< Luka 7 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kusema haya yote watu wakiwa wanamsikiliza, akaingia Kapernaumu.
Dăpă aja če tot azăs alu naroduluj, Isusu apljikat ăn trg Kafarnaum.
2 Mtumishi wa jemadari mmoja wa Kirumi, ambaye bwana wake alimthamini sana, alikuwa mgonjwa sana karibu kufa.
Ănklo afost njeki kapetan alu rimuluj karje avut argat karje avut d jel milă. Ăla argat afost bulnav p muartje.
3 Jemadari huyo aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee wa Kiyahudi kwake, wakamwomba aje kumponya mtumishi wa huyo jemadari.
Kănd kapetanu auzăt d Isusu, atrimjes la jel vođe alu lumjaja karje irja Židovurj ăn trgula s l ruađje s vije š s likujaskă p argatu aluj.
4 Wale wazee walipofika kwa Yesu, wakamsihi sana amsaidie yule jemadari wakisema, “Mtu huyu anastahili wewe umfanyie jambo hili,
Kănd jej avinjit la Isusu, mult la rugat: “Zaslužăt s ji fač aja
5 kwa sababu analipenda taifa letu tena ametujengea sinagogi.”
daja če vrja p narodu alu nostru, frzdă jel noj nam putja s sagradim sinagoga anuastră.”
6 Hivyo Yesu akaongozana nao, lakini alipokuwa hayuko mbali na nyumbani, yule jemadari akatuma rafiki zake kumwambia Yesu, “Bwana, usijisumbue, kwani mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu.
Isusu apljikat ku jej. Š kănd avinjit la upruapje la kasă, atrimjes kapetanu p ortači la Isusu. Jej azăs: “Kapetanu azăs asta: Domnulje, nu tu mučja. K nu sănt vrjedan s uncăr ăn kasa amja.
7 Ndiyo maana sikujiona hata ninastahili kuja kwako wewe. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona.
Nu sănt vrjedan s viuv pănla tinje. Njego samo zi dundje god ješt s s likujaskă argatu alu mjov.
8 Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”
Asta štiuv k š jo mora s askult p kapetanu alu mjov. Am š jo vuastje dusu minje. Š zăk alu unu: ‘Fuđ!’ š jel pljakă. Š alu altuluj zăk: ‘Vină aiča!’ š jel vinje. Š alu argatu alu mjov zăk: ‘Făj aja!’ š jel fače.”
9 Yesu aliposikia maneno haya, alishangazwa naye sana. Akaugeukia ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akawaambia, “Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli.”
Kănd auzăt aja, sa mirat Isusu š sa okrinit la mulc lumje karje apljikat dăpă jel š zăče: “Istina je, ăn Izrael na găsăt p unu Židov karje krjadje kašă ăsta karje nuje Židov karje aša krjadje.”
10 Nao wale watu waliokuwa wametumwa kwa Yesu waliporudi nyumbani walimkuta yule mtumishi amepona.
Kănd sa tors akas ălja p karje kapetanu atrimjes, angăsăt p argatu likujit.
11 Baadaye kidogo, Yesu alikwenda katika mji mmoja ulioitwa Naini. Nao wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu walikwenda pamoja naye.
Dăpă aja Isusu apljikat ăn trg karje s kima Nain. La sljedit učenikurlje aluj š mulc lumje.
12 Alipokaribia lango la mji, alikutana na watu waliokuwa wamebeba maiti wakitoka nje ya mji. Huyu aliyekufa alikuwa mwana pekee wa mwanamke mjane. Umati mkubwa wa watu wa mji ule ulikuwa pamoja na huyo mwanamke.
Kănd avinjit la upruapje la uša alu trguluj, baš atunča njeka lumje aduče p mort fălkov dăn trg pănla gruapă s l ăngruapă. Fălkovu karje amurit afost jedinac la mamă, karje afost udovică, š mulc lumje dăn trg irja ku ja.
13 Bwana Yesu alipomwona yule mjane, moyo wake ulimhurumia, akamwambia, “Usilie.”
Kănd Domnu Isusu avizuto ja fost žau d ja š ja zăs alu je: “Nu plănđa!”
14 Kisha akasogea mbele akaligusa lile jeneza na wale waliokuwa wamelibeba wakasimama kimya. Akasema, “Kijana, nakuambia inuka.”
Avinjit š adotaknit nosiljilje, a lumja karje la dučja astat. Isusu azăs: “Fălkovulje, c zăk, skual!”
15 Yule aliyekuwa amekufa akaketi akaanza kuongea, naye Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
Š fălkovu sa drikat š arubit, a Isusu azăs alu mumusăj: “Jakăc kupilu alu tov”.
16 Watu wote wakajawa na hofu ya Mungu, nao wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea miongoni mwetu, Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.”
Toc sa mirat la săla alu Dimizovuluj. L slavja š zăča: “Marje proroku trijaštje ăntră noj! Dimizov avinjit s ažută alu narodu aluj!”
17 Habari hizi za mambo aliyoyafanya Yesu zikaenea Uyahudi wote na sehemu zote za jirani.
Š toc ăntră Židovj š ăn altje lokurj auzăt aja če Isusu afukut.
18 Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakamweleza Yohana mambo haya yote. Hivyo Yohana akawaita wanafunzi wake wawili
Učenikurlje alu Ivan arubit alu Ivan d tot aja če Isusu afukut. Ivan akimat p doj učenikurj aluj
19 na kuwatuma kwa Bwana ili kumuuliza, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
š lja trimjes la Domnu Isusu s l ăntrjabje: “Ješt tu ăla karje Dimizov aobečit k osă vije ili dal trjebje s štiptăm p altu s vije?”
20 Wale watu walipofika kwa Yesu wakamwambia, “Yohana Mbatizaji ametutuma tukuulize, ‘Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?’”
Kănd jej avinjit la Isusu, azăs lumjaja: “Ivan karje bătjază atrimjes p noj la tinje s t ăntribăm: ‘Ješt tu ăla karje Dimizov aobečit k osă vije ili dal trjebje s štiptăm p altu s vije?’”
21 Wakati huo huo, Yesu aliwaponya wengi waliokuwa na magonjwa, maradhi na pepo wachafu, na pia akawafungua vipofu wengi macho wakapata kuona.
Pănd jej afost ănklo, Isusu alikujit p mulc d buală, d patjală š d sufljeti alji rovj. Š alikujit p multă lumje karje vorbj s puatje s vjadă.
22 Hivyo akawajibu wale wajumbe, “Rudini mkamwambie Yohana yote mnayoyaona na kuyasikia: Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa habari njema.
Atunča aodgovorit alor: “Fuđic š javic alu Ivan ča vizut š auzăt: vorbi vjadje, lumja karje nu puatje s umblă akuma umblă, lumja karje avut buală p pjalje, akuma je likujic, surdi audje, morcă s skuală, š alu săračilor s rubjaštje Bună vorbă d Dimizov.
23 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
Blagoslovit ăla karje nu kadje ăn vjeră dăn minje.”
24 Wajumbe wa Yohana walipoondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
Kănd apljikat učenikurlje alu Ivan, Isusu ančiput s rubjaskă alu multă lumje d Ivan. Jel azăs: “Aspljikat ăn lok undje nuje nimika. D karje om aspljikat ănklo s vidjec? Dal aspljikat s vidjec p njeko karje kašă trstika karje văntu uljigăna? Nu! Nas pljikat aja s vidjec.
25 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari na kuishi maisha ya anasa wako katika majumba ya kifalme.
Ili aspljikat s vidjec p omu karje măndru ănbrăkat? Nu! K lumja karje aduče măndrje cualje š trijaštje ăn bugacije s nalazaštje ăn palače alu caruluj.
26 Lakini mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
Aspljikat s vidjec p proroku? Da! Jel je maj marje prorok.
27 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
Ivan je ăla d karje je skris ăn Svăntă pismă: ‘Jakă, trimjet p omu karje duče vorba amja s pljače la intja ata s pripremjaskă drum d tinje.’
28 Nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hakuna aliye mkuu kuliko Yohana. Lakini yeye aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana.”
Punjec binje urjajke: d tuată lumje karje ikad atrijit nimilja nuje maj marje d Ivan. A ipak, ăn cara alu Dimizov, ăla karje je maj mik je maj marje d jel.”
29 (Watu wote hata watoza ushuru waliposikia maneno ya Yesu, walikubali kwamba mpango wa Mungu ni haki, maana walikuwa wamebatizwa na Yohana.
Tuată lumja karje apus urjajke la Isusu, čak š carinikurlje, već askultat poruka alu Ivan š p jej jel lja bătizat. Atunča, kănd jej auzăt če Isusu azăs, sa složăt k Dimizov zaista atrimjes p Ivan s kjamje p narodu s s pokajaskă.
30 Lakini Mafarisayo na wataalamu wa sheria walikataa mpango wa Mungu kwao kwa kutokubali kubatizwa na Yohana.)
Naprotiv, farizeji š učitelji alu zakonu alu Mojsije aodbit planu alu Dimizov d jej daja ča odbit s lji bătjază Ivan.
31 Yesu akawauliza, “Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Wanafanana na nini?
Isusu azăs: “A ku činje s lji usporidjesk p lumja ăn asta vrijamje? P činje samănă?
32 Wao ni kama watoto waliokaa sokoni wakiitana wao kwa wao, wakisema: “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkulia.’
Jej je kašă kupi karje šadje la tržnică š unu p alt s strigă: ‘Noj amkăntat vuavă vjasăl kăntič š voj na žukat! Noj amkăntat vuavă tužne kăntič a voj na plăns!’
33 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali mkate wala hanywi divai, nanyi mkasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
K, avinjit Ivan karje bătjază na mănkat mălaj nič vin na but, a zăčec: ‘Ăn jel je sufljetu alu rov!’
34 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nanyi mnasema: ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’
Jo, Bijatu alu Omuluj, avinjit karje amănkat š ambut, a zăčec: ‘Jakă, omu karje vrja mult s mălănče š s bja mult vin, ortaku alu carinikuluj š ku grešnikurlje!’
35 Nayo hekima huthibitishwa kuwa kweli na watoto wake wote.”
Toc karje prihvatjaštje mudrost alu Dimizov razumjaštje k Dimizov atrimjes š p minje š p Ivan.”
36 Basi Farisayo mmoja alimwalika Yesu nyumbani kwake kwa chakula. Hivyo Yesu akaenda nyumbani mwa yule Farisayo na kukaa katika nafasi yake mezani.
Unu farizej akimat p Isusu s mălănče ku jel. Jel auntrat ăn kasă alu farizej š alat loku la astal s mălănče.
37 Naye mwanamke mmoja kwenye ule mji, ambaye alikuwa mwenye dhambi, alipojua kwamba Yesu alikuwa akila chakula nyumbani kwa yule Farisayo, akaleta chupa ya marhamu yenye manukato.
Afost njeka mujarje, kunuskută ăn trgula p grešala alu je. Ja adoznajit k Isusu mălănkă la farizej ăn kasă. Š jakă, mujarja adus skumpă ulje karje miruasă ăn măndru bukal.
38 Yule mwanamke akasimama nyuma ya miguu ya Yesu akilia. Akailowanisha miguu yake kwa machozi yake, kisha akaifuta kwa nywele zake, akaibusu na kuimiminia manukato.
Š astat la pičuarje dăpă Isusu. Ančiput s plăngă š lakrmilje kădja p pičuarje. Ku păru lja frikat, š lja surutat š lji uns ku skumpă ulje karje miruasă.
39 Yule Farisayo aliyemwalika Yesu alipoona yanayotendeka, akawaza moyoni mwake, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua kwamba ni nani anayemgusa, na kwamba yeye ni mwanamke wa namna gani, na ya kuwa huyu mwanamke ni mwenye dhambi.”
Kănd avizut farizej karje akimat p Isusu, agăndit: “Kănd ăsta om zaista arfi prorok, aštija činje je mujarasta karje l dotaknjaštje, k ja je marje grešnică.”
40 Yesu akanena akamwambia, “Simoni, nina jambo la kukuambia.” Simoni akajibu, “Mwalimu, sema.”
P aja Isusu ja zăs: “Šimune, am s c zăk nješto.” A jel azăs: “Učiteljulje, zi!”
41 “Palikuwa na mtu mmoja aliyewakopesha watu wawili fedha: Mmoja alidaiwa dinari 500na mwingine dinari hamsini.
A Isusu azăs: “Doj omurj duguja alu unu om banj. Unu om ja dugujit činč sutje kovanic d arđint, a altu om činzăč.
42 Wote wawili walipokuwa hawawezi kulipa, aliyafuta madeni yao wote wawili. Sasa ni yupi kati yao atakayempenda yule aliyewasamehe zaidi?”
A kum jej na vut dundje s ăntuarkă, alu amiždoj aoprostit datorija. Atunča karje d jej doj maj mult osă l vrja?”
43 Simoni akajibu, “Nadhani ni yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi.” Naye Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
Šimun azăs: “Găndjesk alu ăla karje maj mult oprostit datorija.” Azăs Isusu: “Binje azăs.”
44 Kisha akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, “Je, unamwona mwanamke huyu? Nilipoingia nyumbani mwako, hukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini huyu ameninawisha miguu kwa machozi yake, na kunifuta kwa nywele zake.
Atunča Isusu sa okrinit la mujarje š zăče alu Šimun: “Vjez p asta mujarje? Jo auntrat ăn kasă ata, ali tu nu maj dat apă s spăl pičuarilje, a ja aplăns š lakrmilje alu je akăzut p pičuarje a ja lja asplat š ku păru mi lja frikat.
45 Hukunisalimu kwa busu, lakini huyu mwanamke hajaacha kuibusu miguu yangu tangu nilipoingia.
Nu maj dučukit ku poljubacu, a ja, d kănd jo amuntrat na prestanit s m surutje pičuarilje.
46 Hukunipaka mafuta kichwani mwangu, lakini yeye ameipaka miguu yangu manukato.
Tu nu maj uns kapu ku ulja, a ja ku skumpă ulje karje miruasă auns pičuarilje.
47 Kwa hiyo, nakuambia, dhambi zake zilizokuwa nyingi zimesamehewa, kwani ameonyesha upendo mwingi. Lakini yule aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo.”
Dăče găndješt k ja apokazăt atăta d marje ljubav? C zăk istină: aja je daja če grešala alu je, š akă lja fost multă, afost oprostit. Ăla karje găndjaštje k trjebje aluj ucără s s oprostjaskă, ăla vrja ucără.”
48 Kisha akamwambia yule mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa.”
Atunča alu mujarje azăs: “Zaista, grešala ata cam oprostit.”
49 Lakini wale waliokuwa wameketi pamoja naye chakulani wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani ambaye hata anasamehe dhambi?”
Ălja karje afost ănklo ančiput ăntri jej s rubjaskă: “Činje je ăsta š grešala s oprostjaskă?”
50 Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”
A jel zăče alu mujarje: “Daja čaj krizut, tu ta spasăt! S c dja Dimizov mir pănd plječ!”