Glejte, tisti, ki so krasno oblečeni in žive prefinjeno, so na kraljevih dvorih.
26 Lakini mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
Toda kaj ste odšli ven, da vidite? Preroka? Da, povem vam in veliko več kakor preroka.
27 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
To je on, o katerem je pisano: ›Glej, svojega poslanca pošljem pred tvoj obraz, ki bo pripravil tvojo pot pred teboj.‹
28 Nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hakuna aliye mkuu kuliko Yohana. Lakini yeye aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana.”
Kajti povem vam: ›Med temi, ki so rojeni iz žensk, ni večjega preroka kakor Janez Krstnik, toda kdor je v Božjem kraljestvu najmanjši, je večji od njega.‹«
29 (Watu wote hata watoza ushuru waliposikia maneno ya Yesu, walikubali kwamba mpango wa Mungu ni haki, maana walikuwa wamebatizwa na Yohana.
In vsi ljudje, ki so ga slišali in davkarji, so resničnost Boga opravičili s tem, da so se krstili z Janezovim krstom.
30 Lakini Mafarisayo na wataalamu wa sheria walikataa mpango wa Mungu kwao kwa kutokubali kubatizwa na Yohana.)
Toda farizeji in izvedenci v postavi so zavrnili nasvet Boga, sami zoper sebe, tako da se mu niso dali krstiti.
31 Yesu akawauliza, “Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Wanafanana na nini?
In Gospod je rekel: »S kom naj torej primerjam ljudi tega rodu? In čemú so podobni?
32 Wao ni kama watoto waliokaa sokoni wakiitana wao kwa wao, wakisema: “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkulia.’
Podobni so otrokom, sedečim na trgu, ki kličejo drug drugemu ter govorijo: ›Piskali smo vam, pa niste plesali; objokovali smo vam, pa niste jokali.‹
33 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali mkate wala hanywi divai, nanyi mkasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
Kajti Janez Krstnik je prišel [in] niti ni jedel kruha niti ni pil vina; vi pa pravite: ›Hudiča ima.‹
34 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nanyi mnasema: ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’
Sin človekov je prišel in jé ter pije; vi pa pravite: ›Glejte, požrešen človek in vinski bratec, prijatelj davkarjev in grešnikov!‹
35 Nayo hekima huthibitishwa kuwa kweli na watoto wake wote.”
Toda modrost je opravičena po vseh svojih otrocih.«
36 Basi Farisayo mmoja alimwalika Yesu nyumbani kwake kwa chakula. Hivyo Yesu akaenda nyumbani mwa yule Farisayo na kukaa katika nafasi yake mezani.
Eden izmed farizejev pa ga je prosil, da bi lahko jedel z njim. In odšel je v farizejevo hišo ter se usedel k obedu.
37 Naye mwanamke mmoja kwenye ule mji, ambaye alikuwa mwenye dhambi, alipojua kwamba Yesu alikuwa akila chakula nyumbani kwa yule Farisayo, akaleta chupa ya marhamu yenye manukato.
In glej, ko je ženska, ki je bila v mestu grešnica, spoznala, da je Jezus sedel v farizejevi hiši pri obedu, je prinesla alabastrno škatlo mazila
38 Yule mwanamke akasimama nyuma ya miguu ya Yesu akilia. Akailowanisha miguu yake kwa machozi yake, kisha akaifuta kwa nywele zake, akaibusu na kuimiminia manukato.
ter jokajoč od zadaj pristopila k njegovim stopalom in njegova stopala začela umivati s solzami in jih brisati z lasmi svoje glave in poljubljala je njegova stopala ter jih mazilila z mazilom.
39 Yule Farisayo aliyemwalika Yesu alipoona yanayotendeka, akawaza moyoni mwake, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua kwamba ni nani anayemgusa, na kwamba yeye ni mwanamke wa namna gani, na ya kuwa huyu mwanamke ni mwenye dhambi.”
Ko je torej to videl farizej, ki ga je povabil, si je rekel sam pri sebi, rekoč: »Če bi bil ta človek prerok, bi vedel, kdo in kakšne vrste je ta ženska, ki se ga dotika, kajti grešnica je.«
40 Yesu akanena akamwambia, “Simoni, nina jambo la kukuambia.” Simoni akajibu, “Mwalimu, sema.”
In Jezus mu odgovori ter reče: »Simon, nekaj ti imam povedati.« On pa reče: »Učitelj, povej.«
41 “Palikuwa na mtu mmoja aliyewakopesha watu wawili fedha: Mmoja alidaiwa dinari 500na mwingine dinari hamsini.
»Bil je nek upnik, ki je imel dva dolžnika. Eden mu je bil dolžan petsto denarjev, drugi pa petdeset.
42 Wote wawili walipokuwa hawawezi kulipa, aliyafuta madeni yao wote wawili. Sasa ni yupi kati yao atakayempenda yule aliyewasamehe zaidi?”
In ko nista imela nič, s čimer bi plačala, jima je obema odkrito odpustil. Povej mi torej, kateri izmed njiju ga bo bolj ljubil?«
43 Simoni akajibu, “Nadhani ni yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi.” Naye Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
Simon je odgovoril in rekel: »Domnevam, da tisti, ki mu je več odpustil.« On pa mu je rekel: »Pravilno si presodil.«
44 Kisha akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, “Je, unamwona mwanamke huyu? Nilipoingia nyumbani mwako, hukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini huyu ameninawisha miguu kwa machozi yake, na kunifuta kwa nywele zake.
In obrnil se je k ženski ter rekel Simonu: »Vidiš to žensko? V tvojo hišo sem vstopil, pa mi nisi dal vode za moja stopala, toda ona je moja stopala umila s solzami in jih obrisala z lasmi svoje glave.
45 Hukunisalimu kwa busu, lakini huyu mwanamke hajaacha kuibusu miguu yangu tangu nilipoingia.
Nisi mi dal poljuba, toda odkar sem vstopil, ta ženska ni prenehala poljubljati mojih stopal.
46 Hukunipaka mafuta kichwani mwangu, lakini yeye ameipaka miguu yangu manukato.
Moje glave nisi mazilil z oljem, toda ta ženska je moja stopala mazilila z mazilom.
47 Kwa hiyo, nakuambia, dhambi zake zilizokuwa nyingi zimesamehewa, kwani ameonyesha upendo mwingi. Lakini yule aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo.”
Zato ti pravim: ›Njeni grehi, ki jih je mnogo, so odpuščeni, ‹ kajti veliko je ljubila, toda komur je malo oproščeno, ta malo ljubi.«
48 Kisha akamwambia yule mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa.”
Njej pa je rekel: »Tvoji grehi so odpuščeni.«
49 Lakini wale waliokuwa wameketi pamoja naye chakulani wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani ambaye hata anasamehe dhambi?”
In tisti, ki so pri obedu sedeli z njim, so v sebi začeli govoriti: »Kdo je ta, da tudi grehe odpušča?«
50 Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”
In ženski je rekel: »Tvoja vera te je rešila, pojdi v miru.«

< Luka 7 >